Helikopta ya kwanza ya Zimamoto kununuliwa

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,817
4,566
Serikali imesema imepanga kufanya maboresho makubwa katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ikiwa ni juhudi za kupambana na athari za majanga pindi zitokeapo ajali mbalimbali ikiwemo ajali ya moto ili kuweza kuokoa mali na maisha ambapo kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania itanunuliwa Helikopta ya kusaidia uokoaji.

Maboresho hayo yanajumuisha ununuzi wa magari ya kuzimia moto yasiyopungua 150, magari 20 ya kubebea Wagonjwa, boti za kisasa 25 za uokozi na Helikopta moja maalum ya uokozi.

Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni amesema hayo Kibaha Mkoani Pwani wakati akiongea katika mkutano wa kuwajengea uwezo Wakuu wa Mikoa yote Tanzania Bara na Makatibu Tawala ulioandaliwa na TAMISEMI.

“Kwa mara ya kwanza katika historia ya Nchi hii, Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan inakwenda kufanya uwekezaji mkubwa katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, nawaomba Wakuu wa Mikoa kuhakikisha kunakuwepo vituo vya kuchotea maji ambayo yatatumika pindi yatokeapo majanga ya moto”
 
Serikali imesema imepanga kufanya maboresho makubwa katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ikiwa ni juhudi za kupambana na athari za majanga pindi zitokeapo ajali mbalimbali ikiwemo ajali ya moto ili kuweza kuokoa mali na maisha ambapo kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania itanunuliwa Helikopta ya kusaidia uokoaji.

Maboresho hayo yanajumuisha ununuzi wa magari ya kuzimia moto yasiyopungua 150, magari 20 ya kubebea Wagonjwa, boti za kisasa 25 za uokozi na Helikopta moja maalum ya uokozi.

Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni amesema hayo Kibaha Mkoani Pwani wakati akiongea katika mkutano wa kuwajengea uwezo Wakuu wa Mikoa yote Tanzania Bara na Makatibu Tawala ulioandaliwa na TAMISEMI.

“Kwa mara ya kwanza katika historia ya Nchi hii, Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan inakwenda kufanya uwekezaji mkubwa katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, nawaomba Wakuu wa Mikoa kuhakikisha kunakuwepo vituo vya kuchotea maji ambayo yatatumika pindi yatokeapo majanga ya moto”
Ni jambo jema,wajitahidi angalau kila kanda iwe na helkopta 1,Nchi yetu kubwa hii

Uwepo wa helkopta 1 kwa kanda itakua ni jambo jema zaidi
 
Serikali imesema imepanga kufanya maboresho makubwa katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ikiwa ni juhudi za kupambana na athari za majanga pindi zitokeapo ajali mbalimbali ikiwemo ajali ya moto ili kuweza kuokoa mali na maisha ambapo kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania itanunuliwa Helikopta ya kusaidia uokoaji.

Maboresho hayo yanajumuisha ununuzi wa magari ya kuzimia moto yasiyopungua 150, magari 20 ya kubebea Wagonjwa, boti za kisasa 25 za uokozi na Helikopta moja maalum ya uokozi.

Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni amesema hayo Kibaha Mkoani Pwani wakati akiongea katika mkutano wa kuwajengea uwezo Wakuu wa Mikoa yote Tanzania Bara na Makatibu Tawala ulioandaliwa na TAMISEMI.

“Kwa mara ya kwanza katika historia ya Nchi hii, Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan inakwenda kufanya uwekezaji mkubwa katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, nawaomba Wakuu wa Mikoa kuhakikisha kunakuwepo vituo vya kuchotea maji ambayo yatatumika pindi yatokeapo majanga ya moto”
Zaidi ya miaka 60 ya uhuru helicopter ya kwanza? Sasa hiyo itasaidia upcoming Dodoma, Dar, Mwanz, Arusha au Tandahimba na Mpitimbi?
 
Serikali imesema imepanga kufanya maboresho makubwa katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ikiwa ni juhudi za kupambana na athari za majanga pindi zitokeapo ajali mbalimbali ikiwemo ajali ya moto ili kuweza kuokoa mali na maisha ambapo kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania itanunuliwa Helikopta ya kusaidia uokoaji.

Maboresho hayo yanajumuisha ununuzi wa magari ya kuzimia moto yasiyopungua 150, magari 20 ya kubebea Wagonjwa, boti za kisasa 25 za uokozi na Helikopta moja maalum ya uokozi.

Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni amesema hayo Kibaha Mkoani Pwani wakati akiongea katika mkutano wa kuwajengea uwezo Wakuu wa Mikoa yote Tanzania Bara na Makatibu Tawala ulioandaliwa na TAMISEMI.

“Kwa mara ya kwanza katika historia ya Nchi hii, Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan inakwenda kufanya uwekezaji mkubwa katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, nawaomba Wakuu wa Mikoa kuhakikisha kunakuwepo vituo vya kuchotea maji ambayo yatatumika pindi yatokeapo majanga ya moto”
Hivi zile drone mbona hata kk imeungua hatujaziona, na vile vibomu vyao vya kuzimia moto
 
WaTz milioni 60, tunaokatwa tozo Takriban bilioni 200 kwa mwezi, hadi leo tunaongelea kununua helicopter ya kwanza ya zimamoto isiyozidi bilioni 1 au 1.5, hivi sisi wakati tunarogwa tulikuwa uchi au?
Tulia basi ndugu yangu bajeti yenyewe aslimia 30% tukakope tupewe msaada kama tozo zinatosha si tungeanzia huko
Tupongeze kwa hatua tunazopiga hata kama tumechelewa ila bado taifa litaendelea kuwepo watafaidi kizazi hiki na kinachokuja tuweke msingi wa uchumi huru sasa.
 
Tatizo la nchi hii ni kuwa wenye uwezo hawana nafasi, na wenye nafasi hawana uwezo
Tumia uwezo wako au hao waliokuwa hawana uwezo bado hawana excuse kwa kuwa fursa zipo nyingi mfano mo dewji na bakhresa wanalitendea haki taifa lao kwa kujiendeleza wao na kuajiri maelfj ya watanzania na kulipa kodi ili huduma za kijamii zipatikane kwa hio uwezo wako akili yako kubwa bado unaweza kuitumia vizuri kusaidia jamii ya kitanzania bila kuwa na uongozi wa kisiasa alisema jf.kennedy jiulize unaifanyia nini nchi yako na sio ncho yako inakufanyia nini ila sisi tunataka tu au sana nchi itufanyie tubadili hizi mindset.
 
Back
Top Bottom