charldzosias
JF-Expert Member
- Nov 10, 2013
- 2,448
- 3,334
Unamjua KENGE vzr? Hapa kuna Mifugo mbalimbali unajua wanasababisha HASARA kias gani?Huu ni ukatili dhidi ya viumbe! Umemuua kakukosea nini bro ? Nao wanahitaji kuishi
Unamjua KENGE vzr? Hapa kuna Mifugo mbalimbali unajua wanasababisha HASARA kias gani?Huu ni ukatili dhidi ya viumbe! Umemuua kakukosea nini bro ? Nao wanahitaji kuishi
Kama umezungushia ukuta ni vzr.. chukua Oil chafu.. mwaga chini kuzunguka nyumba.
Pili Tumia Dawa kali ya Fumigation puliza miti na vichaka vyote.
Unaogopa mende... Hehe last week nilivyokuw MAPORINI nimelala na TANDU mweusi kitandani kilichonishtua ni zile sharubu zake alikuw ananigusa gusa maskioni.. nikawasha Taa nilizan ni mdudu tu wa Kawaida nikamkuta Tandu.. so ni vitu vya kawaida.. hapa kwenyewe nishaua KENGE.. mdg lkn alikuwa anasumbua sumbua nje.
Huku kukaa katika sofa na ukaona nyoka kajilaza kwa nyuma ya shingo yako ni kawaida tu, muhimu ni kuondoa hamaki ili usimshtue akajihami.Uwiiii yani unasimulia wewe mimi huku natetemeka .
Anang'ata mkuu hata kama hujamkanyaga ila tu sumu yake sio tishio kama wengine.Nyoka wa kijani hangati kutokana na maumbile ya meno yake, hana meno kwa mbele, meno yake yameanzia katikati ya taya, hivyo kungata mpaka umkanyage na ahangaike kutoka
mzee kwan unaishi kwny hifadhi au kwny makazi ??Huku kukaa katika sofa na ukaona nyoka kajilaza kwa nyuma ya shingo yako ni kawaida tu, muhimu ni kuondoa hamaki ili usimshtue akajihami.
Wa Kawaida mno.. haina haja ya kuwaogopa kuna Hawa na kuna wale Buibui weusi.. naruka nao sana😳😳😳😳😳 tandu kitandani? Hicho chumba ntapata wakati mgumu kushawishiwa kulala tena. Hao wadudu nikimwona tu mwili unasisimka. Napoteza sana.
wanaume wa dar kama kawaida yenuMimi ni NYOKAPHOBIA na WADUDUPHOBIA. Nipo tayari kupambana na mbwa lakini si wadudu.
Hangati kirahisi, we mchunguze meno yake yako mbaliAnang'ata mkuu hata kama hujamkanyaga ila tu sumu yake sio tishio kama wengine.
Ni makazi mapya nyumba zipo mbali mbali na eneo kubwa ni msitu mkubwa.mzee kwan unaishi kwny hifadhi au kwny makazi ??
Naam ni mpaka ahisi hatari.Hangati kirahisi, we mchunguze meno yake yako mbali
Nikaamua kuhama. Mimi binafsi hata mende mkubwa akiwa room kama hajatolewa (sipendi auliwe ndani) siwezi lala.
Usimdanganye kuwa nyoka wa kijani hana madhara. Inategemea ni nyoka gani kwakua nyoka wa kijani wapo wengi ambao ni venomous kama Green Mamba, Boomslang n.kNyoka wa kijani hawanaga madhara,unaweza lala nae ktandani,tuliwah ishi mahala walkuwa weng sana lakin hawakuwah kuleta madhara mwanzo tuliwauwa sana kwa sku tulkuwa tunaua watatu mpaka watano,jamaa mmoja akatueleza kuwa waacheni tu hawana shida mpaka Leo Mimi kama nyoka hayupo ndani hata kama ni wale weusi siwezi kumuua ni dhambi pale hajafanya kosa lolote why umuue
Huku niliko kwangu kuna nyoka sana na kupambana nao ni jambo la kawaida, nilishawahi kung'atwa na kisa nikaleta humu.
Kuna majoka ya kila aina haipiti wiki lazima uwaone au uwaue wawili watatu na mpaka juzi saa moja usiku tumeua joka lenye unene wa tyre ya gari likitoka maeneo yangu na wenyeji wa huku wanaliita Bafe na kusifu kuwa ana sumu kali sana hivyo huua haraka sana.
