Henry Matata: Dr. Slaa mwongo no. 1 duniani

Henry Matata: Dr. Slaa mwongo no. 1 duniani

Ichaguzi ujao hatutakuwa na nafasi ya vichaa kwenye chama, wagombea hata wa udiwani ndani ya Chadema watakuwa wengi na watateuliwa wenye akili timamu tu
 
Mwongo namba 1 duniani? loh

Yaani kwa maneno mepesi ni kuwa ukichukua waongo wote duniani mchumba wa josephine anaongoza kwa uongo.

hili neno kubwa sana! mtake radhi slaa.

usiwe unaandika vitu as if umeshikishwa ukuta ***** wewe..mbona mchumba wa mama yako humtaki radhi
 
Mi naamini kabisa mabadiliko ya nchi hii mungu yupo nyuma yake, sasa je ni nani mwenye uwezo wa kuepusha mabadiliko hayo, lazima huyo aende na maji 2.
 
Huyo matata na Dr.slaa wanamengi yapo nyuma ya pazia..Ukiona pnafuka moshi ujue pana moto.
 
Mnyonge Mnyongeni lakini Haki yake........

Jamani kata ya Kitangiri iliyo chini ya Matata matunda yanaonekana leo Kigari changu kidogo (Carina) ninaweza kupanda nayo Milimani barabara ya kwenda Jiwe kuu sasa hivi inapitika bila shida. Pia barabara ya kwenda Milimani mpaka Ziwani (Mihama) pia yapitika bila tabu na hivi alikuwa na mpango wa kufufua barabara ya Matauro

Ahhh Chungu lakini.......
 
Chadema itaendelea kuwapima na kuwachuja wale wote ambao ni pandikizi la CCM au wenye tamaa na uchu wa madaraka kwa manufaa yao wenyewe. Kauli ya Bw. Matata ni kauli ya mwendawazimu.
 
Anafanya kile kilchotarajiwa na wengi.Tatizo alilonalo ni tabia yake ya kutopanga hoja zake kimtitiriko.Kama akifanikiwa kuzipanga hoja zake mimi naamini atafanikiwa kisaidia CCM.Go on mstahiki.
 
mtoa uzi huu, kwanza ungeweka ushabiki wako pembeni, kisha utuabarishe vzr aliyosema meya. nasi tupate nafasi ya kuukubali / kuukataa usemi huo wa,,,,,,,,,,,,, no 1 duniani . vinginevyo tukishindwa sisi basi mwenyewe mlengwa atusithibitishie vinginevyo.
 
Henry Matata...?! Mla rushwa, Mamluki na ......utoto wa maisha unamsumbua huyu...

Ndugu wana JF, hayo si maneno yangu bali ni maneno ya Diwani mmoja jijini mwanza mwenye mgogoro na CHADEMA Bwn. HENRY MATATA.

Nianze kwa kusema kuwa leo asubuhi hii imekuwa ni mpya ya kufungia mwaka huu kwangu, baada ya jana kituo kimoja cha redio cha kidini (KWA NEEMA FM RADIO) hapa Mwanza kumuita diwani mmoja wa CHADEMA aliyefukuzwa uanachama (Kapera) na Matata ambaye ni meya mwenye mgogoro, wa manispaa ya Ilemela leo ilikuwa zamu ya Henry Matata kwenye kufanyiwa mahojiano kwenye kituo hicho.

Kusema ukweli kabisa sikuwahi kumsikia Henry Matata kwenye mahojiano, leo nimemsikiliza na kwa saikolojia ndogo tu si amini kama ni mzima timamu kutokana na jinsi alivyokuwa anaongea hoja zake.

Pia nipende kusema kwamba huyu ni mmoja kati ya watu ambao walitumia vizuri upepo wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 kugombea udiwani na kufanikisha kupitia CHADEMA, hafai hata chembe wala haihitaji muda kumsoma, kuongea kwake tu kuna kudhibitishia, na pia kwa kuwa kuna madai ya kuwa anatumiwa na CCM na hata mwenye alisema hivi majuzi kwenye kikao cha Mwigulu na hapa Nape, hapa mwanza kuwa yeye ni meya wa ccm, hivyo basi hata CCM wanazidi kujipambanua kuwa hawana nia ya dhati ya kuwa mfano wa uongozi bora na hawana nia njema na wananchi wa Ilemela, Kiufupi Matata hafai kuwa meya wala diwani, nitanukku machache ya aliyoyasema leo:-

Msikilizaji mmoja amepiga simu aksema "Naomba kumuuliza huyo bwana matata swali" kabla hajaendelea kuongea mtangazaji akasema "usimwite bwana matata mwite mstahik meya Matata" msikilizaji akasema "nyie ndo mnamwita hivyo mimi namwita bwana matata", ndipo matata akasema kama hawezi kuniita meya kata simu yake, akasema siwezi kumsikiliza, basi huyo msikilizaji kweli akakata simu kweli.

