Halafu bahati mbaya zaidi ni kwamba tumeshindwa kabisa kukashinda haka kamdudu.Sijui tatizo liko wapi,au labda ni mradi wa watu wanaotengeneza vyandarua na dawa za malaria..?? Hainiingii akilini kabisa kuwa miaka nenda rudi haka kamdudu kameendelea kuwa kasumbufu wakati tunajua wapi kanazaliana, kanaishi vipi na mbinu zote za kukaangamiza tunazijua.Mbona wenzetu kule America wakati wanajenga Panama kanal waliweza kusimamisha ujenzi wa Kanal hiyo ili kukaangamiza kwanza haka kamdudu, sisi tunashindwa nini..??Halafu tunazungumzia maendeleo,maendeleo yapi wakati mdudu tu ametushinda na anapoteza nguvu kazi ya Taifa kila kukicha..