Hawa hawastahili kuwa 'Usalama wa Taifa'

Status
Not open for further replies.

Consigliere

JF-Expert Member
Sep 9, 2010
12,037
24,595
Wakati nchi ikiendelea kuelea katika mawimbi na Kimbunga cha misukosuko ya kiuchumi, kimaadili, usalama, na kitaaluma, watu tumekujikuta tukiwa katika hamaki kubwa, hatua mbali mbali zimechukuliwa ili kukabiliana na mambo yatokanayo, matokeo yake hatua hizo zimekuwa zikitutumbukiza katika katika matatizo na mifarakano zaidi ya kijamii na kutuacha tukiwa tumegawanyika, na kuona dalili zote za mass mass hysteria at anytime.

Idara ya usalama wa taifa (National Intelligence) ilikuwa ndiyo chombo ambacho tulitegemea kijenge ukuta kati yetu watanzania na hali niliyoitaja au hata itoe red alert kwa policy makers kuhusiano na mabadiliko na mwelekeo tunaoulekea, lakini hali imekuwa ni kinyume cha hapo, idara hiyo imekuwa ikitumika dhidi ya raia wakati mambo yanayowahusu yakizidi kuharibika na kuonekana kama wahusika hawajui na kutambui wajibu wao halisi kwa taifa.

Hali sasa imekuwa mbaya zaidi kwani imeonekana kana kwamba baadhi ya watumishi wa idara hii kutaka na wao kujiinua na kujiweka juu ya sheria kwa kujaribu kutumia nafasi zao kukabiliana na raia kwa kuwatisha na kujaribu kulazimisha mazingira ya kutaka kutambulika wao ni nani and what are they capable of, japo kumekuwa na jitihada za kuisafisha na kuhakikisha idara hii inatimiza majukumu yake ipaswavyo, bado kumekuwepo na watumishi wachache wa idara hii kwa kuongozwa na hulka za kupenda ku-show their real Identity na kuzi-misuse in public kwa ajili ya tabia na matokeo ya ki-binafsi.

Kama taifa, tuna matatizo mengi yanayohitaji ufumbuzi, na mengi yameingia au kuingizwa nchini ikiwa ni matokeo ya idara ya usalama wa taifa kukosa umakini, najua na wengi wetu tunatambua kuwa ni kweli kuna ugumu ambao idara hii huwa inakumbana nao katika utendaji wake, ugumu ambao husababishwa na watunga sera, hata Martin Petersen ambaye ni retired senior CIA Directorate of Intelligence (DI) officer aliwahi ungelea katika moja ya maandiko yake (articles). Kwa maandiko yake Peterson alipata kulalamika kuwa "It is not surprising then that Policymakers do not always see how we can help them" akaendelea kulalamika kuwa unaweza kumfuata policy makers kwa lengo la wewe kuufanya wajibu wako wa kumshauri na kumsaidia namna ya kuliangalia jambo, lakini ataishia kukudharau na kukujibu kuwa:

"After all, I, the policymaker, am smart and have excellent sources of information (including all the ones you have), and I am very busy, so why should I spend some of my most precious commodity on you?"

Hapa najaribu kuonyesha kuwa kuna baadhi ya vikwazo ambavyo idara yetu ya usalama wa taifa imekuwa ikikumbana navyo katika kufanya majukumu yao yapo very global, Uingereza yapo, Marekani yapo, Italy yapo, Russia yapo, na sehemu nyingine nyingi yapo, hivyo wasisuse kwa kuwa mazingira yanawabana kutimiza wajibu wao, bali wana wajibu wa kujifunza na kutengeneza mbinu ya namna ya kukabiliana na changamoto hizo.

Nimemkariri Peterson ili kukiri na kukubali kutambua vikwazo vilivyopo.

Naendelea na upande lengwa uonyeshao namna ambavyo kushindwa huko wakati mwingine na mwingi hausababishwi na Policy makers bali wao wenyewe, na zaidi kwa ulevi wa sifa zitokanazo na kubahatika kuingia katika idara hiyo nyeti na kichwa cha jamii. Mtanisamehe wasomaji sitapiga moja kwa moja bali huu nitaufanya kama mwanzo katika kuelekea kufumua uozo unaofanywa na watumishi wachache wa idara hii wasio waaminifu, nikiwa na mifano halisi na mmoja ukiwa umenitokea binafsi na jamaa mmoja kutoka idara hii nyeti ambaye anafanyia katika NGO moja, naangalia namna ya kushughulika naye ila nimeamua kuufanya huu kama mwanzo.