Msikilizaji mwingine akauliza, mbona Dr. Slaa juzi kwenye TV, alisema kuwa uliulizwa kama kweli ulipokea pesa kutoka CCM zaidi ya mara 4 na ulikubali, na hapa hata katika maelezo yake matata mwanzoni mwa kipindi alikubali, kwa hoja kwamba alizichukua kama ambavyo CHADEMA wanapewa na Sabodo, jibu la Mtata likawa, Slaa ni mwongo number 1 duniani we endelea kumwamini Slaa, hata wakati wa uchaguzi 2010 alisema atashusha bei ya cement hadi sh. 5000, kwanza hata slaa mwenyewe hakujui we unamtetea tu wakati hata kule karatu kwao hawamtaki kwanza ameiba pesa zao kutoka kwa wafadhiri ujerumani.

Mtangazaji akamwambia naomba siku moja niwakutanishe hapa na Kapera, akasema we mlete tu hata ngumi zitapigwa humu ndani, we diwani gani eti anataka umeya wakati kaishia la tatu atafanya nini mimi nimesoma bwana, kwanza anaishi kwa wakwe zake na mke wake Sofia.

Hayo ni machache tu, kwa machache hayo mimi nimeelewa kama mtu asiye timamu sijui wewe mwenzangu kama ndo meya huyo kweli ni wa kichina kama CHADEMA wanavyomwita huku, na pia CCM watatumia hiyo nafasi vilivyo kufanikisha mipango yao.
 
Huyo mtu ni dhahiri yuko frustrated. Na sijui MEDIA zinapowaita watu walio out of mind zinategemea nini kama si matumizi mabaya ya airtime!

Ninategemea sasa ni wakati wa vyombo vya habari kuonyesa ukomavu na kufnya kazi yake ya kujenga nchi kwa kumaanisha. Tafuta watu ambao ni competitive and constructive ili watoe taarifa za manufaa na ujenzi wa taifa linalopumulia mashine. Acha ushabiki wa kisiasa kwa kushadadia ujinga usio na tija kwa yeyote. Wapo watu sahihi wenye uelewa na uwezo wa kuchambua hoja kwa mitazamo tofauti na wasikilizaji wakapata manufaa.

Sasa watu kama matat unawaweka ili nini?
 
Chadema inabidi ijipange sana kuchuja wagombea katika hatua za awali ndani ya chama ili watu ambao wa akili kama hizi wasifikie hapo walipofika
 
mtoa uzi huu, kwanza ungeweka ushabiki wako pembeni, kisha utuabarishe vzr aliyosema meya. nasi tupate nafasi ya kuukubali / kuukataa usemi huo wa,,,,,,,,,,,,, no 1 duniani . vinginevyo tukishindwa sisi basi mwenyewe mlengwa atusithibitishie vinginevyo.

Mkuu mbona maelezo yanaeleweka sana, kweli umeshindwa kufahamu ufinyu wa akili wa huyo diwani katika hata majibizano ya simu na mpiga kura wake aliyekua anataka kumuuliza swali.Ama ni ushabiki wako ambao unashindwa kuelewa maelezo ambayo yanaeleweka hata kwa mtu ambaye hana elimu ya darasani?
 
Apimwe akili mnaweza jikuta mnapoteza muda wenu bure
 
Kwanini asiseme Pinda ndo mwongo namba moja maana ndiye aliyedanganya Bunge mpaka hoja ya Lema ikazimwa
 
Huyu Bw. anaeitwa Henry Matata sio mzima hata kidogo. Mara ya kwanza kumwona ilikuwa kwenye harambee ya kuchangia Kanisa hapa Pasiansi na mgeni rasmi alikuwa Mhe. Waziri Mkuu. Jamaa alibehave kihuni sana. Wanaomfaham wanasema anafujo sana na anarekodi ya kuwai kuwa mhalifu sana (jambazi). Tatizo CDM inakomba kila aina ya mtu ilimladi anataka kugombea uongozi. matokeo yake ndo haya. Ila huu upinzani wa CCM na CDM hapa Mwanza utarudisha maendeleo nyuma. Nashangaa sana waliomchagua kuwa meya, sijui walitumia akili gani kati ya kwenye visigino na makalio?!! Hapa ndo ninapoichukia siasa.
 
Back
Top Bottom