Hii kwangu imekuwa changamoto kubwa. Hata natamani kukimbia home

Chizi Maarifa

JF-Expert Member
Jul 29, 2013
10,471
23,744
Habari! Mimi nmejenga sehemu moja hapa Dar kms 16 kufika Posta kwenye Mnara wa Askari. Nachelea kusema ni mbali na Jiji au si mbali sana.

Kiwanja nilinunua kikubwa sana.of course Mzee alitununulia miaka hiyo ya 90s then nami nikaja ongezea so nina eneo la kutosha hasa. Nmejenga na nimepata sehemu ya kupanda miti miwili mitatu ya matunda.

Nina migomba, michungwa,miembe mbegu fupi,makoma manga,mipapai mbegu fupi na migomba.

But pia nina kaeneo ka bustan so wanalima kiasi mboga mboga na mapassion.

Eneo lote nimezungushia.nmezungushia kwa ukuta mrefu sana na kuacha kidogo tu kwa mbele ili kupitisha hewa.

Shida inayonifanya nianze kuchukia hapa home ni wadudu. Nimeshaambiwa mara mbili pameonwa na kuuliwa nyoka wa kijani.

Mimi ni NYOKAPHOBIA na WADUDUPHOBIA. Nipo tayari kupambana na mbwa lakini si wadudu.

Nakumbuka mwaka flani nikiwa chuo nlienda panga sehemu moja Msewe ukipita lile gate la Chuo kama unaelekea Changanyikeni. Nlihama ndani ya mwezi mmoja nikaacha chumba na kodi sababu ya uwepo wa Tandu na Nge wengi eneo lile.

Nlijikuta nashindwa kulala au kukaa room.sikuwa na amani kabisa.nlitafuta dawa nyingi mpaka nilikuja pata flani ambayo kidogo nami iniue.ile dawa ilikuwa unapulizia. Sikuwa nimeziba pua.ilikuwa ina hewa kavu na yenye kukaba kiasi kwamba ukipuliziwa ndani ukafungiwa unakufa.ilikuwa kavu sana na inakata pumzi huwezi vuta.

Nikaamua kuhama. Mimi binafsi hata mende mkubwa akiwa room kama hajatolewa (sipendi auliwe ndani) siwezi lala. Au nimwone mjusi wale wanaopenda kukaa ndani.siwezi pata amani mpaka atolewe (na sipendi auliwe pia)

Hili tatizo sielewi maana ikinyesha mvua hata kumbikumbi sipendi waniguse.napata shida sana. Kifupi sipendi mdudu yoyote around me.

Nyoka hata awe amekufa sipendi mwona au itokee nimguse.sipendi nyoka awe wa rangi yoyote ile.mweupe,mwekundu,njano,kijani au blue. Ni kwamba sipendi nyoka.

Lakini ukinambia kuna sehemu kuna mbwa mkali huyo wala haniogopeshi.nimetembea porini kwenye wanyama wakali sana na wakutisha sikuwa naogopa hata kidogo.ila nambie tu kuwa room kwao nmeona nge au tandu. Sitolala mpaka apatikane atolewe.

Nimeshawahi kimbiza fisi porini mara mbili nikiwa na panga,nmewahi kimbiza duma nikiwa na panga na mkuki. Lakini siku hiyo nmemkimbiza duma nmerudi kwenye tent jamaa yangu akasema amemwona mjusi kafiri kaingia kwenye tent yangu sikufunga vizuri zip. Sikulala.

Najaribu kuwaza nifanye nini kuepukana na hali hii ya kuogopa wadudu lakini pia kwa hapa home nazuiaje kabisa nyoka na wale mijusi wasikanyage kabisa home. Maana naanza kukosa amani.na binafsi sipendelei kwenda ishi kwenye maghorofa kule upanga,mikocheni n.k
 
Kama umezungushia ukuta ni vzr.. chukua Oil chafu.. mwaga chini kuzunguka nyumba.

Pili Tumia Dawa kali ya Fumigation puliza miti na vichaka vyote.

Unaogopa mende... Hehe last week nilivyokuw MAPORINI nimelala na TANDU mweusi kitandani kilichonishtua ni zile sharubu zake alikuw ananigusa gusa maskioni.. nikawasha Taa nilizan ni mdudu tu wa Kawaida nikamkuta Tandu.. so ni vitu vya kawaida.. hapa kwenyewe nishaua KENGE.. mdg lkn alikuwa anasumbua sumbua nje.
 
Dah pole mkuu ila mwanaume kuogopa wadudu kama mende na nyoka ni ajabu sana.

Njia nzuri ya kuzuia wadudu ni pamoja na kuhakikisha kuwa maeneo ni masafi ili kupunguza kuzaliana kwa wanyama kama panya wanaovutia nyoka, pia mazingira masafi yatapunguza wadudu kama mende na mbu hivyo hata hao mijusi watapungua.

Fumigation mara kwa mara itasaidia pia.
 
Vitu vya kawaida..
 

