Heshima ya CHADEMA yaongezeka duniani

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,343
217,381
Baada ya Freeman Mbowe kuachiwa Huru kutoka kwenye kesi ya uongo ya Ugaidi , aliyobambikiziwa kwa sababu ya harakati zake za kudai KATIBA MPYA na TUME HURU YA UCHAGUZI , Na sasa tena baada ya kinachoitwa KIKOSI KAZI CHA SERIKALI kinachodaiwa kutumwa kukusanya maoni ya wananchi KUTOA MAPENDEKEZO YAKE HADHARANI ( Huku Tume ya Warioba ikiwa imekusanya maoni ya wananchi huko nyuma , tena kwa uwazi ) , wadau wa duru za kisiasa wanaona kama CHADEMA NDIO CHAMA MAKINI NA CHENYE KUSTAHILI KUHESHIMIWA NA KUAMINIWA.

Hii ni kwa sababu hakuna Mtanzania yeyote anayepingana na hoja zao , hakuna mtanzania asiyekubaliana na Matakwa ya Chadema kuhusu KATIBA MPYA wala TUME HURU YA UCHAGUZI , Hata Rais Samia Suluhu kwa sasa anakubali kwamba upo umuhimu wa kuwapo kwa Katiba mpya na Tume Huru ya Uchaguzi , kinachosumbua ni kile Kigugumizi kinachoitwa NITOKE VIPI , na hii inasababishwa na WAHAFIDHINA walio Serikalini , walio ccm na kwenye idara nyingine za serikali wanaohofia UGALI WAO.

Dunia yote sasa imethibitisha UMAKINI WA HOJA YA CHADEMA ya kuwapatia wananchi wa Tanzania KATIBA MPYA pamoja na TUME HURU YA UCHAGUZI , tena si kuwapatia bure hivihivi tu , CHADEMA imetoka DAMU , JASHO LA MWILI NA MENO , na Maumivu mengine yasiyoandikika humu JF, Dunia imejua kwamba Chadema tangu awali ndio Tegemeo na nguzo ya Haki , ndio chama cha Kizalendo kinachostahili kuheshimiwa na Kuaminiwa .

Shukrani ziende kwa wote waliounga mkono jambo hili , Wakiwemo akina Askofu Mwamakula , Sheikh Issa Ponda , Askofu Bagonza na wengine wote ambao wametukanwa kila aina ya matusi yakiwemo na yale ya Nguoni , huku wengine wakikamatwa na kudhalilishwa kwa msimamo wao huu wa Kizalendo .

Hatimaye Haki Imeshinda .
 
Heshima itaongezeka wakiwa well cordinated,wakipunguza matamko na wakisimamia wanachokiamini kwa weledi mkubwa.

Suala la katiba mpya lisiwe la kubishana na serikali lakini matumizi ya technolojia yachukue nafasi na wahamie katika kuwaeleza wananchi KWANINI KATIBA mpya ni muhimu.Kwa lugha nyepesi waonyeshe na kwa mifano mapungufu makubwa ya katiba iliyopo kwa wananchi.


Chadema inahitaji msemaji mmoja mwenye sauti ya mamlaka,anayejua kupanga maneno na anayejua kuvikwepa vipengele vya sheria!!
 
Heshima itaongezeka wakiwa well cordinated,wakipunguza matamko na wakisimamia wanachokiamini kwa weledi mkubwa.Suala la katiba mpya lisiwe la kubishana na serikali lakini matumizi ya technolojia yachukue nafasi na wahamie...
Katiba Mpya ina umuhimu mkubwa sana, mfano;

- Kuleta mgawanyo na usimamizi wa rasilimali za taifa utakaowawezesha watanzania kwa wingi wao kufaidi matunda ya keki ya taifa lao, tofauti na ilivyo sasa kikundi kidogo cha watu kufurahia keki hiyo huku asilimia kubwa ya watanzania wakibaki kwenye lindi la umasikini.

- Itaondoa upendeleo na kuleta usawa wa wananchi, mfano nafasi za ajira ziwe zinatangazwa wazi mfano DED na wenye sifa ndio wapewe nafasi bila kujali itikadi za vyama vyao, tofauti na ilivyo sasa wengi wanaopewa wanakuwa na vinasaba na chama tawala.

- Mapato yatakayopatikana kutoka kwa usimamizi mzuri wa rasilimalinza taifa kama madini na nyinginezo yatatumika kutoa mikopo nafuu kwa vikundi vya vijana na kina mama hili litasaidia kuwakwamua kutoka kwenye umasikini wa kipato, tofauti na sasa mapato hayo hukwapuliwa na wajanja wanaolindwa na chama chao.

