Hawa ndio watu wanaonikera zaidi

Kambi ya Fisi

JF-Expert Member
Feb 3, 2018
13,480
21,955
Yaani wananikera sana hawa watu watatu...

1. Watu wenye PhD feki

Ni watu wanaojivika PhD pasipo kuhudhuria masomo yoyote chuo kikuu.

Hivi kwa nini wadanganye kile wanacho weza kukipata kwa heshima?

Kuna vyuo vingi sana vinavyoaminika hivyo badala ya kujipachika PhD feki waende chuo kikuu na wakafurahie uzoefu wote wa masomo ndipo waipate hiyo PhD.

2. Watenda miujiza feki makanisani

Watu hawa hudanganya kwamba wana nguvu za Mungu na wengi wao hutembea huku wakilindwa na mabaunsa walio Waajiri

Ni waongo na hata hiyo miujiza feki huwauzia watu kwa kutoza hela nyingi (sadaka) ili wajipatie hela za kula bata na makahaba huko nightclubs ila kiukweli sio watumishi wa Mungu bali ni wahuni fulani tu.

3. Marais wala rushwa

Wanapata mshahara zaidi kuliko raia,hawalipi bili yoyote lakini hawaridhiki.

Wao hufurahi wanapoona mamilioni ya watu wakitumbukia katika umaskini, huwa hawana mipango ya kustawisha jamii, bali mipango yao ni kujinufaisha kibinafsi na familia zao.

Kiukweli kiongozi wa juu anapokuwa fisadi huiporomosha serikali yake yote.

Mabadiliko huanza na kichwa. Kichwa kinapoharibika mwili wote huharibika.

#Nani anakukera zaidi?
 
Yaani wananikera sana hawa watu watatu...

1. Watu wenye PhD feki.
Ni watu wanaojivika PhD pasipo kuhudhuria masomo yoyote chuo kikuu.

Hivi kwa nini wadanganye kile wanacho weza kukipata kwa heshima?

Kuna vyuo vingi sana vinavyoaminika hivyo badala ya kujipachika PhD feki waende chuo kikuu na wakafurahie uzoefu wote wa masomo ndipo waipate hiyo PhD.

2. Watenda miujiza feki makanisani.
Watu hawa hudanganya kwamba wana nguvu za Mungu na wengi wao hutembea huku wakilindwa na mabaunsa walio Waajiri

Ni waongo na hata hiyo miujiza feki huwauzia watu kwa kutoza hela nyingi (sadaka) ili wajipatie hela za kula bata na makahaba huko nightclubs ila kiukweli sio watumishi wa Mungu bali ni wahuni fulani tu.

3. Marais wala rushwa.
Wanapata mshahara zaidi kuliko raia,hawalipi bili yoyote lakini hawaridhiki.

Wao hufurahi wanapoona mamilioni ya watu wakitumbukia katika umaskini, huwa hawana mipango ya kustawisha jamii, bali mipango yao ni kujinufaisha kibinafsi na familia zao.

Kiukweli kiongozi wa juu anapokuwa fisadi huiporomosha serikali yake yote.
Mabadiliko huanza na kichwa. Kichwa kinapoharibika mwili wote huharibika.

#Nani anakukera zaidi?
Ke wenye makalio, nywele, ngozi, maziwa, hipsi, kucha, nyusi feki hawakukeri, huoni wauziwa mbuzi kwenye gunia hata K ikawa bandia?

Ubinadamu ni kazi/Humanity is a work.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Wanaojipongeza timu yetu kupata point mbili na goli moja

😄😄😄kweli? Eti tumepambana serious? Tumeiprove?

Timu katika miaka 34+ imefuzu mara 3 AFCON
 
Back
Top Bottom