Hii la mahakama ya kadhi limekaaje?

Hii la mahakama ya kadhi limekaaje?

Status
Not open for further replies.
hiyo peleka msikitini wala sio la serikali maana serikali ni ya wote yaani wala nguruwe na wasiokula nguruwe hivyo hilo limekaa zaidi kidini
 
...kaka wanasiasa pia wana mawakala wao miongoni mwetu ambao ni wengi katika maimamu na masheikh wetu...! lazima tuwaambie mbele ya nyuso zao kwamba "sisi waislam tunataka siasa ya kiislamu, na si uislam wa kisiasa"...!....ktk nchi yetu, waislam kwa umoja wetu, hatutakuwa na matatizo na serikali wala wenzetu wasiokuw waislam kama tu, tutasimama katika siasa ya kiislam, na kuachana na uislam wa kisiasa ambao tunaushuhudia miongoni mwa "wanasiasa na vibaraka wao ktk misiki yetu".....!

Mwanajamvi samahani,siasa ya kiislam ni ipi?
 
Unafiki kitu kibaya sana.Yaani wanataka mahakama ya kadhi kwenye ndoa na mirathi tu?Nataka kuona mahakama inawapopoa mawe waasherati mpaka wafe,wazinzi nao wale mboko mpaka wajinyee,vibaka wakatwe mikono mpaka wawe vikatuni hapo ndo nitajua kweli SHARIAH inafanya kazi.Hizi mahakama za kadhi kama zinafuata shariah nusu nusu ni unafiki tu na hazina maana yoyote.
 
mambo yote yanafanyka kama ALLAH alivyo kadiria mahakama ya kadhi muda wake ukifka tuta ipata tu. assalam alykum



mimi siione hasara ya kutokua na mahakama yakadhi wala siioni faida ya kuwa nayo....
-mie hainiletei ajira, wala hainisomeshei mtoto wala kunipa msosi!1
tupate katiba yenye kuleta maandeleo kwa kila mtanzania hilo ndo la msingi
 
....kaka na dada zangu ktk imani ya kiislamu..! tumeshagawanyika mno! wanasiasa na viongozi wetu wameshatugawa mno! ukikaza jicho "usawa wa kati, mbele", utaona kuzungumzia mahakama ya kadhi ktk katiba ni fimbo ya kisiasa inayotumiwa na wanasiasa (naam!) na vibaraka wao waliojivika uimamu, na usheikh kuchapiana kwa sababu za kisiasa zaidi!...la msingi hapa ni moja tu!...TUNAIHITAJI KWA DHATI KABISA MAHAKAMA YA KADHI?...kama jibu ni: "Naam..tunaihitaji", basi na tuiunde wenyewe! hatuwezi shindwa!..lkn (1:LAKINI 2:LAKINI 3:LAKINI)...sisi wenyewe tunayoihitaji, tuwe na imani thabit ktk "emaan", na insha allah, ktk mahakama, na mahakimu wake na hukumu, na maamuzi yatakazokuwa yakitolewa katika mahakama hizo...kisha tuone...yule atakaedharahu......na sisi (KATIKA UMOJA WETU WA KIIMANI KTK HILI) tutamfanya mfano "KIMAKWELIKWELI"....

Issue si kulipia tu. Mahkama hii iwe na nguvu kisheria..kwamba ikishahukumiwa then si ruhsa kwenda kukata rufaa kwenye mahkama nyingine. Ndio maana ikawa kuna haja ya kuwekwa kisheria. Tume ya Katiba haijakanusha kama iwepo au isiwepo. Ila hii ni rasimu ya Katiba ya Muungano na mahakama ya Kadhi si issue ya Muungano..kwa kuwa Zanzibar tayari ipo.


''Ndugu wananchi,
Jambo la pili ni mahakama ya kadhi. Tume ilipokea maoni mengi kuhusu suala hili. Baadhi ya wananchi walitaka mahakama ya kadhi iingizwe kwenye Katiba na wengine walipinga. Baada ya kuamua kuwa Muundo wa Muungano uwe wa Serikali Tatu, Tume iliona kuwa Mahakama ya Kadhi siyo suala la Muungano na imeliacha ili lishughulikiwe na Washirika wa Muungano.
Hata hivyo ilionekana kuwa suala siyo kuwapo au kutokuwapo kwa mahakama ya kadhi. Mahakama hizo zinaweza kuwapo bila ya kuwa katika Katiba. Zanzibar kuna mahakama ya kadhi bila kuingizwa kwenye Katiba ya Zanzibar. Kwa kutumia uzoefu huo hata Tanzania Bara inaweza kupata ufumbuzi wa suala hili.''


Hivi ndivyo Tume ilivyotamka..though it sounds as technical na kama njia za kupoza Waislamu ili wasiriakti otherswise..na hata kina Sheikh Ponda wakija juu hivi ndivyo ambavyo watajibiwa....hasa pale iliposema kama jambo hili litashughulikiwa na washirika wa muungano..(here being the case..Serikali ya Tanzania Bara)..kwa kuwa kutakuwa na Serikali tatu.

