Hii mikasa inanipata mimi pekee?

Hii mikasa inanipata mimi pekee?

We Jamaa kilichokuponza ni kulidhika kushika Pesa za Mtu mwingine na kulala nazo ghetto. Ukahisi kama ni zako.
Huwezi kukataa kuwa ulikuwa humpigi ganji. Itakuaje Mtu akupi mshahara halafu uwe umelidhika kama nawe hauli ganji? Hata kama una miradi yako pembeni haiwezekani.

Boss wako anakufikiriaje akikuona una Pikipiki, Grocery na umeoa wakati akupi mshahara?
Ila chief kama ulimsoma dogo between the lines amesema waligawana na dadaye kidogo kilichoachwa na wazazi wao akaanzisha biashara ambayo ilikuwa inasonga fresh na jamaa kabla hajamuajiri alimuona nahiko kidogo chake akiendeshea maisha yake,kuwa na pikipiki sio hoja Tanzania ya leo ukiwa hata na lak7 unapata pikipiki na kama nimemuelewa hata kama angekuwa anachukua faida ya grocery na kununua hiyo chombo ni jambo linalowezekana hofu ingekuwa kama angekuwa na IST au Spacio,huyo kaka yake wa kufikia nae ni mmoja wapo wa maskini tu asiyejua utu wa mtu nini...mtu unayeweza kuzungusha hadi 40mill sio wa kuwa na roho ya kudhulumu yatima kama huyu tena damu yako hata ukijua alikupiga unakausha kiutu uzima ili kuepuka laana watu pesa tunazitafuta tunajua mkuu!
 
Nakushauri achana naye usimpeleke kwenye vya dola wala kwa wazee anza upya kwakuwa it is not too late kuanza upya.
Mkianza vutana utapoteza muda na utasababisha ugomvi mkubwa na alivyo na nafasi serikalini anaweza kukuharibia sehemu kibao
nashukuru mkuu
 
Achana nae huyo kaka yako maana kama ameamua kukudhulumu hata ukimshitaki wapi atakubambikia kesi ya wizi akukomoe zaidi....

Acha kazi kwake endelea na mishe zako, huyo mkeo kama ni mama wa nyumbani basi muweke hapo grocery aendelee kusimamia, wewe chukua hyo pikipiki ingia mtaani kama boda boda ukiongeza kipato huku unatafuta kazi sehemu tofauti tofauti. Mtumainie Mungu na umsamehe huyo dhulumati na utaona Mungu atakavyokuinua mkuu. Usikate tamaa wala kulalamika, pambana kiume utawin tu nafasi bado unayo
ntaufanyia kaz huu ushauri
 
Naomba nikupe ushauli wa tofauti kwa sababu nimeguswa sana, japo Upande wangu sio muoga kama wewe.

Kama upo katikati ya mji hama na mkeo, kapange pembezoni ya mji na ukaanze boda boda maana ni mzoefu katika pikipiki.

Pakia abiria upate pesa ya kula kisha tengeneza mabanda ya kuku wa kienyeji, fuga kuku watano mmoja jogoo mwambie mke awasimamie vizuri.

Endesha bodaboda uku unasoma ramani wapi ufungue banda la chips, na hiyo sehemu utakayo weka banda hakikisha mbeleni unaweza kuongeza supu na chakula.


Tafuta wapemba kaombe kazi bila malipo jifunze, natumaini week moja tu utakuwa umejua kila kitu.

Fanya boda boda jioni saa 12 ingia jikoni tengeneza chips yenye viungo vyote pilipili ukwaju saladi na n.k ukisaidiana na mkeo

Utatoa ajira kwa zaidi ya watu wawili na maisha yatakuwa safi, Utampenda mkeo nae atakupenda, Mwanamke anamtegemea mume kuwa road map so mpe map mwambie ukweli mambo magumu, kama anakupenda mtakuwa wote.

Ukiendelea kuangaika kutafuta suruhu utapoteza time na utalost mpaka pesa ya kunyoa nywele uonekane sio mzima kwenye mabaraza ya wazee shauli yako, nimekupa ushauli kwa sababu njia yako nyepesi sana, sema wewe mzito kufikiri ndio maana huna direction yako.
 
Mijitu mingine bwana ina roho mbayaa mpaka unajiuliza kwann wanaendelea kuishi,.anyway hiyo kazi mliandikishiana(mkataba)au mlifanya ki-undugulization!???

Kama mliandikishiana fuata sheria,ikiwezekana umsh'taki kwa kutaka kwenda kinyume na makubaliano na kutaka kukudhulumu

Kama mlifanya kiundugu,basi kuwa mpole achana nae kung'uta vumbi songa mbele,anza upyaa,pambana japo inaumiza lakini heri nusu shari kuliko shari kamili.

Mungu akutie nguvu.
 
Bro life is full of opportunities achana na huyo bro wako tapeli. Ukikubali kuruhusu akili yako iamini huwezi toboa bila hio hela unayomdai bro utafeli sana,je asipokupa ndo maisha yataishia hapo?Kumbuka wewe na huyu mpenz wako mnaweza kuunda team ya kujikwamua na hali ngumu mlionayo sasa.Tumia resources ulizonazo sasa mfano kamata bodaboda yako kula vichwa huku ukiwa na malengo ya kukusanya mtaji ili umfungulie mkeo biashara.Kwa kufanya hivyo utajikuta unarudi kwenye reli.Nikukumbushe mafanikio hayaji kama mvua yatachukua muda utafanikiwa tu.Katika kufanya hayo mtangulize Mungu na usisahau kutoa fungu la kumi kwa unachoingiza ktk biashara zako.Wakati mwingine tunapoteza mali,fedha na kazi kwa kuwa tunamwibia Mungu kwa kutokumtolea zaka na sadaka ya shukrani na mungu huamua kuchukua mibaraka yote na kukuacha ktk majaribu.Mrudie mungu wako hakika hatakuacha ktk shida yoyote ile
 
ndugu yangu chuma kimekaza mpaka huku mtaani kwetu kuna dada ana mimba analaamika kila siku anadai mimba sio yake wamemsingizia, sasa endelea kumchekea huyo kaka yako wa ukoo
 
Sijaona mkasa wowote hapo.
Kama kufiwa na wazazi kila mtu anafiwa.
Malimbikizo ya mshahara mbona kitu cha kawaida sana.

Jeshi linakuita unakataa kwenda.
Unamaliza Chuo unapata ajira una iacha.
Unalala na Milioni 40 ghetto halafu unalalmika kutapeliwa.
Pompoma fala kabisa wewe.
 
ndugu mizinguo huwez kufanikiwa kwa kufanyanya shughuli na ndugu,mm kuna jamaa yangu ndugu zake wamemlostisha na degree yke,next time kuwa makini ndugu wanakutmia kama ngazi tu.ushauri husimshtaki maana bdo atabaki ndugu yako milele kikubwa kumueleza ukweli wako wa ugumu unaoupata ikishindikana tumia ndugu aliyekaribu naye mweleze matatizo na shida ulizopitia ili yeye amweleze alichafanya sio sahiii anaweza kuelewa kwa kipitia uyo MTU au itisha kikao cha ukooo eleza ili mlitatua ndani kwanza badala ya kupelekana polisi ,pesa zinaisha makini udugu upo milele
 
Sijaona mkasa wowote hapo.
Kama kufiwa na wazazi kila mtu anafiwa.
Malimbikizo ya mshahara mbona kitu cha kawaida sana.

Jeshi linakuita unakataa kwenda.
Unamaliza Chuo unapata ajira una iacha.
Unalala na Milioni 40 ghetto halafu unalalmika kutapeliwa.
Pompoma fala kabisa wewe

aisee!!! mda mwingine sio lazima ufikie hatua hio
 
Duh. Acha hapo,nenda katafute ajira ufanye,kwa maana ukimtegemea yeye utadharirika mjini hapa.
 
Hiyo biashara ya grocery achana nayo fanya biashara Mungu anapenda na atakuinua usisahau achana nayo ni uwakala wa shetan
 
Mtu na elimu yako kwann unga'ang'nie hapo, kwanza ulifanya kosa una mafunzo ya kijeshi mazuri unazubaa mitaani, ulikua pale pale ulipopata mafunxo uingie jeshini badae ungechukua degree kaxini na kupandishwa cheo na mshahara mzuri, nakushangaa sana mtu na elimu yako na ujuzi wako unamrumikia mtu anakuzoritesha hapo nawe unakubali, swala la ndoa sio baya mana umejikinga na zinaa, ilo huyo jamaa co poa kwako, mrejeshee kampuni yake, nawe pambana na hali yko kivyako
 
Kazi za ndugu mi nilishasema sitaki hata kuziskia sembuse kufanya!sijui kwanini ndugu ndio huwa wabaya kuliko watu baki
 
Back
Top Bottom