Hii inakaaje, ni halali mtu kuoa shemeji yake.

Dam55

JF-Expert Member
Oct 8, 2015
5,592
11,831
Ni hivi wandugu
Kuna jamaa wetu hapa amejikiuta kwenye matatizo makubwa kifamilia.
Chanzo ni kwamba amempenda mdogo wa mke wa kakayake (kitamaduni zetu ni shemeji yake) huyu binti wamezaliwa tumbo moja na mke wa kakayake ambaye ni brother wake wa damu.

Jamaa anaeleza kuwa walianza mahusiano kitambo na huyo dem tangu wakiwa wanasoma waliahidiana mengi ya kimaisha hasa kuoana, jamaa anakili kuwa huyu dem amemsaidia sana kimaisha hadi kufika hapo alipo.
Jamaa anasema umefika wakati sasa anataka kutimiza ahadi yake ya kumuoa lakini tatizo likaje upande wa wazazi wa binti wamekataa kabisa suala hilo wakidai ni kinyume na mila zao ndugu wawili wa damu kuoa familia moja,

Kwa kweli umekuwa mtafaruku mkubwa huku baadhi wakiunga mkono na wengine wakipinga vikali suala hilo.
Kibaya zaidi imegundulika tayari binti ana mimba ya jamaa.
Binti ametishia kujiua ikiwa ndugu zake wataendelea kushikilia msimamo wao wa kukataa kuolewa na jamaa lakini bado wazazi na ndugu wengine wameendelea kupinga hilo.
Mpaka sasa hali imezidi kuwa mbaya baada ya binti kutoroka kwako na kuhamia kwa jamaa, siku ya pili hii Sasa, wazazi wa binti wametoa onyo kuwa kama hata rudi nyumbani na kuachana na jamaa wao hawata mtambua kama mtoto wao.

Matatizo yamekuwa makubwa hadi sasa familia hazielewani.

Je wandugu hili linakuwaje ni halali kwa watu hawa kuoana na kama sivyo ubaya hasa uko wapi hapa?
Nini kifanyike katika hili na ni kweli kuwa kitamaduni za kwetu hapa TZ kuwa hili haliruhusiwi? Au ni kudhurumu tu nafsi za hawa wapendanao?
 
Kuna kesi kama hii ninaifahamu. Mdogo wa mke wa kike alihamia kwa dada yake ili asome shule ya day Secondary. Mume nae mdogo wake amemaliza form four amekwenda kwa kaka kungonjea majibu.

Wawili hawa walipendana na majibu yalipotoka kijana alikwenda form Five. Binti aliendelea kukaa kwa dada yake mpaka anamaliza shule.

Yule kijana baada ya kumaliza form Six familia ilimpeleka USA kusoma degree. Alijitahidi akamvuta binti.

Sasa wanafamilia na bado wanapendana sana.
 
Watu wanaoana Baba mdogo kwa Baba mkubwa, Shangazi kwa Mjomba au Mama mkubwa kwa Mama mdogo sembuse shemeji hao Wazazi mitambo ya Gongo
 
Watu wanaoana Baba mdogo kwa Baba mkubwa, Shangazi kwa Mjomba au Mama mkubwa kwa Mama mdogo sembuse shemeji hao Wazazi mitambo ya Gongo
Kikabila hawa ni warugulu sijui ndo kweli wanavo dai kuwa kikwao hiyo hairuhusiwi
 
Kuna kesi kama hii ninaifahamu. Mdogo wa mke wa kike alihamia kwa dada yake ili asome shule ya day Secondary. Mume nae mdogo wake amemaliza form four amekwenda kwa kaka kungonjea majibu.

Wawili hawa walipendana na majibu yalipotoka kijana alikwenda form Five. Binti aliendelea kukaa kwa dada yake mpaka anamaliza shule.

Yule kijana baada ya kumaliza form Six familia ilimpeleka USA kusoma degree. Alijitahidi akamvuta binti.

Sasa wanafamilia na bado wanapendana sana.
Sasa hawa huku sijui wana matatizo gani nashindwa kuwaelewa kiukweli.
 
Kama wamependana wajisogeze mkoa wa mbali, wakirudi nyumbani wana watoto wawili familia zitaelewana.
Ata me nna mawazo kama yako ...wakafanye yao then wakirud kutakuwa hakuna namna tena...

Au bora wangekaa kimya kwanza kama uyo binti alielewa uwepo wa mila hzo kwny koo yao
 
Ni complications za kipuuzi tu, Toka lini shemeji akawa ndugu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom