PreGE2025 HECHE: Nilimshauri Magufuli lakini hakunisikiliza

PreGE2025 HECHE: Nilimshauri Magufuli lakini hakunisikiliza

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)
We mama sijui unaongea nini?Karne na Karne coal imetumika kutengenezea haya maendeleo ya viwanda vilivyopo Leo hata kabla ya umeme wa viwandani,viwanda vyote duniani vilianzia makaa ya mawe,viwanda vya meli,treni etc halafu wewe unasema eti makaa sio issue!!!Ok Leo hilo bwawa lenu la Nyerere limekamilika Mbona bado gharama za umeme zipo juu???Viwanda Mbona vina prefer coal sana kuliko umeme???Punguza uchawa mama
Acha kutetea ujinga. Umeme unahitajika kuliko hicho kiwanda. Umeme una manufaa kwa watanzania wote ila kiwanda hakitagusa maisha ya watanzania wote. Umeme wa uhakika utazalisha viwanda vingi zaidi. HECHE NI AKILI NDOGO SANA.
 
Hicho kiwanda cha chuma kingeendeshwa kwa umeme wa mafuta taa? Nchi ilikuwa na MW 1600 tu kuhudumia watu 60m.. umeme ulihitajika kwanza kuliko kitu kingine. Ushauri wake ulikuwa mzuri kama kungekuwa na umeme wa kutosha.
Kingeendeshwa kwa makaa ya mawe
 
Hicho kiwanda cha chuma kingeendeshwa kwa umeme wa mafuta taa? Nchi ilikuwa na MW 1600 tu kuhudumia watu 60m.. umeme ulihitajika kwanza kuliko kitu kingine. Ushauri wake ulikuwa mzuri kama kungekuwa na umeme wa kutosha.


Makaa ya mawe yangezalisha umeme wa kutosha kuendesha smelter, na ziada ingeingizwa kwenye grid ya Taifa.
 
Makaa ya mawe yangezalisha umeme wa kutosha kuendesha smelter, na ziada ingeingizwa kwenye grid ya Taifa.
Mkiingia madarakani mwaka 2455 mtafanya yote mnayosema... kwa sasa twende na ilani ya uchaguzi ya CCM.
 
"Wakati bwawa la mwalimu Nyerere linajengwa nikaishauri serikali chini ya Rais Magufuli, unataka kujenga bwawa unataka kujenga SGR unahitaji chuma, sisi tuna chuma pale Liganga, Ludewa tuna chuma cha kuchimba miaka 100 tuna mlima wa chuma tutatumia hiko chuma hata miaka 100, Mungu akaweka na makaa ya mawe ya kuyeyushia hiko chuma pale pale Liganga, mchanga wa kusafishia hiko chuma akaweka pale Iringa hakuna kitu tunaagiza kutoka nje"

"Nikamwambia Rais kabla hatujaanza kujenga bwawa letu la Mwalimu Nyerere tujenge kwanza kiwanda chetu kile kiwanda ambacho kilikuwa kinahitaji Dola za kimarekani Bilioni 3 ambazo ni Trilioni 7.8 halafu tuchimbe miaka 100, halafu ukishajenga hiko kiwanda kingeajiri vijana elfu 60 halafu unamuita mkandarasi ajenge bwawa la Mwalimu Nyerere unampa hela lakini unamwambia chuma utanunua hapa kwahiyo unampa hela kwa mkono huu halafu unachukua kwa mkono mwingine."

"Hawakunisikiliza wakanipuuza leo tunaagiza chuma kutoka nje, mwaka jana pekee yake tumeagiza chuma chenye thamani ya dola Bilioni 1.2 sawa na Tsh. Trilioni 3 kwa mwaka, huo ni mwaka mmoja, mwaka juizi hivo hivo kwa miaka 3 tumeagiza chuma cha Trilioni 10 ambacho tungejenga kiwanda chetu cha Trilioni 7.8 tungechimba miaka 100"

John Heche - Makamu Mwenyekiti CHADEMA akihutubia wananchi wa Serengeti.

Huyu jamaa ni hazina kubwa sana kwa Taifa huwa namuelewa sana.

#EastAfricaTV
Tumwalike Traore Ibrahim aje atuambukize maarifa ya kutumia rasilimali!!
 
Back
Top Bottom