Pia Nimeandika hapa ili wajiangalie na kujaribu kurekebisha mwenendo wao, na washiriki ktika kulinasua taifa kutoka katika mwelekeo wa kusambaratika. Ujinga wa kudhani wanafahamu kila kitu ndiyo udhaifu unaowafanya wabaki watazamaji katika mambo yanayo wapasa kuyatimiza au kuyagundua yakiwa tayari kwenye vyombo vya habari sawia na sisi raia wengine.

Hivyo wasidhani kuwa wana kazi ngumu ili hali wanaishi maishi mazuri maishi yatokanayo na uwepo wetu sisi kama taifa, kwani waelewe kuwa si na sisi tayari tuna jukumu kubwa na gumu la kuishi katika umaskini na unyonge huu tulio nao. Pia hawakuingia katika idara hiyo ili kutaafuta unafuu wa maisha bali kuitumikia jamii iliyopana na yenye migongano ya kimawazo na wakati mwingine vigeugeu, na zaidi waongeze katika uelewa wao kuwa wao kama ilivyo kwa wanajeshi na polisi si wafanyakazi. Na zaidi wanajukumu la kuto exist.

Watu wa namna hi kama tutaamua kuwaita wajinga na malimbukeni basi tutakuwa tunawakosea nidhamu wajinga na malimbukeni halisi.

Ni afadhali kama una personal issue zishughulikie kwa uwezo wake kama raia mwingine ili kulinda your true Identity na si kutengeneza mazingira ya kutaka watu wakufahamu wewe ni nani, mulewe kuwa jamii ni pana kuliko uwezo wenu wa kufikri unapoishia and you may think that you are snoping us, but be reminded that we are watching you as run in the circles like headless chicken. We are capable in so many and in so less things, but we wont let you know, we will keep on living our life and do the living as we supposed to do.

Tangu kuanzishwa kwake idara hii ya usalama wa taifa ilitegemewa iwe ndiyo an eye and if possible think-tank ya taifa lakini wameacha au hawajui majukumu yao, na sisi tukiwa kama raia tunaoheshimu uhuru wetu, wajibu na mipaka msidhani tunatishika tena na upupu na upumbavu wa baadhi ya watumishi hao wasiojua miiko ya kazi yao, tuna uwezo wa kujilinda na hata kulinda wenzetu iwe kwa mapambano au diplomasi au kisheria, tumeamua kujitwisha jukumu la kufikiri na kujilinda badala ya wao kufanya kazi hiyo kutokana na mapungufu wanayoyaonyesha katika utendaji.

Inawezekana vipi mtu ambaye alichunguzwa na kufuatilia hatua kwa hatua kwa muda wa miaka miwili kabla hajawa enrolled kwenye intake, anarudi uraina akiwa ame qualify mafunzo na kuishia kufanya madudu ya kiwango tukionacho? Unadhani tutabaki tena kuwa na imani ile ile na watu wa idara ya aina hii? Mnaweza mkatupa sababu nzuri ya kwanini tusiingilie kazi zenu na kuzifanya sisi kwa maslahi ya taifa letu na la ya vizazi vijavyo?

Mbegu ili iote na kustawi ni lazima ife sawa nadhani matumizi mabovu ya falsafa hii ndiyo yameharakisha baadhi yenu mlifikishe taifa letu hapa lilipo japo kulikuwa hakuna ulazima wa kuliua.

Ninamaliza kwa kusema sasa itakuwa ni hatua kwa hatua and many more to come...... Si lazima tuwafahamu ninyi bali kuna umuhimu wa ninyi kuufahamu wajibu wenu.
 
Hatuna USALAMA WA TAIFA!

Ni Usalama wa CCM, wameapa kulinda maslahi yao,maana kama badiliko la serikali litakuja ,wamekwisha.

Kuna aina mbili,wale rank and file ni njaa tu,wengi tunakunywa nao vikaoni

Kuna elites, kama wakuu wa wilaya/mikoa ambao wanapata nyingi toka serikalini. Wengine elites wala weny misafara ya Mawaziri, Rais, wanaokwend

Ulaya kila siku.
 
Musembi nimejitahidi sana kusoma lakini sidhani kama nimekuelewa sawasawa unaweza kutuambia kwa summary lengo la thread hii ni nini

Je wewe ni mmoja wa UWT uliyechoshwa na uongozi humo ndani au wewe ni raia unayelalamika utendaji wa UWT.
 
Musembi nimejitahidi sana kusoma lakini sidhani kama nimekuelewa sawasawa unaweza kutuambia kwa summary lengo la thread hii ni nini
Je wewe ni mmoja wa uwt uliyechoshwa na uongozi humo ndani au wewe ni raia unayelalamika utendaji wa uwt.

