Hayati Magu miaka mitano kama 15.
Spidi ya maendeleo aliyokuwa anaendanayo Hayati magu kwa miaka mitano ukilinganisha na miaka ya nyuma kabla hajawa Rais,unaweza kudhani alikaa miaka 10.
Nitataja kwa uchache nawewe utaongezea kwa sauti ama kimya kimya.
1, Kuweka nidhamu kwa watumishi, yani mtumishi wauma alijuwa wazi akiharibu kinacho fuata ni kupoteza kazi.
2, Kuanzisha mradi mkubwa wa umeme.
Pamoja na figisu fugisu kutoka kwa mabeberu na mawakalawao lakini Jembe alikomaa na tukaanza ujenzi wa bwawa.
Wote tuna fahamu mizengwe iliyokuwa inawekwa,mara tunaharibu misitu,mara urithi wa dunia,na ujingaujinga mwingine mwingi lakini jembe alifumba macho na kuchukua maamuzi kama kiongozi na kazi inaendelea.
Miundo mbinu, flyivers madaraja kama Tanzanite,Busisi,na Wami.
Ununuzi wa ndege,na ujenzi wa viwanja vya ndege.
SGR na mengine mengi, yanaonyesha spidi yake katika kukuza uchumi wanchi ilikuwa kubwa sana ukilinganisha na tulivyo zoea miaka ya nyuma.
Kwamfano miaka iliyopita kuanzia Mkapa, tunaona maendeleo yake kwa miaka kumi kwa vitu vinavyoonekana kirahisi ni Daraja la Mpkapa kusini, na uwanja wampira Taifa.
Kwa mzee Kikwete maendeleo yanayoonekana kirahisi ni Ujenzi wa barabara nchi nzima kwa usimamizi wa Hayati Magu na daraja la Nyerere kigamboni.
Sasa ukihesabu miradi ya magu utaona ni mingi na mikubwa mara 20 kwa miradi iliyo anzishwa na wenzake hao wawili kwa miaka 20.
Kuna watu wanaumiza vichwa saizi jinsi ya kwenda na speed yake japo amesha kufa.