Attachments

  • IMG_20200408_182519_547.jpg
    IMG_20200408_182519_547.jpg
    136 KB · Views: 9
Mkuu ulimkimbiza duma wap, na huyo fisi wap? , Mbna kama kamba hii umetupiga, tatzo lako hujazoea hao wadudu na hyo ni Kwa sababu umezaliwa town na umekulia hapo town, mbwa huwaogopi c'se umekua ukiwaona unakutana nao unaona jins watu wanavyowatreat so uko aware nao, badlisha mtazamo wa fikra wachukulie Tu hao ni wadudu na jukumu lako ni kuwakabili na ukilegea wanakudhuru ...simple tuu , tofaut na hapo utaendelea kuwa muoga na hao wadudu wenyewe wapo Tu enzi na enzi na hawawez Isha , popote Tu wakiona fursa ya kuishi wanaishi... Kunguni na mbu ndo wadudu ambao sipatani nao kabisa hata kuwaona tuu ila hawaniogopeshi

Usitumie nguvu Sana kutuaminisha et huogopi hata Simba ila ukiona Mende unachora ...
 
Nyoka wa kijani hawanaga madhara,unaweza lala nae ktandani,tuliwah ishi mahala walkuwa weng sana lakin hawakuwah kuleta madhara mwanzo tuliwauwa sana kwa sku tulkuwa tunaua watatu mpaka watano,jamaa mmoja akatueleza kuwa waacheni tu hawana shida mpaka Leo Mimi kama nyoka hayupo ndani hata kama ni wale weusi siwezi kumuua ni dhambi pale hajafanya kosa lolote why umuue
 
Pole sana mkuu kitaalamu phobia yako inaitwa Entonophobia, ni phobia commom sana kuliko zingine. Ni hali inayodevelop taratibu hasa kuanzia utoto. Pengine ulipokuwa mtoto kuna incident ilitokea ukakumbana na mdudu katika hali ambayo hukutegemea na hapo ndio shida ikaanzia.
Njia rahisi ni kuface hiyo hali na kupambana nayo.
Mfano mimi zamani nlikuwa naogopa sana minyoo ile inayotokea baada ya mvua kunyesha, lakini siku moja rafiki yangu akaushika mnyoo tukaenda nae kutega samaki kwa ndoano.
Tangu kipindi hicho siogopi minyoo na wadudu wengine nawashika tu.
 
Mkuu ulimkimbiza duma wap, na huyo fisi wap? , Mbna kama kamba hii umetupiga, tatzo lako hujazoea hao wadudu na hyo ni Kwa sababu umezaliwa town na umekulia hapo town, mbwa huwaogopi c'se umekua ukiwaona unakutana nao unaona jins watu wanavyowatreat so uko aware nao, badlisha mtazamo wa fikra wachukulie Tu hao ni wadudu na jukumu lako ni kuwakabili na ukilegea wanakudhuru ...simple tuu , tofaut na hapo utaendelea kuwa muoga na hao wadudu wenyewe wapo Tu enzi na enzi na hawawez Isha , popote Tu wakiona fursa ya kuishi wanaishi... Kunguni na mbu ndo wadudu ambao sipatani nao kabisa hata kuwaona tuu ila hawaniogopeshi

Usitumie nguvu Sana kutuaminisha et huogopi hata Simba ila ukiona Mende unachora ...
Nadhani umenjibu pasipo kujua undani wa shida husika. Umejibu kishabiki
 
Huku niliko kwangu kuna nyoka sana na kupambana nao ni jambo la kawaida, nilishawahi kung'atwa na kisa nikaleta humu.
Kuna majoka ya kila aina haipiti wiki lazima uwaone au uwaue wawili watatu na mpaka juzi saa moja usiku tumeua joka lenye unene wa tyre ya gari likitoka maeneo yangu na wenyeji wa huku wanaliita Bafe na kusifu kuwa ana sumu kali sana hivyo huua haraka sana.
Mazingira yeyote yanapokutokea usiogope bali jenga ujasiri! Mimi hadi hapa nilipo sasa hivi nimepumzika hapa ndani lakini najua kama sio chini ya kitanda basi nyuma ya makabati kuna nyoka, maana kila baada ya muda nakuta gamba nene jeusi lililo vuliwa na nyoka.
 
Huku niliko kwangu kuna nyoka sana na kupambana nao ni jambo la kawaida, nilishawahi kung'atwa na kisa nikaleta humu.
Kuna majoka ya kila aina haipiti wiki lazima uwaone au uwaue wawili watatu na mpaka juzi saa moja usiku tumeua joka lenye unene wa tyre ya gari likitoka maeneo yangu na wenyeji wa huku wanaliita Bafe na kusifu kuwa ana sumu kali sana hivyo huua haraka sana.
Mazingira yeyote yanapokutokea usiogope bali jenga ujasiri! Mimi hadi hapa nilipo sasa hivi nimepumzika hapa ndani lakini najua kama sio chini ya kitanda basi nyuma ya makabati kuna nyoka, maana kila baada ya muda nakuta gamba nene jeusi lililo vuliwa na nyoka.
Uwiiii yani unasimulia wewe mimi huku natetemeka .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom