Hii haki kweli kwa wasafiri wa uwanja wa Ndege JKN

Meneja wa uwanja chukua Hiro kwani unyanyasaji na mzigo ulizidi mbona taratibu zote alikotoka zilifuatwa na kama ni malipo yalishafanyika!meneja kuwa makini hapo uwanjani maana sasa hivi shirika letu linafufuliwa usije ukafukuza wateja sababu ya manyanyaso ya abilia ndege zetu bombadier zikakosa wateja!
 
Hawa jamaa wengi ni magumashi magumashi tu! KIA ndo balaa, wanapenda hela mpaka baasi
 
SIKUWEPO
je ukisafiri ukinunua nguo zako za kuvaaa natakiwa nilipe ushuru ...? . na nikinunua kule kule nikivaa kodi ipo pia nikija nazo tz
 
Wanataka rushwa hao. Nilishawahi kuwaaachia majani ya chai kibao tena nikawachimba na mkwara kuwa atakayeenda kuyatumia hatakaa akojoe tena maishani mwake. Sijui waliyafanya nini!
 
hii huwa ipo dar tu, si bandarini si airport, hawa jamaa ni shida kwa kweli, hata ununue kitoy chako (eg. mwanasesere) mradi kipo kwenye kibox, na risiti unayo uliyonunulia ukifika dar wao wanaganda ulipe tena na wakikupa risiti utakuta yale maandishi ya tin number yapo kutoka kwenye muhuri sio kama yameandikwa moja kwa moja
 
Kama una chupi zako chafu.utaumbuka
wala sio kuumbuka, nikiwa bado mwanafunzi nilishawahi jaza begi condoms kama 50 hivi halafu zinafata chupi chafu bandarini dar, manake ilikuwa usumbufu, nakumbuka yule mama alinitizama kisha akauliza we mwanafunzi nikamwambia ndio, akadai kijana taraatibu, alinimark sura kila nikipita pale anacheka tu
 
Hebu Ngoja niwaambie,
Kufunguliwa Begi kwa airport ni swala la kawaida na km wana mashaka na kilichomo ndani!! Na kwamujibu wa video huyo mama ana TV na hlo bag sasa huwez kubeba Tv ukapita nayo hapo Lazima ulipie kodi!! Narudia tena LAZIMA!! sasa amebeba TV ndyo maana wakapata mashaka nae na wakafungua na beg lake! Mfano mzuri ukienda Mozambique kupitia Mtwara, pale msimbati Idara ya mapato ya Mozambique wanakata kodi hata ukibeba doti 5 za vitenge!! So in this case LAZIMA alipe KODI


~Cmb
 
Mara zote issue huwa ni approach ya kutatua tatizo, na hao watu wa airport na tra hawajuia kama case ya jana sio ya leo wala ya kesho. Pia kama huyo dada kama katoka nje ya nchi (anavyozungumza hakuwapo kama miaka miwili hivi) na alikuwa huko miaka miwili hakuna cha kulipa hapo labda lingekuwa gari ambalo linataka miezi kumi na mbili kabla ya kurudi Tanzania (source website ya tra).

Halafu kesho kutwa anakuja kuwa boss wake ndio atashika adabu.
Kotojua sheria cyo sababu ya kutofungwa mkuu!! Alipaswa aulize taratibu
 
Huyu Dada wa KAZITAMU yuko sahihi kabisa. Huyu aliyetoka nje angeongea kiingereza cha kutokea puani wala asingeguswa hata. Angesema I VE BEEN OUT DE COUNTRY FOR TWO DECASES WHAT DO YOU EXPECT ME TO HAVE ? DO YOU WANT A BRIBE ? angefunguliwa mageti yote na shikamoo angepewa. Sasa anaongea kiswahili halafu cha kijaluo. Lazima wasaidiane tu....
 
Back
Top Bottom