Mazingira yeyote yanapokutokea usiogope bali jenga ujasiri! Mimi hadi hapa nilipo sasa hivi nimepumzika hapa ndani lakini najua kama sio chini ya kitanda basi nyuma ya makabati kuna nyoka, maana kila baada ya muda nakuta gamba nene jeusi lililo vuliwa na nyoka.
Kuhusu kuzuia nyoka kuja kwako onana na Mama Diamond ama Muha yeyote wa Kigoma, wale ni wachawi wa asili na wanajuwa kuishi na hao wadudu.Habari! Mimi nmejenga sehemu moja hapa Dar kms 16 kufika Posta kwenye Mnara wa Askari. Nachelea kusema ni mbali na Jiji au si mbali sana.
Kiwanja nilinunua kikubwa sana.of course Mzee alitununulia miaka hiyo ya 90s then nami nikaja ongezea so nina eneo la kutosha hasa. Nmejenga na nimepata sehemu ya kupanda miti miwili mitatu ya matunda.
Nina migomba, michungwa,miembe mbegu fupi,makoma manga,mipapai mbegu fupi na migomba.
But pia nina kaeneo ka bustan so wanalima kiasi mboga mboga na mapassion.
Eneo lote nimezungushia.nmezungushia kwa ukuta mrefu sana na kuacha kidogo tu kwa mbele ili kupitisha hewa.
Shida inayonifanya nianze kuchukia hapa home ni wadudu. Nimeshaambiwa mara mbili pameonwa na kuuliwa nyoka wa kijani.
Mimi ni NYOKAPHOBIA na WADUDUPHOBIA. Nipo tayari kupambana na mbwa lakini si wadudu.
Nakumbuka mwaka flani nikiwa chuo nlienda panga sehemu moja Msewe ukipita lile gate la Chuo kama unaelekea Changanyikeni. Nlihama ndani ya mwezi mmoja nikaacha chumba na kodi sababu ya uwepo wa Tandu na Nge wengi eneo lile.
Nlijikuta nashindwa kulala au kukaa room.sikuwa na amani kabisa.nlitafuta dawa nyingi mpaka nilikuja pata flani ambayo kidogo nami iniue.ile dawa ilikuwa unapulizia. Sikuwa nimeziba pua.ilikuwa ina hewa kavu na yenye kukaba kiasi kwamba ukipuliziwa ndani ukafungiwa unakufa.ilikuwa kavu sana na inakata pumzi huwezi vuta.
Nikaamua kuhama. Mimi binafsi hata mende mkubwa akiwa room kama hajatolewa (sipendi auliwe ndani) siwezi lala. Au nimwone mjusi wale wanaopenda kukaa ndani.siwezi pata amani mpaka atolewe (na sipendi auliwe pia)
Hili tatizo sielewi maana ikinyesha mvua hata kumbikumbi sipendi waniguse.napata shida sana. Kifupi sipendi mdudu yoyote around me.
Nyoka hata awe amekufa sipendi mwona au itokee nimguse.sipendi nyoka awe wa rangi yoyote ile.mweupe,mwekundu,njano,kijani au blue. Ni kwamba sipendi nyoka.
Lakini ukinambia kuna sehemu kuna mbwa mkali huyo wala haniogopeshi.nimetembea porini kwenye wanyama wakali sana na wakutisha sikuwa naogopa hata kidogo.ila nambie tu kuwa room kwao nmeona nge au tandu. Sitolala mpaka apatikane atolewe.
Nimeshawahi kimbiza fisi porini mara mbili nikiwa na panga,nmewahi kimbiza duma nikiwa na panga na mkuki. Lakini siku hiyo nmemkimbiza duma nmerudi kwenye tent jamaa yangu akasema amemwona mjusi kafiri kaingia kwenye tent yangu sikufunga vizuri zip. Sikulala.
Najaribu kuwaza nifanye nini kuepukana na hali hii ya kuogopa wadudu lakini pia kwa hapa home nazuiaje kabisa nyoka na wale mijusi wasikanyage kabisa home. Maana naanza kukosa amani.na binafsi sipendelei kwenda ishi kwenye maghorofa kule upanga,mikocheni n.k
Tunatakiwa kujifunza jinsi ya kuishi nao. Uli wao waishi nasi pia tuishi.Unamjua KENGE vzr? Hapa kuna Mifugo mbalimbali unajua wanasababisha HASARA kias gani?