Kiongozi! Usipate tabu. Najua wengi watashangaa hili lakini ndiyo ukweli wenyewe.
Nazi chini ya Adolf Hitler walikuwa na kikundi cha siri kilichoitwa "The Vril" na jina hili asili yake imetokana na jamii ya kale ya Sumeri(Sumerian) ikimaanisha "godlike". Mkuu wa hiki kikundi walikuwa ni mwanamke kwa jina ni Maria Orsic. Huyu mwanamke alikuwa na uwezo wa ajabu, alikuwa ana communicate with extraterrestrials na hayo maelekezo aliyokuwa akiyapata ndiyo teknolojia ya hali ya juu ambayo Nazi walikuwa nayo. Hayo maelekezo alikuwa anayatamka kwa lugha mbili(alikuwa hana tofauti na waganga wa kienyeji wakipandisha mizimwi). Lugha ya kwanza hata yeye mwenyewe alikuwa haielewi ni lugha gani. Lugha ya pili ni lugha ambayo inavinasaba na kijerumani cha kale ilikuwa inatumiwa na jamii ya " THULE". Jamii ya THULE ilikuwa ni jamii inayotumia uchawi.
Hizo lugha akizitamka wajumbe wengine walikuwa wanaandika hayo maelekezo na baada ya Maria Orsic kumaliza kuongea asichokielewa wanaanza kutafsiri yale maelekezo na hayo maelekezo ndiyo yamefanya Nazi kuwa na teknolojia ya hali ya juu. Miongoni mwa mwanasayansi wa Hitler ambaye alichukuliwa na Wamerikani baada ya Ujerumani kushindwa vita alikiri hili waziwazi kabisa. Hata kutengeneza flying saucer ni maelekezo kutoka kwa hawa viumbe. Huyu mwanasayansi anaitwa Hermann Oberth Von Brawn.
Kuna vitu hapa inabidi viangaliwe. Kwa nini "THE VRIL" asili ya jina lao ni la Sumeri? Ukisoma history Sumeri ni moja ya tawala kongwe hapo mashariki ya kati, ni tawala ambayo iliyopiga hatua kubwa kwa nyakati yake na baada ya tawala yao kuanguka Babylon ikanyanyuka na ikachukua mila, tamaduni na ustaarabu kama wa Sumeri, na vyanzo vinasema asili ya uchawi ni Babylon ambao tamaduni za Sumeri.
Kwa kifupi Wazungu wanatumia majini(mizimwi) katika mambo yao. Ili kuficha haya mambo ndiyo wanaongopa wanasema ni Aliens. Hamna aliens wanaofika kwenye mfumo wa sayari yetu. Isipokuwa wana communicate na majini na majini wapo wa aina mbalimbali, wapo weupe, wa bluu, wekundu, wakijani na wanapaa vilevile.