Hii hali ni dalili ya nini wakuu??

crankshaft

JF-Expert Member
Jun 12, 2019
1,410
3,376
Inanitokea mara kadhaa nikiwa nimelala hata mchana huwa ninahisi mwili kunesanesa kwa kasi, nashindwa kufumbua mdomo na macho na kuhema wakati huo,
ni wakati ambao huwa ninaomba sana kimoyomoyo kwani huwa ninaona ndio tumaini pekee lililobaki ni kama nahisi kufakufa hivi na sitamani kabisa kuguswa wakati huo.
ni dalili ya nini hii?
kuna ambao mnapitia hii?
 
Inanitokea mara kadhaa nikiwa nimelala hata mchana huwa ninahisi mwili kunesanesa kwa kasi, nashindwa kufumbua mdomo na macho na kuhema wakati huo,
ni wakati ambao huwa ninaomba sana kimoyomoyo kwani huwa ninaona ndio tumaini pekee lililobaki ni kama nahisi kufakufa hivi na sitamani kabisa kuguswa wakati huo.
ni dalili ya nini hii?
kuna ambao mnapitia hii?
Nimepitia sana nikiwa form four,mambo mengi mno ....kiufupi ni nguvu za Giza.Anza wewe kuzikemea kabla hata hujakimbilia Kwa wachungaji.Omba sana
 
Sio wewe peke yako, mimi karibu kila siku hunitokea, kuna sababu fulani ya kimwili nilisomaga mahali, nikikumbuka nita ku-direct
 
Zamani sana hama iyo nyumba sio kila nyumba zinalalika ilinikuta kwenye nyumba Fulani nakaa mwaka 2020
 
Jiongoze sala ya toba, mpokee Yesu moyoni mwako, lala: usingizi ni zaidi ya mtoto aliyezaliwa leo

Kumbuka kuleta mrejesho
 
Zamani sanaaa iliwahi nisumbua hiyo Hali, sema ilikuwa ni usiku tuu, mpaka nikawa naogopa ikifika usiku, sitamani usiku ufike... Maana nahisi kabisa mtu ananigusa na kunivuta , nashindwa kugeuka Wala kufanya nini. Kauli yangu pekee inabakia ni "Yesu nisaidie". Naita Hilo jina mpak inapotea.. Kuna siku ilinitokea mchana, mpaka watu wa pembeni wakasikia ndo kuja kuniamsha. But Mpk Leo haikuwahi nirudia tena.
 
Inanitokea mara kadhaa nikiwa nimelala hata mchana huwa ninahisi mwili kunesanesa kwa kasi, nashindwa kufumbua mdomo na macho na kuhema wakati huo,
ni wakati ambao huwa ninaomba sana kimoyomoyo kwani huwa ninaona ndio tumaini pekee lililobaki ni kama nahisi kufakufa hivi na sitamani kabisa kuguswa wakati huo.
ni dalili ya nini hii?
kuna ambao mnapitia hii?
''Sleeping Paralysis''
 
Hiyo ni sleep paralysis bro, ni hali ya kawaida tu usiogope.. hutokea ukisinzia umelala chali (kulalia mgogo ukitazama juu), au hata ubavu. Jitahidi ulalie tumbo haitakutokea.. inawezekana pia una bakteria tumboni wanatengeneza gesi, hizi huleta mauzauza usingizini pia.. jitahidi usishibe sana uendapo kulala. Hutokea pia kama uko na stress. Ni KAWAIDA USIPANIK
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom