The_Analyst
JF-Expert Member
- Nov 25, 2008
- 243
- 86
...nasubiria sura yake kwenye noti...
Wasira huyu huyu mzee wa gombe,mweee!!!!!!!!!!!
Lakinii PIA ni AJABU kupata kura HIZO kaanza kuifanyia kazi CCM Miaka 2 iliyopita sio WENGI wanaomfahamu - Hana PURUKUSHANI kama NAPE NNAUYE au MCHEMBA
Kwahiyo HE DID VERY WELL...
Kwahiyo nchemba kampita kwa kura kutokana na purukushani? kati ya purukushani na utendaji, purukushani reigns?
Da nilikuwa staki kuchangia thread hii lakini baada ya kuona mchango wako leo uko katika aina hii ya uchangiaji,kwa mara yangu ya kwanza naona leo wewe umekuwa critics wa CCM publically hivi.CCM imegeuka kuwa chama cha ajabu sana; Yani Katibu Mkuu wa Chama aliyepo madarakani anaponea chupuchupu kwa kushika nafasi ya tisa kwa idadi ya kura, kati ya jumla ya idadi inayotakiwa ya watu kumi?
Mambo kama haya hayajawahi kutokea; Ina maana huyu Katibu Mkuu alikuwa anafanyeje kazi na viongozi waliomshinda kura ambao technically ni junior kwake kicheo ndani ya chama, hasa yeye akiwa ndio mtendaji mkuu - Kina nchemba, Makamba, Shigela? Hii inatoa ishara gani kuhusu nani ndio alikuwa anakiendesha chama, na nani atakiendesha chama kuelekewa 2015 na kwwa malengo yepi? Kwa kweli matokeo haya yametoa picha very interesting kuhusu jinsi gani chama hiki hakitaisha na migogoro;
Vinginevyo naona majina mawili tu ambayo yatajenga, mengine yatabomoa tu zaidi!
Mkuu,
Hiyo inaonyesha kuwa demokrasia imefuata mkondo wake, pia hiyo ni 'statement' na 'verdict' kuonyesha kuwa utendaji wake kama katibu mkuu ulikuwa haukizi matarajio ya wana CCM wengi. Nitashangaa kama ataendelea tena kuwa katibu mkuu.
Ninawapongeza waasisi wa CCM kwa kuwa na maono ya mbali na kukata mrija wa demokrasia katika nafasi ya mwenyekiti taifa kwa sababu ninaamini wameepusha aibu isimfike 'incumbent' wa mwaka huu kwa sababu utendaji wake katika chama na serikali.
Labda tu niseme na kupingana nawe kidogo. Utendaji wa CCM hautegemei sana mtu mmoja kama ilivyo katika vyama vingine na ndiyo maana pamoja na udhaifu wa hali ya juu aliyoonyesha Mukama, CCM bado haikuyumba sana katika utekelezaji wa majukumu yake ya kawaida. Halafu unasahau kuwa haya majina ni muendelezo wa wajumbe wa NEC waliochaguliwa kupitia wilaya zao.
Kuna habari ziliwahi kuvuja kwamba Mukama alimuandikia barua mwenyekiti wake akitaka kuachia ngazi ya ukatibu mkuu, kwamba nape na mwigulu walikuwa wamejitwalia madaraka ya kukiendesha chama kama mali yao, nadhani hiyo inaweza kuthibitisha kwamba hakuwa na nguvu ya kutosha kukiongoza chama, na hayo matokeo yameonyesha ukweli wa mambo.
Kwa mtazamo wangu Mukama kuwania nafasi ya UNEC ni kuthibitisha kwamba ccm inatarajia kujipatia katibu mkuu mwingine kipindi hiki, atakayejaza nafasi ya Mukama.
Mchambuzi,
Haumfahamu Mukama. Huyu ni mmoja kati viongozi wachache sana ndani ya CCM asiyejua kuhonga, asiyejua kununua kura, hana maswahiba, hana kundi wala kambi ndani ya CCM. Watu wa aina yake wanachaguliwa kwa taabu sana ndani ya CCM. Mimi nilimshangaa sana alipojitumbukiza kwenye kundi hili. Kura za KIITIFAKI zimemsaidia sana.
Huyo kwenye nyekundu ndo ambae alitakiwa awe our Presidaaa 2005 kabla ya organized mafia haijamcingizia kuhucika na mauaji ya Karume.. Naamini kama tungebahatika kuwa nae as our President tungekuwa na mafanikio zaidi.. Cidhani kama atataka tena kujihusisha na siasa tena.. Kiongozi muadilifu kama yeye ana ethics zake.. Hao wengine uliowataja mh..
...hii bidhaa ya uraisi ndani ya CCM imekuwa bei raisi sana kila mtu anauwezo wa kununua...sitoshangaa mbele ya safari kunako majaaliwa Mulugo nae akajitosa...