Huyu Lazaro Nyalandu anachofanya sasa hivi ni usanii tu, siku zote alikuwa wapi? Nani alikuwa anamzuia kufanya kazi yake, tumuone eti kacharuka ghafla sasa hivi. Wanasema "life is not a dress rehearsal," ila Lazaro anafanya role rehearsal ili watu wasiokuwa na fikra sahihi wamuone ni mchapa kazi na apewe cheo cha Waziri wa Maliasili na Utalii kuchukua nafasi ya Khamis Kagasheki. Huyu Lazaro naye ni mzigo tu, siku zote alikuwa wapi asichukue hizo hatua. Kazi kuzunguka na media tu kila kona ili aonekani ni waziri jembe.
Kwenye Operesheni Tokomeza naye amehusika, kwani alikuwa ni naibu waziri wa wizara na accountability ni lazima viongozi wote wakuu wa wizara wachukue, siyo waziri tu. Kwa heshima ya roho za wananchi zilizopotea kwenye Operesheni Tokomeza, ni lazima viongozi wafuatao wa wizara ya maliasili na utalii nao watolewe waletwe viongozi wapya:
1. Naibu waziri wa maliasili na utalii, Lazaro Nyalandu.
2. Katibu Mkuu
3. Mkurugenzi wa Idara ya Wanyama Pori
4. Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA