Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 19,768
- 49,934
- Thread starter
- #61
Sijasema kuwa mabadiliko ya sheria na mikataba ni kosa kufanyika lakini yafanyike for the better. Mabadiliko yasiache nia ya msingi ambayo ni kuhakikisha tunavutia uwekezaji wenye manufaa. Mambo hayo mawili ni sharti yaende pamoja. Huwezi kupata faida kubwa kwa kuweka urasimu sumbufu. Unatakiwa kuwa mwerevu ili kuhakikisha kuna mifumo efficient lakini isiyoua uwekezaji na lengo lako kuu.Mkuu with due respect maandiko yako ni propaganda tupu. Hutoi mifano halisi ila unataja nchi kwa ujumla wake tu. Mfano Botswana wanafanyeje? Ghana wanafanyeje nk. Tumeibiwa vya kutosha sana na imetosha sasa.
Mfano Botswana ukija na upembuzi wa mradi wako wa tuseme umepanga kuvuna ounces million 2.5 za dhahabu, ukiwekeza na ukavuna kweli kiasi hicho lakini kulingana na halisi ukawa bado kuna reserve ya kutosha, wanaingia ubia na wewe wa 50 kwa 50. Nakumbuka wakati ukiwa unavuna wakia millioni 2.5 ulikuwa ukilipa royalty na kodi zake kama kawa.
Pia fikiria sisi tunaumiliki wa karibu asilimia 30 mgodi wa almasi mwadui lakini tangu kabla ya uhuru mpaka leo hakuna gawio ni hasara juu ya hasara. Ni upuuzi mtupu kutuambia watakimbia. Wacha wakimbie tutavuna sisi na technology yetu.
Tanzanite inapatikana Tanzania wauzaji wakubwa wahidi, marekani na Kenya. Sisi sijui ni wanne, upuuzi gani huu!
Tunataka haki sawa na mimi.niko mgodini tangu 2005 najua uhuni wote. Sydney wanaandika taarifa nyingi za uongo na uzushi na wanafanya biashara za kufa mtu kwenye masoko yao ya hisa kwa mali zikiwa Tanzania. Transfer price arrangement ndo usiombe
Sent using Jamii Forums mobile app
Kutopata chochote kutoka kwenye mgodi wa almasi Mwadui kunatokana na serikali kutojua biashara ya sekta hii ilivyo. Waliowekeza kwenye makampuni ya madini wanapata faida zaidi kwa kuuza hisa na siyo malipo ya dividends. Kama hatukuuza shares zetu, tutapataje faida wakati hakuna dividends zilizogawiwa? Hata kwenye mabadiliko ya sasa kitakachoongezeka ni mapato yatakayotokana na royalty ya 7%, na siyo mapato yatakayotokana na ongezeko la free carried shares la 16%. Unaweza kuongeza mpaka 30% na usipate chochote.
Kwenye transfer ya leseni kwa makampuni unayoyasema, unaweza kunipa mfano hata wa kampuni moja? Nijuavyo mimi, zamani makampuni yalikuwa yanaweza kufanya license transfer baada ya kulipa tu transfer fee lakini kwa sheria ya 2010, license transfer haifanyiki mpaka kulipwe capital gain tax, na anayefanya transfer apate TRA clearance.
Ifahamike kuwa migodi haipatikani bila miradi ya utafiti. Utafiti ni aghali, na unapotafiti uwezekano wa kupoteza pesa ni zaidi ya 90%. Ukimwekea masharti magumu mtafiti, hafanyi maana hakuna anachopoteza.
Makampuni yenye migodi nchini yanalazimika kuvumilia kwa sababu tayari wamewekeza infrastructure isiyoondosheka. Ambaye hajawekeza chochote au hajawekeza kiasi kikubwa kwenye utafiti haoni hasara ya kutokuwepo Tanzania. Wanaoifahamu vizuri sekta hii huweka mazingira rafiki na rahisi sana kwa makampuni ya utafiti maana hayo ndiyo huleta makampuni ya uchimbaji. Masharti magumu ya utafiti yatazuia wawekezaji wa shughuli za utafiti na hivyo tutabakia na miradi ya uchimbaji tuliyo nayo bila ya kupata miradi mipya.
Ikumbukwe kwamba migodi iliyopo inazidi kwenda chini, gharama zinazidi kuongezeka, faida inazidi kupungua, na mwisho itafungwa wakati hakuna migodi mipya itakayokuwa inafunguliwa.
Kuhusu serikali kupata 50 free carried shares baada ya kuchimba kiasi kilichoripotiwa mwanzo wa mradi, sina uhakika kama kitu hicho kipo au hakipo. Nilicho na uhakika nacho ni kuwa kila mining project, serikali huwa na 10% free carried shares na serikali hulipia shares inapotaka kuchukua zaidi ya hiyo 10% kwa taratibu ambazo kampuni na serikali wanakubaliana.
Sent using Jamii Forums mobile app