Picha hizi zinaonyesha ni kwa namna gani udhalilishaji ulivyokithiri. Huyu mama ni mama wa watu huko nyumbani na pia ni miongoni mwa raia ambaye anaamini kabisa haki zake zinapaswa kuheshimiwa. Lakini hili walilofanya mgambo kwa kuwa tu naibu waziri Nyalandu anakwenda kutembelea soko ni la kukemewa kwa nguvu. Kuna haja ya kuongeza sauti zetu, tupaze zaidi, tupinge hatua unyanyasi huu na ule unaoweza kuleta mauaji. Ni wakati sasa wa kusema hapana. Hawa watu wanaomfanyia hili huyu mama hawana moral authority wa kuendelea na kazi yao.
Picha hizo nimezitungua blog ya jiachie zikionyesha mgambo wakisafisha wamachinga kabla ya ziara ya naibu waziri.
sasa hilo ni tatizo la mgambo au la huyo mama? maana mtoa hoja yeye anaelekeza lawama kwa mgambo tu!Well hao ni wale wanaoitwa wamachinga wanaofanya biashara katika maeneo yasiyotakiwa. Nami pia nimejaribu kufuatilia, inasemekana huyo mama walimwambia watamkamata na yeye akawatishia kuvua nguo zote.