Nakumbuka kuna issue ya Uraia wa nchi mbili wamejibu hivyo hivyo kuwa inaweza kujadiliwa kwenye Serikali husika. Hivyo basi kutiana ndimu na hamaki kwa lengo la ku-provoke sidhani kama inasaidia sana. Judge Warioba na wajumbe wake bado wanaheshimika sana..na kazi waliyoifanya ni ya kupongezwa..sidhani kama waliongozwa na Askofu Pengo katika kutoa rasimu hii kama wachangiaji wengi wanavyojaribu kufikiri. This issue is very delicate and thus it needs to be handled with extra care.

Kwemwale.
 
Serikali inachukua mpaka kodi za nguruwe, pombe, sigara, gesti, umalaya, sasa hizi zinafaa kulipia mahakama ya kadhi?
Mbona mnataka hela kharam!
 
Hili la mahakama ya kadhi limekaaje mbona tulihamasishana sana lakini kwenye rasimu ya katiba limekwepwa

Kwa sasa mimi naona suala kubwa litakuwa kwenye serikali ya tanganyika... hapo ndipo penye shoka kukatika mpini... i can see the watu wanavyotunisha misuli kwenye serikali ya tanganyika... yaani ccm hapo ndio inaweza kupiga bao... nawaonya kuwa macho yote yawe kwenye serikali ya tanganyika itakayoongoza watu mil 43.... rais wa tanganyika atakuwa na nguvu kuliko wa jamhuri... bunge la tanganyika litakuwa na ushawishi mkubwa kuliko na hata la jamhuri... tanganyika itakuwa na wabunge wangapi? mawaziri wangapi? raisi atakuwa nani? toka chama gani? naam hapa sasa ndio kazi ipo.... tujipange
 
Acheni hizo...Serikali haina dini, na suala hilo liko katika Katiba! Kama ni Mahakama ya Kadhi anzisheni wenyewe!
Tatizo lenu mlidhani kwa vile top layer ya uongozi wa sasa ni wa dini yenu basi mtaundiwa hiyo Mahakama! Tukiweka udini ndani ya katiba, Waislamu wadai Mahakama ya Kadhi. Wakristu watadai Mahamaka yao, Wapagani nao watadai Mahakama yao, nk. Tutaipeleka wapi Tanzania yetu?!
 
Huo ndo udini tusioutaka.
Hiyo haikuwa rasimu ya kidini.
Kila dini ijiwekee utaratibu wake wa kiuongozi bila kuihusisha katiba ya nchi
 
washirika wa Muungano wameona halifai kuwekwa kwenye katiba
 
Huo ndo udini tusioutaka.
Hiyo haikuwa rasimu ya kidini.
Kila dini ijiwekee utaratibu wake wa kiuongozi bila kuihusisha katiba ya nchi

Niliwai kusikia mawaidha kwenye Msikiti wa Mtambani Kinondoni, wakihamasishana kuwa wahakikishe madai yao yanashughulikiwa kabla Kikwete hajamaliza muda wake, kwasababu hawajuai Rais ajaye atakuwa wa dini gani.
 
Waislamu walishiriki katika kutoa maoni kuhusu kurejeshwa Mahakama ya Kadhi lakini hakuna aliyetegemea kuwa Warioba atatupa Mahakama ya Kadhi!

Ninachotaka kusema ni kuwa hakuna jipya! ilitegemewa na Waislamu kuwa suala la Mahakama ya Kadhi litatupwa, lakini kama wasemavyo wazungu There is always plan B.

Serikali haina dini
 
Mahakama ya kadhi imeshaanza kazi nchini lakini waislamu wa mlengo wa PONDA wanapinga mahakama hiyo kuwa chini ya BAKWATA ambayo tayari imeteua kadhi mkuu na makadhi wa mikoa kwa maelezo kwamba BAKWATA ni chombo cha serikali lakini hao hao wanataka mahakama ya kadhi iwe chini ya serikali.

Hapo nimepapenda ,ila pananichanganya kidogo,nipambanulie kidogo sir
 
Mahakama ya kadhi siyo ishu ya kitaifa. kuwepo kwake ni juhudi za waislamu na wala sio tume ya katiba. Na kuchinja je?
 
Hili la mahakama ya kadhi limekaaje mbona tulihamasishana sana lakini kwenye rasimu ya katiba limekwepwa


Katika mambo ambayo tume ilifanya vizuri ni kutupilia mbali hoja ya ofisi ya kadhi kuwa serikalini.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Niliwai kusikia mawaidha kwenye Msikiti wa Mtambani Kinondoni, wakihamasishana kuwa wahakikishe madai yao yanashughulikiwa kabla Kikwete hajamaliza muda wake, kwasababu hawajuai Rais ajaye atakuwa wa dini gani.

Basi wameula wa chuya,Maana hata wakihamasishana kuipinga hii Rasimu ya Katiba,Kikwete mwenyewe kabakiza miaka miwili,Kwa maana hiyo ataiacha Katiba ya zamani.Kama ni Mchakato mwingine utafanywa na Rais mwingine ambae anaweza akashawishi hata neno "MAHAKAMA YA KADHI" lisijitokeze kwenye Rasimu maana ni UDINI pasee.
 
Nafas bado unayo kuanzia sasa,ila nakutahadharisha kuwa si kila kiongelewacho kwenye kampeni lazma kiwe kweli.
 
mbona Kenya iliwezikana kuwekwa kwenye katiba?

Kwani sisi wakenya. Kila kitu kenya hivi mitanzania mingine ikoje...,kwani jirani yako akila mavi na wewe lazima uige? Mahakama ya kadhi ni kama kula mavi
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom