Hawa 'Maprince' wanaendeleaje?

Hawa 'Maprince' wanaendeleaje?

Wabunge wa Chalinze (Ridhiwani Kikwete) na wa Kalenga (Geofrey Mgimwa) wanaendeleaje? Hawa wote ni 'wana mfalme' walorithi mikoba ya uongozi toka kwa baba zao wazazi. Ridhiwani Kikwete ni mtoto wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete aliyewahi kuwa Mbunge wa Chalinze. Naye Geofrey Mgimwa ni mtoto wa aliyekuwa Mbunge wa Kalenga hayati Dr. Mgimwa.

Hawa Wabunge wote wamerithi mikoba ya baba zao katika chaguzi ndogo. Wanaendeleaje Maprince hawa na utimizaji wa ahadi zao? Bungeni wako kimya sana kwakweli.

....hawa waliomba kugombea, wakapitishwa na chama chao, wakafanya kampeni, wengi wa wapiga kura ktk majimbo yao wakawaelewa na kuafiki kuwa wanafaa kuaminiwa kuwa wawakilishi wao, wakawapa kura...hakuna u prince hapo kamanda, ila tu kama demokrasia unaitafsiri kivyako ktk kujiliwaza, au chuki binafs, au wivu....au "xxx"
 
Mbona safari hii wameongezeka sana? Ona huyu prince Warioba na princes Bulembo aliyekwisha pitishwa viti maalum. Ccm si ya wote bali ya wachache wenye nayo. Bora kife tuanze mwanzo.
 
Mbona safari hii wameongezeka sana? Ona huyu prince Warioba na princes Bulembo aliyekwisha pitishwa viti maalum. Ccm si ya wote bali ya wachache wenye nayo. Bora kife tuanze mwanzo.

Nikisikia viti maalum sijui najisikiaje,kizembezembe tu mtu ananyaka 8M+ kwa mwezi. UKAWA waingie wafute hizi kitu.


Uwoya aliishia wapi?
 
Anakuja Prince mwingine huko Ulanga Mashariki ehehehe
 
Nikisikia viti maalum sijui najisikiaje,kizembezembe tu mtu ananyaka 8M+ kwa mwezi. UKAWA waingie wafute hizi kitu.


Uwoya aliishia wapi?

Uwoya alishinda kwa kapu la vijana!Kama CCM watapata wabunge wengi wa Majimbo na kura nyingi za U Rais basi tutamuona Uwoya na Juliana Shonza Dodoma

What a hectic shame?
 
Last edited by a moderator:
Ndugu Petro E. Mselewa mwana mfalme Geofrey Mgimwa yeye kisheria ndo Prince hasa kwa tafsiri halisi ya mwana mfalme kwa kuwa alirithishwa kiti baada ya kifo cha baba yake. Ndugu Ridhwan Kikwete si mwanamfalme kwa tafsiri ya kurithishwa kwa maana hakupokea kijiti toka kwa baba yake isipokuwa alichukua toka kwa bwana mdogo. Hivyo basi tuweke kumbu kumbu sawa kwa kumtambua ndugu Ridhwan kama mwana wa ukoo wa Mfalme! Narudisha hoja kwako mtoa mada!

Kumbuka Bwana Mdogo inasadikika ni MJOMBA...................
 
Back
Top Bottom