Hawa YONO wamepewa mamlaka na nani?

dev senior

JF-Expert Member
Aug 12, 2012
458
557
Habari zenu wakuu..

Siku ya leo asubuhi ilinikuta kasumba iliyonikasirisha kupita maelezo, ikiwa ni mara ya pili ndani ya wiki hii moja nimepigwa faini ya jumla ya pesa taslimu laki moja na themanini elfu (180,000) na hawa watu wanaokamata magari maeneo ya mjini maarufu kwa jina la YONO (tambaza auction mart & general broker).

Nakiri kwamba, mara ile ya kwanza nilikuwa nimefanya kosa. kwa sababu nilipaki sehemu sio, nikimsubiri mtu pembezoni ya barabara maeneo ya gerezani...japo sehemu ile niliyopaki kulikua hakuna kiashiria chochote ninachokataza kupaki eneo lile... baada ya dakika takribani 4 kundi la watu kama watano walinivamia na kujitambulisha kama mawakala wa YONO ( tambaza auction mart), na kuniambia kwamba nimefanya kosa ivyo natakiwa niende yard yao iliyopo keko nikalipe faini hiyo 50,000.

Ndipo nilipoenda na wale jamaa mpaka kwenye jengo ilo la serikali, na nikaacha gari hapo nakwenda kulipa pesa hiyo benki ya crdb, na kisha kupeleka pay-in-slip halmashauri... lakini cha ajabu nilipofika pale na kuwaonyesha stakabadhi za halmashauri, walinikabidhi gate-pass yakutolea gari pale yard, na kwakuwa nilikuwa na haraka sikubishana nao, lakini nikawauliza hii ndo risiti ya kuonyesha kwamba nimelipa hii faini.

Yule mdada ambaye ni muhudumu hakuwa na jipu zaidi ya kuniambia "onyesha hii gate-pass pale mlangoni watakuruhusu"...siku ile gate-pass niliwaachia.

Sasa leo hii ilikuwa hivi, nilipita mtaa fulani maeneo ya kariakoo, na nilipofika kwa mbele kuumaliza huo mtaa nikakutana na noah ambayo ilinisimamisha na vijana kama wanne wa YONO wakatoka kwenye ile noah... wakaniambia mzee umefanya kosa, nikauliza kosa gani, wakasema umepita kinyume na one way-drive...

Nikauliza kibao kinachoonyesha one way-drive kiko wapi? twendeni mkanionyeshe na nitalipa faini bila hivyo silipi hii faini, ndipo mabishano yaliendelea na wao kugoma katukatu kunielekeza wapi kilipo hicho kibao kilipo... mabishano yalipozidi ndipo wakaita break-down na kuichukua gari yangu mpaka yard yao keko....

Nilipofika keko wakaniambia nikalipe laki moja na thelathini 130,000, nikauliza je, ni lazima niende benki kulipa? Wakaniambia lipa hapo kwa cashier..

Kwa kweli nilikuwa na hasira, leo nilikasirika, hela yenyewe kuipata ilivyokuwa shida namna hii hawa jamaa wananifanyia SIFA namna hii yani wananikomoa.... Kwa kweli nilitamani kulia.... lakini kama ilivyokuwa mara ya kwanza, baada ya kujichanga na kukopa kwa marafiki zangu nilienda kulipa pesa hiyo... lakini cha ajabu sikupewa risiti, na niliuliza kama mara ya kwanza..risiti iko wapi, je kama nimelipa nitajuaje kwamba hii hela imeenda serikalini au halmashauri... yule mdada cashier anayetoa gate-pass akakosa jibu... nikasema hili swala lazima niliulizie maswali...

Hawa YONO nani kawapa mamlaka ya kukamata magari maeneo ya mjini, je ni jeshi la polisi na usalama barabarani au ni halmashauri ya jiji? Kwanini wanatoza faini pasipo kutoa risiti?

Je, hawa watu ni matapeli? Na kwanini hawa watu wanatumia majengo ya serikali, kuendesha shughuli zao?

Je, wizara ya mambo ya ndani imeshindwa kutumia jeshi la polisi kuendesha operation kama hizi?

Gate-pass yenyewe hii hapa..

345454-2fd661096eab982f1bb0ab0e361e3109.jpg


Kwa kweli leo nimejiuliza maswali mengi wakuu.. Kwa dhati naomba kufahamishwa kuhusu hawa wanyang'anyi..
 

Attachments

  • tambaza auction.jpg
    tambaza auction.jpg
    237 KB · Views: 48
Dawa unakariri afu unaanza tengua kiuno mmoja mmoja hakika wataikimbia hiyo kazi
 
Kuna kipindi Meki Sadik aliwapiga marufuku. Sasa naona wameibuka na makonda.
 
Hapa Dar barabara nyingi hazina alama sitahiki. Tunaendeshea uzoefu tu na sio alama
 
Wewe ndio umewalea kukubali gari yko ivutwe n breakdown hpo ulifanya kosa
mkuu sijawalea wala nini, ni hivi trafiki anakusimamisha maana ndo wao wanaoweza fanya hivyo, baada ya hapo kesi inachukuliwa na hao wahuni... alafu isitoshe unajikuta uko peke yako umezongwa na watu takribani watano... baada ya hapo wanachukua gari yako na break-down.. usiseme nimewalea, leo ningekua na bastola ningejerui...
 