Pia yatasaidia uboreshaji wa huduma za afya kama upatikanaji wa madawa hospitalini, lakini hata wazee na walemavu wataweza kutibiwa bure kwa kupewa bima za afya kutokana na mapato yatakayokuwa yanakusanywa na halmashauri au serikali kuu chini ya sheria zitakazowekwa kuwabana wezi.

- Kwa upande wa sheria na utoaji haki, pakiwepo na njia nzuri za kuwateua majaji na mahakimu, hili litawafanya wawe huru kutimiza majukumu yao bila hofu ya kumchukiza mtawala ambaye anaweza kuwaadhibu kwa kuwanyima teuzi, hili litawaepusha majaji na mahakimu kuwa watumwa wa watawala na kuchelewesha utoaji haki makusudi kwa wanaostahili au kutokutoa haki hizo kabisa.
 
Wacha Porojo nyingi bali tuwekee ushahidi wa kuthibitisha hayo unayoyasema ili tuone ni wapi Duniani wameifuatilia chadema na kuleta hiyo impact.

Au unaongelea Dunia ya the Space na Maria Sarungi?

Halafu Chadema mna too much projects ONCE.

Ebu tupeni mrejesho wa kipi kati ya hivi mmewahi kuifikisha mwisho na kuja na mrejesho.

Operesheni Sangara.
M4Change.

Yaani miingi mpaka tunaisahau mingine ila ya hivi karibuni ni

Chadema Digital.
Katiba mpya.
Mbowe sio gaidi.
Join the chain?
Maridhiano ya kitaifa.
ACT sio chama kikuu cha upinzani.
Hatuitambuwi TCD.

Sasa tushike lipi na tuache lipi?

Eeh jamani eeh!
 
Operation Sangara na M4C nakumbuka zilisaidia sana kuongeza hamasa hasa kanda ya Ziwa, Chadema ilivuna wanachama wengi kanda ile na majimbo kama Nyamagana, Serengeti, Musoma Mjini, Tarime, nk

Kilichokuja kuharibu mpangilio ule ni upigwaji marufuku mikutano ya siasa, hili lilisababisha kuzorotesha movement zilizokuwepo, pia kama pasingekuwepo na ukiukwaji wa wazi za sheria ya uchaguzi 2019 & 2020 nina hakika Chadema ingevuna zaidi.
 
Katiba Mpya ina umuhimu mkubwa sana, mfano;

- Kuleta mgawanyo na usimamizi wa rasilimali za taifa utakaowawezesha watanzania kwa wingi wao kufaidi matunda ya keki ya taifa lao, tofauti na ilivyo sasa kikundi kidogo cha watu kufurahia keki hiyo huku asilimia kubwa ya watanzania wakibaki kwenye lindi la umasikini...
Umelishwa wimbo wa Katiba Mpya na Tume huru ya uchaguzi na wewe utauimba mpaka utakufa na Hakuna utakachoambulia.

Mbowe, Heche, Msigwa, Lema na Lissu mpaka sasa hivi Ni MATAJIRI chini ya Katiba hii hii MBOVU ya mwaka 1977.

Lakini wewe unaambiwa ili ukwepe umasikini lazima ipatikane Katiba Mpya na Tume huru ya uchaguzi.

Sometimes wanakuchochea ingia barabarani upambane, ukipigwa au hata kuuawa wanachukua picha zako wanatumia wafadhili, kuonesha namna serikali inakiuka demokrasia wanapewa pesa wanashiba.

Ona Kenya Wana Katiba Mpya na Tume huru ya uchaguzi, lakini mpaka leo bado wanapambania mabadilikooooo🤣🤣🤣🤣🤣

Maana yake kila mtu ana agenda zake ili aone mabadiliko lazima apate anachotaka, hivyo mabadiliko Ni wimbo usio na mwisho.

Screenshot_2022-03-11-05-29-13-617_com.twitter.android.png
 
Heshima itaongezeka wakiwa well cordinated,wakipunguza matamko na wakisimamia wanachokiamini kwa weledi mkubwa...
Ni bahati mbaya sana Kwa Wananchi wa Tanzania kudhaniwa hawajui lolote kuhusu umuhimu wa Katiba mpya na mapungufu ya Katiba ya sasa , Sasa tujiulize ni nani aliyetoa maoni kwenye Rasimu ya Katiba ya Warioba?

