Haya maisha haya! Acheni tu

Haya maisha haya! Acheni tu

genious wa kijiji

Senior Member
Joined
May 1, 2014
Posts
173
Reaction score
250
Mwaka juzi nilichaguliwa Chuo cha Mwenge kule Moshi lkn sikufanikiwa kwenda kutokana na hali ngumu ya kiuchumi. Sikuwa na hela hata kidogo na wakati huo ndo nilikua nimetoka form six. Home wazazi ni hohehahe wa kutupwa hawana mbele Wala nyuma.

Sikupata mkopo hata ASILIMIA sifuri hivyo nikaamua kuahirisha masomo nipambane mtaani.

Nikaanza kufanya vibarua kwenye mashamba ya mpunga kule ifakara. Nikapambana nikapata hela kidogo nikaenda maeneo ya kibaigwa nikakodi shamba ekari tatu za mahindi.

Huku kibaigwa Kuna mjomba angu mmoja ndo nikawa nakaa kwake. Nimelima kwa kujibana Sana Nikapata gunia kumi za mahindi. Nilivyouza nikapata laki sita nikaenda kukodi ekari tano huko huko zikawa Saba.

Nikalimia vizuri mwaka Jana kuanzia Novemba. Mahindi yalistawi Sana nikajipa imani kuwa mwaka huu lazima nikaanze chuo maana Kama ningevuna vizuri nisingekosa gunia 50 za mahindi na ningeyauza nisingekosa chini ya million mbili na nusu.

Hii ingetosha kabisa kulipia ada na michango mingine ya chuo.

Wakati napanga hayo mvua kubwa ikaendelea kunyesha. Mashamba yangu yalikua mbugani hivo yaliharibiwa Sana na mvua. Wakulima wa mbugani wanajua jinsi mvua ya mwaka huu ilivyotuletea hasara.

Hivyo sikufanikiwa kuvuna hata debe Moja na hivo sikurudisha hata Mia.

Baada ya kupata hasara hiyo kidogo nichanganyikiwe ndo nikaenda Dodoma kwa ndugu yangu mmoja akawa ananipa bodaboda nafanya deiwaka.

Nimefanya kwa muda wa miezi kadhaa, akapata matatizo akaiuza boda yake hivo hata riziki kidogo nikaacha kupata.

Nilikua nimekusanya Kama laki mbili hivi nikaenda veta kusoma driving. Sasa Nina cheti Cha udereva ila bado Sina leseni. Nikaanza kupambana Tena mtaani.

Nikawa nasaidia mafundi kujenga ila malipo ni ya kutosheleza Kula tu siwez kusevu kwa ajili ya kulipia Ada endapo nitaamua kwenda chuo mwezi wa 11.

Nipo hapa nimechanganyikiwa kabisa Sina Hili Wala lile. Nataman Sana nikasome ila sijion nikitimiza lengo Hilo.

Nikawaza nije humu jukwaan mnisaidie Moja kati ya haya yafuatayo.

(1) kazi

Kama mtu Ana kazi yoyote halali yenye malipo mazuri (kutosheleza Kula na kusevu kidogo kwa ajili ya Ada) anipe connection.

Nipo vizuri kwenye kompyuta, sales management n.k

Mapishi pia nayaweza Sana. Kuuza duka, stationary, na hata kuwa houseboy wa mtu ni sawa kwangu. Napendekeza kazi iwe Dodoma ila hata mikoani Niko Tayari Kama itakua na maslahi.

2. Mtu mwenye bodaboda aniajiri kwa hesabu ya siku au kwa mkataba. Nitafanya kazi kwa uaminifu mkubwa Sana Hadi tajiri utafurahi.

3. Mtu anayeweza kuniajiri kwenye gari. Ingawa bado Sina leseni ila akitokea mtu akanipa gari nauza hii simu chapu ( thaman yake ni 90 elfu) naenda kukata leseni daraja D ambayo ni elfu sabini.

Nikipata gari dogo Kama kirikuu itakua vema. Au Kama Kuna kampuni inahitaji dereva naomba connection.

Ikiwa dodoma itapendeza zaidi.

Naombeni msaada ndugu zangu nipo Dodoma
 
Polee Sanaa ndugu...

Hyo mvua binafsi imeniathiri ktk kilimo changu cha mpunga huwez amini eka moja mtu unapata gunia 3 adi 2...

Kuna jamaa yngu nae alilima ufuta pande za Kilwa katoka patupu hajarudisha ata cent..

So,usijihisi vibaya ktk Hilo janga,ni janga la taifa kila mkulima limemgusa so usikate tamaa.

Sina kazi ya kukuajiri Ila nina mawazo ya kukupa ili ufikie malengo yake.
1:- Jipange urudi tena ktk kilimo cha maindi naamini unauzoefu wa kutosha ktk hcho kilimo,pia naamini mwakani ni mwaka hali ya hewa itakuwa shwari kwa wakulima hvyo usikate tamaa.

2:- Kabla hujafikiria kuajiriwa embu kaa chini fikiria wazo zuri la biashara ambayo utaweza kuiendesha upate chochote kitu,jaribu kuwa mbunifu kulingana na changamoto zinazokuzunguka.
Najua utasema tatizo mtaji Ila amini mtaji upo Ila tatizo mawazo.(money is all about an idea that why we have a business idea)

Tengeneza idea nzur ya biashara theni itengenezee business plan yako nzuri na iwe simple tu afu feel as if unaimiliki na unaiendesha hyo biashara...then washirkishe watu wako wa karibu kuhusu hyo idea yako ikiwezekana ata apa jf ilete watu wenye uzoefu nayo watakupa mwangaza.

3:- naomba uamini kwenda chuo si ndio kutoboa maisha...usijihisi mpweke hyo elimu uliyo nayo apo inatosha kwako kukuwezesha kutoboa life.

Mwisho Kama upo tayar kushare na mimi mawili matatu kuhusu idea mbalimbali za biashara ni pm mkuu...Mana nami nipo ktk kupambana japo namalizia degree yangu niingie mtaani kupambana kikamili.

Kama utapata pa kujishikiza nakuomba fungamana na vtu hivi.
1. Uamini
2.kujituma
3.subira (uvumilivu)
4.nidhamu
 
Mkuu pole sana na ninakuomba usichoke endelea kupambana hata sisi wengine tumetoka huko huko. Style hiyo ya maisha ndiyo wazazi wote wanaojiita wanyonge wamechagua watoto wao wapitie, maana chama Chao kile kinachoitwa chama tawala au chama bora Africa ndo kimetutengenezea style hii ya maisha Kama wewe ni mtoto wa mnyonge basi your future is highly uncertain
 
Dogo achana na story za chuo kabisa. Tafuta kazi upate mtaji ufungue biashara. Ajira hamna.

Watu tuna Masters zetu ila tupo tu tunashinda jf kusoma story za kula tunda kimasihara.

Sent from my Infinix Zero 3 using JamiiForums mobile app
hana refaree wakumpa school fee je referee wa kumpa kazi atapata wapi?
 
Ebu ngoja nikupe connection...
Upate kirikuu.
Na kama ukifanikiwa, utaleta hesabu ya ngapi kwa siku..??
Are you sure kwamba ukipata utauza simu na upate leseni..??
Na what if akihitajika mdhamini, utakuanae..??
Naomba namba yako ya simu nikupigie.
 
Polee Sanaa ndugu...

Hyo mvua binafsi imeniathiri ktk kilimo changu cha mpunga huwez amini eka moja mtu unapata gunia 3 adi 2...

Kuna jamaa yngu nae alilima ufuta pande za Kilwa katoka patupu hajarudisha ata cent..

So,usijihisi vibaya ktk Hilo janga,ni janga la taifa kila mkulima limemgusa so usikate tamaa.

Sina kazi ya kukuajiri Ila nina mawazo ya kukupa ili ufikie malengo yake.
1:- Jipange urudi tena ktk kilimo cha maindi naamini unauzoefu wa kutosha ktk hcho kilimo,pia naamini mwakani ni mwaka hali ya hewa itakuwa shwari kwa wakulima hvyo usikate tamaa.

2:- Kabla hujafikiria kuajiriwa embu kaa chini fikiria wazo zuri la biashara ambayo utaweza kuiendesha upate chochote kitu,jaribu kuwa mbunifu kulingana na changamoto zinazokuzunguka.
Najua utasema tatizo mtaji Ila amini mtaji upo Ila tatizo mawazo.(money is all about an idea that why we have a business idea)

Tengeneza idea nzur ya biashara theni itengenezee business plan yako nzuri na iwe simple tu afu feel as if unaimiliki na unaiendesha hyo biashara...then washirkishe watu wako wa karibu kuhusu hyo idea yako ikiwezekana ata apa jf ilete watu wenye uzoefu nayo watakupa mwangaza.

3:- naomba uamini kwenda chuo si ndio kutoboa maisha...usijihisi mpweke hyo elimu uliyo nayo apo inatosha kwako kukuwezesha kutoboa life.

Mwisho Kama upo tayar kushare na mimi mawili matatu kuhusu idea mbalimbali za biashara ni pm mkuu...Mana nami nipo ktk kupambana japo namalizia degree yangu niingie mtaani kupambana kikamili.

Kama utapata pa kujishikiza nakuomba fungamana na vtu hivi.
1. Uamini
2.kujituma
3.subira (uvumilivu)
4.nidhamu
Chukueni form mgombee ubunge.
 
Tafuta sehem nzur fungua kibanda cha fast food weka na juic nzur maeneo ya chuo au penye mkusanyiko mkubwa

Tumia hiyo fursa kupata ada na connection ya wanafunz wenzako kuku ungisha kweny biashara yako

Naamin ukipambana utapata mtaji wa kuanza nao
 
Hapo niwaka 2014 uliandika uzi kwamba upo kidato cha tano na haujawahi kufanya mapenzi.

Then 2017, ukaandika uzi kwamba upo chuo mwaka wa kwanza.

Kisha 2017, ukaandika tena kwamba umefeli kidato cha nne na ukahitaji usaidiwe usifeli maisha.

Leo 2020 umekuja na uzi kwamba mwaka juzi (2018) ulichaguliwa kujiunga na chuo cha Mwenge huko Moshi.

Sasa nimejaribu kutafakari na nikajikuta ninapata mashaka kidogo mkuu, ebu nieleweshe pengine nisije nikawa ninakuwazia tofauti na nikachuma dhambi bure.
IMG_20200718_124136.jpg
IMG_20200718_123824.jpg
IMG_20200718_123414.jpg
IMG_20200718_123212.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom