Hebu nielezeni labda mie mshamba

Hebu nielezeni labda mie mshamba

cherylsweet

Member
Joined
May 28, 2014
Posts
15
Reaction score
6
Kwanza shikamooni/marahabaa

Mie ndo mara ya kwanza kupost mada humu jamvini, yamenikuta. Kuna kijana nampenda mnooo na yeye anajua hilo, hapo mwanzo tulikuwa wapenzi lakini kwa sababu zisizozuilika tukaachana tukaja onana tena miezi miwili imepita anasema ananipenda bado lakini ana mtu ambaye amempromise kumuoa .

Kwa mantiki hiyo basi anaugulia tuu hata usiku wa manane msg zatumwa na nini na nini lakini anasema hatuwezi kuwa pamoja. Akinipigia simu ananambia nampa shida. Anataka kumuacha huyo msichana lakini hajamkosea kitu anaogopa kumuumiza, ila yeye anaumia kwa kuwa hatupo wote.

Sasa nauliza kwanini mapenzi yakoje, kuumiza mtu au kujiumiza mwenyewe. Kwanini apate shida while he is the decision maker?
 
huyo ni tapeli wa mapenzi, akirudi kwako ipo siku atakutenda
 
mapenzi yako hivi yeye si anataka kuoa na wewe ni pm ili nikuoe
 
Ingawa sijaelewa kati ya wewe na yeye nani anaehitaji kushauriwa.
Ila ngoja nianze kama ifuatavyo, yawezekana jamaa anakupenda kiukweli lakini anaona wewe si waifu matirio kutokana na vigezo vyake ambavyo kajiwekea kuhusiana na mke anae muhitaji. Pia yawezekana alikokwenda ameona hapamfai na akaona wewe unaunafuu kuliko huyo alie mpata.
Nakushauri usiogope, kuwamjasiri, muite na uzungumze nae, kama akikubali kuishi na wewe, usione hatari kulamba matapishi kwakua nawe unaonekana kumpenda, then maisha yataendelea kama kawa na wenye kusema watasema alafu watanyamaza
 
Uliachana nae kwa sababu zisizoweza kuzuilika na sasa anataka kumuacha alie nae bila ya kosa lolote.

Huyo hafai utarudiana nae tena ataendelea kukuumiza kichwa na akimpata mwingine ataendeleza hako kamchezo, kifupi ameshajijengea kitabia hako na hatokiacha, kuwa makini utakuja achwa njia panda
 
Hachana naye uyo ndezi

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
namshukuru mungu sana nimezaliwa mwanaume.
 
Nimeambiwa picha za John komba xipo humu ndani... Nikizipata... Nitakupa ushauri dada
 
Mi naona posti imetungwa tu, anyway rudiana nae tu kwani si mwenyewe umejisifia anakupenda?
 
Angekupenda ukweli angemuacha aliyekuwa nae!
 
Mmmeachana kwa miezi 2 kwa kupotezana???

Gongwa ngozi acha masihara, ushafanywa kipozeo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom