Tusiwe na itikadi za kihisia, kinachofanywa na USA ni kukuacha ugombane na wananchi wako ukianza kuwaua anaingilia kati nakuchukua anachoona kinafaa, kwani akija kwako anatumia pesa pia, ktk nchi zote ulizotaja waliitwa na wananchi kuwasaidia zidi ya viongozi wezi na mafisadi waliojimilikisha mali za nchi hizo na kuwaua wananchi wanapowahoji hao viongozi, na china,urusi sera yao ni kuunga serekali yeyote iliyoko madarakani bila kujali inawaua wananchi wake au laa, wanachoaangalia ni mali wanazozipata,
Hakuna nchi yeyote yenye ushirika wa karibu kiuchumi na urusi au china wamefanikiwa, hata TZ haya ni matokeo ya urafiki wao wa kinafiki wakitudanganya kuwa ni wajamaa kumbe wao wameshabadilika ni mabepari, mfano wa karibu ni kwa mugabe!!. jaribu kufanya uchunguzi wa kina si kwenye mitandao sana utakuta Israel wako visuri sana kijeshi na kiteknologia wana vitu adimu hasa kiulinzi zaidi ambavyo wengine duniani hawana. Ni Vyema kama wananchi tu wakawaida tukafikiri zaidi jinsi viongozi hasa wakubwa na nchi zetu wanavyoenenda kwani kwa wizi wao unakuharibia hata wewe usiye na hatia, mfano serekali ikashindwa kuwaletea wananchi wa eneo lenye gesi na mafuta maendeleo kwa miaka 10, lakini viongozi wanaficha pesa kibao nje na wazungu wanajua kwani wanaficha kwenye bank zao, na wao wakaanza kuandamana na serikali ikaanza kuwaua na kuwaita mateja kama gadafi, wao wakaomba msaada Europer na USA watakua wamekosea?