kaburunye
JF-Expert Member
- May 12, 2010
- 672
- 74
Watanzania tuna ugonjwa mbaya wa kutokufuatilia mambo mpaka yafikie hatima yake. Nadhani vyombo vyetu vya habari ni muhimu visaidie katika hili. Sijui wadau wengine mnasemaje. Kwa mfano sijui mambo haya hapa chini yaliyokamata vichwa vya habari huko nyuma yameishia wapi?
1. Sakata la Dr Slaa kudai kawekewa vinasa sauti kwenye chumba chake - polisi walidai wanafanya uchunguzi. je huu uchunguzi haukamiliki
2. Ripoti ya sababu ya mlipuko wa mabomu ya mbagala - Dr hussein Mwinyi alisema ameunda tume na atatoa ripoti hadhari na kwamba atawajibika kama ikionekana kuna uzembe. Hii ripoti imeshatoka?
3. Kesi za EPA - mwanzoni hizi kesi zilionekana kufuatiliwa sana na tulikuwa tunapata updates za mara kwa mara. Hizi kesi bado zipo au ndo zimekufa natural death??
4. Kesi ya Zombe - tuliambiwa serikali imekata rufaa? hili jambo linaendeleaje?
5. Kifo cha utata cha aliyekuwa naibu waziri - Salome Mbatia - tuliambiwa dereva wa lile lori lililosababisha ajali alikuwa anatafutwa? Jamaa kakimbilia mwezini au yuko sayari gani ambako vyombo vya dola haviwezi kufika? je mwenye lori hakutoa msaada wowote ili jamaa akamatwe. Inasemekana mama aliuwawa kwa sababu za kisiasa - maana ndiye alikuwa mweka hazina wa CCM wakati wa uchaguzi na alijua siri nyingi ikiwemo ya EPA
6. Kesi ya Mramba, Yona na Mgonja - hii kesi ilifunguliwa kwa kumaanisha kweli au ni danganya toto? kipi kinaendelea, naona inaenda kwa mwendo wa kinyonga - au upelelezi bado unaendelea kama kawaida ya jeshi letu la polisi
7. Kiwira - serikali ilisema inafanya tathmini ya kuuchukua mgodi huu - sijui hili nalo limefikia wapi. Nani anaumiliki mgodi kwa sasa
Wadau mi ninayoyakumbuka kwa haraka haraka ni hayo. Kama yako mengine hebu tukumbushane. Nadhani itabidi tuwe na register ya kurekodi hizi skendo zote na kuzifuatilia kwa karibu maana tunasahau kwa wepesi sana na kuanza kushabikia skendo mpya mpya na baada ya muda tunazisahau pia. TUTAFIKA kwa staili hiiii???
1. Sakata la Dr Slaa kudai kawekewa vinasa sauti kwenye chumba chake - polisi walidai wanafanya uchunguzi. je huu uchunguzi haukamiliki
2. Ripoti ya sababu ya mlipuko wa mabomu ya mbagala - Dr hussein Mwinyi alisema ameunda tume na atatoa ripoti hadhari na kwamba atawajibika kama ikionekana kuna uzembe. Hii ripoti imeshatoka?
3. Kesi za EPA - mwanzoni hizi kesi zilionekana kufuatiliwa sana na tulikuwa tunapata updates za mara kwa mara. Hizi kesi bado zipo au ndo zimekufa natural death??
4. Kesi ya Zombe - tuliambiwa serikali imekata rufaa? hili jambo linaendeleaje?
5. Kifo cha utata cha aliyekuwa naibu waziri - Salome Mbatia - tuliambiwa dereva wa lile lori lililosababisha ajali alikuwa anatafutwa? Jamaa kakimbilia mwezini au yuko sayari gani ambako vyombo vya dola haviwezi kufika? je mwenye lori hakutoa msaada wowote ili jamaa akamatwe. Inasemekana mama aliuwawa kwa sababu za kisiasa - maana ndiye alikuwa mweka hazina wa CCM wakati wa uchaguzi na alijua siri nyingi ikiwemo ya EPA
6. Kesi ya Mramba, Yona na Mgonja - hii kesi ilifunguliwa kwa kumaanisha kweli au ni danganya toto? kipi kinaendelea, naona inaenda kwa mwendo wa kinyonga - au upelelezi bado unaendelea kama kawaida ya jeshi letu la polisi
7. Kiwira - serikali ilisema inafanya tathmini ya kuuchukua mgodi huu - sijui hili nalo limefikia wapi. Nani anaumiliki mgodi kwa sasa
Wadau mi ninayoyakumbuka kwa haraka haraka ni hayo. Kama yako mengine hebu tukumbushane. Nadhani itabidi tuwe na register ya kurekodi hizi skendo zote na kuzifuatilia kwa karibu maana tunasahau kwa wepesi sana na kuanza kushabikia skendo mpya mpya na baada ya muda tunazisahau pia. TUTAFIKA kwa staili hiiii???