Hii kauli wadau mmeichukuliaje?

Hii kauli wadau mmeichukuliaje?

anashangaza anapofanya maamuzi kwa mafungu ya watanzania ingekuwa mara ya kwanza tungenyamaza lakini yupo sensitive na mwanza manake hao ndio watanzania kuliko wengine wana damu na nyama kuliko wengine uongozi wake wa manati na ni hovyo
Ni kweli mkuu kaamua kukomaa na shinyanga na mwanza yaani kwa ndugu zake wa Damu lakini mikoa mingine wananchi wanaumia Zaidi pasipo Tamko lolote la kukemea Uovu dhidi ya binadamu hata Zanzibar walipora ushindi wa CUF lakini mpaka leo hakuna Tamko zaidi ya Lipumba kugeuza Dili la kujipatia pesa toka CCM.
 
Nakubaliana na wewe huyo juma ponda maharangwe anasema hilo kimtia mama magumi hadi kalazwa hospital habari inafichwa tu
 
Basi kama ni hivyo asingewachagua hao watu yeye makamo na waziri mkuu wakasimamia shoo mpaka mwisho,ilibidi azunguke tena kila kukicha nchi nzima ili kutatua matatizo ya wananchi na sio kujifungia Magogoni vinginevyo ndo maana kateua wasaidizi.
 
Huwezi kuwa mtawala wa kila sehemu upo, kupitia uwakilishi ndiyo unakuwepo kila sehemu kauri zingine za kuwatisha wenye kumwakirisha ili wafuate maagizo. Hili swala mimi nionavyo lingefanyiwa utaratibu kwap maeneo machinga wa mwanza hawawezi kuwa machinga wa mbeya miji itaharibika mingine
 
naweza kutabiri anguko kubwa sana la utawala huu,

nchi imepoteza rslimali nyingi ku~decentralise,anakuja mmoja ana centralise system ya utawala.

Ninachokiona,maamuzi mengi sana katika halmashauri yatachelewa kwa kuwa utabidi wakuu wa mikoa/wilaya/ wakurugenzi nchi nzima wawasiliane na ikulu kwanza.

Maamuzi yakichelewa haimaanishi muda utasimama,2020 iko palepale.

Sasa hivi halmashauri zitaacha kupima viwanja kwa woga wa kuchukua maeneo ya wananchi hata kama wana hela ya kuwafidia,

sasa hivi watu watajikusanya kikundi,watavamia shamba la mtu,watalima,hata kama muhusika ana nyaraka zote za umiliki,zitafutwa,wananchi wanafundishwa kutofata taratibu na sheria.

uhuru wa serikali za mitaa umepotea,uhuru wa kimaamuzi ya wakuu wa wilaya na watendaji umekwisha(sasa huwezi hata kusikia ATCL imekaa na bodi yake kujadili ununuzi wa ndege,ananunua mtu mmoja tu)

Bora hata maamuzi yangekuwa centralised kiserikali huko serikali kuu kwa maana mawaziri,wakuu wa mikoa,watendaji wa taasisi,sasa maamuzi yako kwa MTU mmoja!!

TRA wakiamua,yeye anatengua maamuzi,nini maana ya kuipa uhuru kimaamuzi TRA?

Huyu mtu mmoja ana utaalam wa kila jambo ?jack of all trades?!
 
Basi kama ni hivyo asingewachagua hao watu yeye makamo na waziri mkuu wakasimamia shoo mpaka mwisho,ilibidi azunguke tena kila kukicha nchi nzima ili kutatua matatizo ya wananchi na sio kujifungia Magogoni vinginevyo ndo maana kateua wasaidizi.
Baraza la Mawaziri lenyewe alichelewa sana kulitangaza.

watanzania "tujiombee wenyewe", tuko njiapanda
 
Hakuna jambo lililoumiza nyoyo za watu kama ile bomoa bomoa iliyokuja kuzuiwa na Mahakama Dar. Nikilinganisha na hili la machinga linakuwa "peanut" ila sikumsikia kusema lolote. What's going on with this man!
Mwanza ndio roho yake, ukigusa Mwanza umegusa roho yake. Hao wa Dar wasubiri Raisi wao 2025 huyu Ni wa usukumani
 
Mm naona alichokiongea mkulu ni sahihi cause baadhi ya wateuliwa walianza kuchukua hatua hata zilizo nje ya mamlaka zao kisheria (kutumia madaraka yao vibaya) huku maamuzi wanayofanya wakiwaathiri wananchi moja kwa moja lakini alichokosea ni kutangaza hadharan maana hao wateule bado wanaendelea na kaz hivyo inaweza kupelekea kwa baadae wakitoa matamko au kuchukua hatua mbalimbali katika utendaji kazi hata kama ni halili ama ziko kwenye mamlaka yao kisheria wananchi wakawapuuza kwa kuwa mkulu ameonesha design kama hana iman nao tena
 
Mm naona alichokiongea mkulu ni sahihi cause baadhi ya wateuliwa walianza kuchukua hatua hata zilizo nje ya mamlaka zao kisheria (kutumia madaraka yao vibaya) huku maamuzi wanayofanya wakiwaathiri wananchi moja kwa moja lakini alichokosea ni kutangaza hadharan maana hao wateule bado wanaendelea na kaz hivyo inaweza kupelekea kwa baadae wakitoa matamko au kuchukua hatua mbalimbali katika utendaji kazi hata kama ni halili ama ziko kwenye mamlaka yao kisheria wananchi wakawapuuza kwa kuwa mkulu ameonesha design kama hana iman nao tena
Kwa hiyo alipaswa kuzungumza na wahusika wote ambao wanaenda kinyume na maelekezo yake ama nje ya Sheria waache tabia hiyo ( mazungumzo privately) na sio public, ama kumuagiza waziri mwenye dhamana awaonye ama kuwakumbusha wanapotoka nje ya utaratibu ama kufanya maamuzi ya kukurupuka yanayopelekea wananchi kuumia
 
Maigizo mengi sana sasaivi vitu vya kurekebishana mezani wanaleta kwenye TV kila mmoja anataka sifa mkuu anataka sifa kwa wananchi watendaji nao wanataka sifa kwa mkuu yani nchi inaendeshwa kwa matukio mwanzo mwisho,wengine wanatoa matamko kila kukicha kisa waonekane wanajituma kufanya Kazi hiii sio sawa kupata maendeleo ni ngumu sana maneno mengi vitendo vichache
 
Rais yuko sawa ndo maana nikasema hivi wasaidizi wake waache vihelehele hasa kudhalilisha watumishi wauma
 
Ni sahihi kabisa, unafikiri wale wakurugenzi waliopindua matokeo wanajua uchungu wa waliotoa jasho na mali zao kuzunguka maeneo kutafuta kuungwa mkono na wananchi halafu siku moja tu kiazi mmoja anamtangaza mwingine. Swala la umeya limeleta chuki ya kubwa na itaendelea mpaka mwisho
 
kiongozi wa aina hiyo hana uwezo wa uongozi kama aunachaguwa viongozi wa kukusaidia kwa mujibu wa sharia lazima uwaheshimu kama unawaona hawakufai basi waondoe lakini sio kuwavunjia heshima utadharauliwa na wananchi kweli kabisa

Siyo Tanzania, labda iwe ulaya
 
Yeye ndio wa kwanza kunyooshewa kidole..si unaona hata kushindwa kwa wanasheria wa lema kutafsiri sheria wanachadema wanamlaumu yeye..hata nyumba INA Kiongozi ambaye ni baba au mama..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom