Haya ndiyo yanayotokea kwa sasa

Haya ndiyo yanayotokea kwa sasa

Mizigo

Member
Joined
May 29, 2014
Posts
12
Reaction score
1
Hapa ninapokaa nipo jirani kabisa na kanisa fulani ambalo kwa mida hii sasa ndo limezama kwenye maombi mazito ya kiroho. Hawa waumini wake wamejizatiti sawa sawa kuziangamiza nguvu za muovu shetani. Lakini sasa hali ni tofauti sana kwangu. Yaani hapa nilipo nawaza vitu vya ajabu ajabu tu visivyo na tija yoyote kabisa. Mbaya zaidi na masaa menyewe haya usiku unaelekea kutulizana sijuwi mwisho wake itakuwaje na masaa ya kuikimbilia siku mpya ya kesho yamebaki machache. Asubuhi yangu ya kesho inaweza isiwe nzuri
 
Nimetoka kapa,kifupi sijaelewa unachokihitaji toka kwa wanajamvi
 
eeehhhh, jf imesaidia sana.Mirembe ingeshajaa

Mkuu Kongosho Mirembe kwa hiyo bila hili jamvi nilistahili kuwa Mirembe kweli? Nikiwa hapo Mirembe ndo ningejiuliza haya sasa si ndiyo maana yake.
 
kwwnda mirembe si.lazima ukazwe. Ila mmu.ni rehab kabisa.

Mkuu Kongosho Mirembe kwa hiyo bila hili jamvi nilistahili kuwa Mirembe kweli? Nikiwa hapo Mirembe ndo ningejiuliza haya sasa si ndiyo maana yake.
 
kwamba unasindikiza mapambio kimya kimya au? mi sijakuelewa
 
Asubuhi ndio hii Mizigo uko njema?

Mkuu wacha Mungu tumwachie cheo chake bila msaada wake ilikuwa utata mtupu. Kila kitu nilimwomba aniongeze maana kikombe kilichokuwa mbele yangu na ambacho nilipaswa nikinywe hakika sikutaka kabisa hata kukiona. Kimerudi kule kiliko toka. Huwezi amini mkuu nilikuwa natembelea unit chache sana za maisha
 
Back
Top Bottom