Dawa unakariri afu unaanza tengua kiuno mmoja mmoja hakika wataikimbia hiyo kazi
Mkuu umeongea point sana me nishawai kumkanyaga vidole mmoja post kanikuta nime simama niamshusha ananiambia long packing nikamwambia unaelewa maana ya ku pck na kusimama akujibu nikamwambia packing ni dereva kushuka ila me sijashuka alaf isitoshe umeona kabisa na mshusha mtu bas yy katoa michuma yake naanza kufunga nikamwambia usifunge akabisha nilichofanya nikapandisha kioo nikaweka D kilichomotokea atokisahau
 
mkuu sijawalea wala nini, ni hivi trafiki anakusimamisha maana ndo wao wanaoweza fanya hivyo, baada ya hapo kesi inachukuliwa na hao wahuni... alafu isitoshe unajikuta uko peke yako umezongwa na watu takribani watano... baada ya hapo wanachukua gari yako na break-down.. usiseme nimewalea, leo ningekua na bastola ningejerui...
Pole sana huo ni uwizi wa kimachomacho wrong parking huwa 50000 tu

Sent from my SM-G7102 using JamiiForums mobile app
 
Ungewambia wakupeleke mahakamani pia hizo faini zao za bila risiti wanatoa Kwa mamlaka ipi sababu hata wale wakamataji ukitupa taka barabara wanakupa vifungu vya sheria ya jiji pia kutokuwa na alama ashira barabarani hayo ni mapungufu ya mamlaka husika
,Pia kuna haja ya Yono kutuweka wazi tujue shughuli zao na pia wawe wakitupa maelezo wanafanya Kazi kama nani au kwa mamlaka IPI ili tujue usalama wa Pesa zetu je zinaingia serikalini au kwenye mifuko IPI .
 
Kwanza pole kwa yaliyokukuta, iwe ulifanya kosa kwa bahati mbaya, au kwa makusudi au umeonewa hapakuwa na kosa. Kwa hali yoyote iwayo kwenye nilizotaja hapo juu ninasema pole. Baada ya hapo ninaomba niendelee na mchango wangu kwenye mada yako.
Mimi binafsi masuala haya ya taasisi za serikali kutumia makampuni binafsi kwenye mambo kama haya ya kukamata wavunja sheria kama hizi za matumizi mabaya ya barabara au kukwepa kulipa kodi za serikali na mambo mengine yanayofanana na haya ni jambo linaloniudhi na kunikera kupita maelezo. Sisi tukiwa kama raia hatuoni sababu za msingi zinazoifanya serikali ishindwe kuwatumia watumishi wake ambao imewaajiri na inawalipa mishahara kama polisi, n.k hadi wanachukua makampuni binafsi ambayo yapo ki-biashara na lengo lao ni kutengeneza faida. Yanapewa kazi kama hizi, ambapo wakati mwingine wanafanya Uonevu na wanawakandamiza na kuwabambika makosa wananchi pasipo kuwepo makosa ya dhahili. Kumbuka kampuni hizi zimeajiri wafanyakazi na wafanyakazi hawa wanalipwa mishahara. Sasa endapo raia waliofanya makosa watakuwa wachache hawa wafanyakazi wa hizi kampuni watalipwa nini. Hapo ndipo wanapolazimisha makosa kwa wananchi. Pia viwango vya faini vinavyotozwa haviko wazi. (Hayajaainishwa makosa na adhabu zake) Vile vile serikali umejiridhisha vipi kuwa akaunti yanakofanyika malipo ndizo akaunti sahihi ili baadae waweze kujiridhisha kuwa kinachostahili kwenye serikalini au kwenye Halimashauri ndicho kilichokusanywa kweli?. Pia hizi yard yanakozuiliwa magari zimekuwa ni sehemu za kuwaibia wananchi pia, mfano gari yako inakamatwa na YONO pale kibaha kwa issues za mapato ya TRA kumbe imekamatwa kimakosa baadae unaleta uthibitisho kuwa hakuna unachodaiwa ilikamatwa kimakosa, jambo la kushangaza unalipishwa garama ya gari kukaa yard na ili hali gari yako haikuwa na tatizo lolote. Huu ni wizi na ni uonevu mkubwa kwa wananchi.
Mimi ninapenda kutoa ANGALIZO ama kwa serikali kuu au kwa Halimashauri zinazotoa hizi kazi kwa haya makampuni kuwa vitendo hivi wanavyovifanya hawa wafanyakazi wa hizi kampuni vya uonevu itafika mahala raia watachoka hivyo itapelekea Uvunjifu wa Amani.
Serikali itumie wafanyakazi wake kufanya hizi kazi na si kuzipa kampuni binafsi zikatumia nafasi hiyo kuonea wananchi kwa lengo la wao kutengeneza faida.
Mamlaka zinazohusika pia zitimize wajibu wao kabla ya kukimbilia kutoa adabu. Mfano dreva anapotumia barabara anafuata alama na michoro iliyopo barabarani kumuongoza. Lakini kuna baadhi ya mitaa huko kariakoo haina alama za barabarani, zingine ama zimefutika ama zilikuwepo zimeondolewa na zingine ziko mahali ambapo haionekani kwa urahisi. Hivyo hawa wanaopewa jukumu la kukamata wanatumia mapungufu hayo kujinufaisha. Na hawachukui hatua za kuondoa mapungufu hayo kwakuwa yanawanufaisha na huu ndio uonevu tunao ulalamikia.
 
Habari zenu wakuu..

Siku ya leo asubuhi ilinikuta kasumba iliyonikasirisha kupita maelezo, ikiwa ni mara ya pili ndani ya wiki hii moja nimepigwa faini ya jumla ya pesa taslimu laki moja na themanini elfu (180,000) na hawa watu wanaokamata magari maeneo ya mjini maarufu kwa jina la YONO (tambaza auction mart & general broker).

Nakiri kwamba, mara ile ya kwanza nilikuwa nimefanya kosa. kwa sababu nilipaki sehemu sio, nikimsubiri mtu pembezoni ya barabara maeneo ya gerezani...japo sehemu ile niliyopaki kulikua hakuna kiashiria chochote ninachokataza kupaki eneo lile... baada ya dakika takribani 4 kundi la watu kama watano walinivamia na kujitambulisha kama mawakala wa YONO ( tambaza auction mart), na kuniambia kwamba nimefanya kosa ivyo natakiwa niende yard yao iliyopo keko nikalipe faini hiyo 50,000.

Ndipo nilipoenda na wale jamaa mpaka kwenye jengo ilo la serikali, na nikaacha gari hapo nakwenda kulipa pesa hiyo benki ya crdb, na kisha kupeleka pay-in-slip halmashauri... lakini cha ajabu nilipofika pale na kuwaonyesha stakabadhi za halmashauri, walinikabidhi gate-pass yakutolea gari pale yard, na kwakuwa nilikuwa na haraka sikubishana nao, lakini nikawauliza hii ndo risiti ya kuonyesha kwamba nimelipa hii faini.

Yule mdada ambaye ni muhudumu hakuwa na jipu zaidi ya kuniambia "onyesha hii gate-pass pale mlangoni watakuruhusu"...siku ile gate-pass niliwaachia.

Sasa leo hii ilikuwa hivi, nilipita mtaa fulani maeneo ya kariakoo, na nilipofika kwa mbele kuumaliza huo mtaa nikakutana na noah ambayo ilinisimamisha na vijana kama wanne wa YONO wakatoka kwenye ile noah... wakaniambia mzee umefanya kosa, nikauliza kosa gani, wakasema umepita kinyume na one way-drive...

Nikauliza kibao kinachoonyesha one way-drive kiko wapi? twendeni mkanionyeshe na nitalipa faini bila hivyo silipi hii faini, ndipo mabishano yaliendelea na wao kugoma katukatu kunielekeza wapi kilipo hicho kibao kilipo... mabishano yalipozidi ndipo wakaita break-down na kuichukua gari yangu mpaka yard yao keko....

Nilipofika keko wakaniambia nikalipe laki moja na thelathini 130,000, nikauliza je, ni lazima niende benki kulipa? Wakaniambia lipa hapo kwa cashier..

Kwa kweli nilikuwa na hasira, leo nilikasirika, hela yenyewe kuipata ilivyokuwa shida namna hii hawa jamaa wananifanyia SIFA namna hii yani wananikomoa.... Kwa kweli nilitamani kulia.... lakini kama ilivyokuwa mara ya kwanza, baada ya kujichanga na kukopa kwa marafiki zangu nilienda kulipa pesa hiyo... lakini cha ajabu sikupewa risiti, na niliuliza kama mara ya kwanza..risiti iko wapi, je kama nimelipa nitajuaje kwamba hii hela imeenda serikalini au halmashauri... yule mdada cashier anayetoa gate-pass akakosa jibu... nikasema hili swala lazima niliulizie maswali...

Hawa YONO nani kawapa mamlaka ya kukamata magari maeneo ya mjini, je ni jeshi la polisi na usalama barabarani au ni halmashauri ya jiji? Kwanini wanatoza faini pasipo kutoa risiti?

Je, hawa watu ni matapeli? Na kwanini hawa watu wanatumia majengo ya serikali, kuendesha shughuli zao?

Je, wizara ya mambo ya ndani imeshindwa kutumia jeshi la polisi kuendesha operation kama hizi?

Gate-pass yenyewe hii hapa..

345454-2fd661096eab982f1bb0ab0e361e3109.jpg


Kwa kweli leo nimejiuliza maswali mengi wakuu.. Kwa dhati naomba kufahamishwa kuhusu hawa wanyang'anyi..
Huyo dada hajakuuliza kwamba umetoka hapo yard yao siku ya nyuma? Lazima atakuona wewe ni tajiri sana, na lazima alikwambia karibu tena.
 
Back
Top Bottom