Nakumbuka kuna mwananchi mmoja , tena alikuwa mlemavu, wakati ule alitoa maoni yake kwamba Wimbo wa Taifa ubadilishwe , huku akinukuu eneo linaloimbwa "WABARIKI VIONGOZI WAKE" Hoja yake ilikuwa kwamba Jukumu la kujiombea liwe la mtu binafsi , awe kiongozi au Raia wa kawaida ni vema akajiombea mwenyewe , kwa vile dhambi zake anazijua mwenyewe .

Hivi mwananchi kama huyu haijui Katiba ya Tanzania kweli?
 
Wacha Porojo nyingi bali tuwekee ushahidi wa kuthibitisha hayo unayoyasema ili tuone ni wapi Duniani wameifuatilia chadema na kuleta hiyo impact.

Au unaongelea Dunia ya the Space na Maria Sarungi...
jikite kwenye mada
 
Operation Sangara na M4C nakumbuka zilisaidia sana kuongeza hamasa hasa kanda ya Ziwa, Chadema ilivuna wanachama wengi kanda ile na majimbo kama Nyamagana, Musoma Mjini..
Tatizo mwanza lilianza pale chadema walipoamua kuutoa mwili wa marehemu Mawazo (R.I.P) kutoka Geita na kuuleta Mwanza.

Kisha ikawa vurugu jijini Mwanza na kupelekea wafanyabiashara kulalamika kwa kusababisha kufunga biashara zao kukimbia vurugu za mabomu ya machozi.
 
Umelishwa wimbo wa Katiba Mpya na Tume huru ya uchaguzi na wewe utauimba mpaka utakufa na Hakuna utakachoambulia.

Mbowe, Heche, Msigwa, Lema na Lissu mpaka sasa hivi Ni MATAJIRI chini ya Katiba hii hii MBOVU ya mwaka 1977...
Una mentality ya enzi za old stone age iliyopitwa na wakati, update your brain uishi na kizazi cha sasa kifikra.

- Nilitegemea upinge hoja zangu hapo juu kwa kuonesha udhaifu wake kama kwa mfano, Katiba Mpya haiwezi kuleta maendeleo kwa wananchi kwa sababu 1..2...3.. lakini sio unasema Lissu na wengine wamekuwa matajiri kwa Katiba iliyopo hivyo kudai Katiba Mpya hakuna maana, huu ni ufinyu wa fikra.

- Kenya uliyoitolea mfano mpaka kufikia sasa atleast wao wana Katiba bora kushinda ya kwetu, kama bado wana mapungufu hayo yanaweza kutumika kama somo kwetu ili tupate Katiba Mpya iliyo bora zaidi kwa kuyafanyia kazi mapungufu yao.

Lakini sio tuache kabisa kutafuta Katiba Mpya kisa wakenya bado wanapata changamoto kadhaa toka kwa Katiba yao, huu wako na wengine wenye mawazo kama yako utakuwa ni udumavu wa akili.
 
Ni bahati mbaya sana Kwa Wananchi wa Tanzania kudhaniwa hawajui lolote kuhusu umuhimu wa Katiba mpya na mapungufu ya Katiba ya sasa , Sasa tujiulize ni nani aliyetoa maoni kwenye Rasimu ya Katiba ya Warioba...
Inapotamkwa wabariki viongozi wetu sio kwa sababu ya dhambi zao binafsi.

Bali kumuomba mungu awape "Busara" za kutuongoza.
 
Tatizo mwanza lilianza pale chadema walipoamua kuutoa mwili wa marehemu Mawazo (R.I.P) kutoka Geita na kuuleta Mwanza.

Kisha ikawa vurugu jijini Mwanza na kupelekea wafanyabiashara kulalamika kwa kusababisha kufunga biashara zao kukimbia vurugu za mabomu ya machozi.
Jeshi la polisi lilikuwa wapi kutoa ulinzi ili kuhakikisha hilo zoezi linafanyika kwa amani?

Hilo sio kosa la Chadema, peleka lawama zako panapostahili.
 
Baada ya Freeman Mbowe kuachiwa Huru kutoka kwenye kesi ya uongo ya Ugaidi , aliyobambikiziwa kwa sababu ya harakati zake za kudai KATIBA MPYA na TUME HURU YA UCHAGUZI , Na sasa tena baada ya kinachoitwa KIKOSI KAZI CHA SERIKALI kinachodaiwa kutumwa kukusanya maoni ya wananchi KUTOA MAPENDEKEZO YAKE HADHARANI ( Huku Tume ya Warioba ikiwa imekusanya maoni ya wananchi huko nyuma , tena kwa uwazi ) , wadau wa duru za kisiasa wanaona kama CHADEMA NDIO CHAMA MAKINI NA CHENYE KUSTAHILI KUHESHIMIWA NA KUAMINIWA .

Hii ni kwa sababu hakuna Mtanzania yeyote anayepingana na hoja zao , hakuna mtanzania asiyekubaliana na Matakwa ya Chadema kuhusu KATIBA MPYA wala TUME HURU YA UCHAGUZI , Hata Rais Samia Suluhu kwa sasa anakubali kwamba upo umuhimu wa kuwapo kwa Katiba mpya na Tume Huru ya Uchaguzi , kinachosumbua ni kile Kigugumizi kinachoitwa NITOKE VIPI , na hii inasababishwa na WAHAFIDHINA walio Serikalini , walio ccm na kwenye idara nyingine za serikali wanaohofia UGALI WAO .

Dunia yote sasa imethibitisha UMAKINI WA HOJA YA CHADEMA ya kuwapatia wananchi wa Tanzania KATIBA MPYA pamoja na TUME HURU YA UCHAGUZI , tena si kuwapatia bure hivihivi tu , CHADEMA imetoka DAMU , JASHO LA MWILI NA MENO , na Maumivu mengine yasiyoandikika humu JF , Dunia imejua kwamba Chadema tangu awali ndio Tegemeo na nguzo ya Haki , ndio chama cha Kizalendo kinachostahili kuheshimiwa na Kuaminiwa .

Shukrani ziende kwa wote waliounga mkono jambo hili , Wakiwemo akina Askofu Mwamakula , Sheikh Issa Ponda , Askofu Bagonza na wengine wote ambao wametukanwa kila aina ya matusi yakiwemo na yale ya Nguoni , huku wengine wakikamatwa na kudhalilishwa kwa msimamo wao huu wa Kizalendo .

Hatimaye Haki Imeshinda .
Kura hazitoki duniani: all politics is local!

Unamwona Seneta Manchin pamoja ni kuwa ni democrat anwapinga democrat wenzie na analaumiwa kutoka kila kona kuwa anakwamisha chama chake lakini yeye anajua local politics za West Virginia.
 
Wacha Porojo nyingi bali tuwekee ushahidi wa kuthibitisha hayo unayoyasema ili tuone ni wapi Duniani wameifuatilia chadema na kuleta hiyo impact.

Au unaongelea Dunia ya the Space na Maria Sarungi?

Halafu Chadema mna too much projects ONCE.

Ebu tupeni mrejesho wa kipi kati ya hivi mmewahi kuifikisha mwisho na kuja na mrejesho.

Operesheni Sangara.
M4Change.

Yaani miingi mpaka tunaisahau mingine ila ya hivi karibuni ni

Chadema Digital.
Katiba mpya.
Mbowe sio gaidi.
Join the chain?
Maridhiano ya kitaifa.
ACT sio chama kikuu cha upinzani.
Hatuitambuwi TCD.

Sasa tushike lipi na tuache lipi?

Eeh jamani eeh!
Alot of Options. Hii inaitwa kupandisha Tanga shusha Tanga
 
Nilitegemea upinge hoja zangu hapo juu kwa kuonesha udhaifu wake kama mfano, Katiba Mpya haiwezi kuleta maendeleo kwa wananchi kwa sababu 1..2...3.. lakini sio unasema Lissu na wengine wamekuwa matajiri kwa Katiba iliyopo hivyo kudai Katiba Mpya hakuna maana, huu ni ufinyu wa fikra.
Good
 
Operation Sangara na M4C nakumbuka zilisaidia sana kuongeza hamasa hasa kanda ya Ziwa, Chadema ilivuna wanachama wengi kanda ile na majimbo kama Nyamagana, Serengeti, Musoma Mjini, Tarime, nk

Kilichokuja kuharibu mpangilio ule ni upigwaji marufuku mikutano ya siasa, hili lilisababisha kuzorotesha movement zilizokuwepo, pia kama pasingekuwepo na ukiukwaji wa wazi za sheria ya uchaguzi 2019 & 2020 nina hakika Chadema ingevuna zaidi.

Uhaguzi wa 2015 mlitegemea kura nyingi kutoka kwa wasukuma, na haikuwa hivyo. Hivyo msitegemee tena kwa wasukuma kama watakipigia chama chenu. Ndoho bhabha.
 
Inapotamkwa wabariki viongozi wetu sio kwa sababu ya dhambi zao binafsi.

Bali kumuomba mungu awape "Busara" za kutuongoza.
Sasa Jiwe ni busara zipi alizotumia hata kama tuliimba huo wimbo 24/7 ?
 
Back
Top Bottom