Mkuu. Kwa kifupi ni kuwa lengo langu ni kueleweka au kutoeleweka. Sitegemei kueleweka na kila mtu, so kitendo cha wewe kutonielewa nakichukua kama changamoto na much thanks kwa kuwa specific, maybe in thext articles nitajaribu ku-play in your box, ila kwa sasa jaribu kufikiri nje ya box na ikibidi jivalishe uhusika tofauti tofauti.
 
MABADILIKO YAJA TANZANIA ZAIDI YA TSUNAMI: VIJANA WALALAHOI TUKAE MKA KULA!!!!!!!!!

Msione Rais Kikwete anavyozunguka ovyo duniani; mambo si shwari tangu ndani ya familia yake, si shwari ikulu, nasema na wenye akili wanajua kwamba mambo si shwari kwenye kikundi cha wanamtandao, serikalini wala kimataifa.

In a nutshell, president Kikwete is by this minute far more than just a MAN UNDER SIEGE under the cobweb of political miscaculations and over-merchinisation.

The centre can no longer hold anymore, things are imminent of falling apart to the very core of his own family government; and that slightly explains Mama Salma's eloquent hybernation from public view with her supposed better half in life.

Na kwa upande wa suala zima la TAASISI ZA SERIKALI NA UENDESHAJI wake; kote huko ni mrundikano wa mashemeji mtindo mmoja, washikaji hivyo utendaji wa tija pengine tuutegemee kwa 2020 huko na wala si leo hii!!!!

Hakika vyombo vya Usalama wa Viongozi wa CCM, Taasisi ya Kuboresha na Kushamirisha Rushwa Nchini pamoja na Tume ya Taifa ya Uchakachuaji Uchaguzi vyote kwa pamoja vikome kutumia jina letu kama Tanzania na viache pia kutumia kodi zetu maana havina TIJA tena kwetu.

Nasema vyombo hivi ni kero kubwa kuliko hata jinsi Rais Kikwete alivyo mzigo wa misumari ya moto mabegani mwetu. Hebu tuacheni tujue kimoja kwamba hatuna Taasisi za Kiserikali zenye kuweza kufanya kazi KWA MASLAHI YA TAIFA (Sisi wananchi).

Kitendo cha Rais Kikwete kupenyeza
WANAMTANDAO (Mdudu aliyoiumba yeye na sasa kumshinda kuidhibiti na sumu zake) dhana ya TAASISI haipo tena Tanzania bali ni kwamba kumebakia tu masimulizi za enzi za Mwalimu Nyerere ambapo TAASISI kweli zilikua zikifanya kazi kwa weledi zaidi na kuheshimika na wananchi walio wengi.

Mabadiliko yaja Tanzania kwa Mtindo ambao ni zaidi ya Tsunami na wachafu wote kusahaulika hivi karibuni.

Hatuna USALAMA WA TAIFA!
Ni Usalama wa CCM ,wameapa kulinda maslahi yao,maana kama badiliko la serikali litakuja ,wamekwisha.

Kuna aina mbili,wale rank and file ni njaa tu,wengi tunakunywa nao vikaoni

Kuna elites,kama wakuu wa wilaya/mikoa ambao wanapata nyingi toka serikalini.Wengine elites wala weny misafara ya Mawaziri,Rais ,wanaokwend
Ulaya kila siku.
 
Wakati nchi ikiendelea kuelea katika mawimbi na Kimbunga cha misukosuko ya kiuchumi, kimaadili, usalama, na kitaaluma, watu tumekujikuta tukiwa katika hamaki kubwa, hatua mbali mbali zimechukuliwa ili kukabiliana na mambo yatokanayo, matokeo yake hatua hizo zimekuwa zikitutumbukiza katika katika matatizo na mifarakano zaidi ya kijamii na kutuacha tukiwa tumegawanyika, na kuona dalili zote za mass mass hysteria at anytime.

Idara ya usalama wa taifa (National Intelligence) ilikuwa ndiyo chombo ambacho tulitegemea kijenge ukuta kati yetu watanzania na hali niliyoitaja au hata itoe red alert kwa policy makers kuhusiano na mabadiliko na mwelekeo tunaoulekea, lakini hali imekuwa ni kinyume cha hapo, idara hiyo imekuwa ikitumika dhidi ya raia wakati mambo yanayowahusu yakizidi kuharibika na kuonekana kama wahusika hawajui na kutambui wajibu wao halisi kwa taifa.

Hali sasa imekuwa mbaya zaidi kwani imeonekana kana kwamba baadhi ya watumishi wa idara hii kutaka na wao kujiinua na kujiweka juu ya sheria kwa kujaribu kutumia nafasi zao kukabiliana na raia kwa kuwatisha na kujaribu kulazimisha mazingira ya kutaka kutambulika wao ni nani and what are they capable of, japo kumekuwa na jitihada za kuisafisha na kuhakikisha idara hii inatimiza majukumu yake ipaswavyo, bado kumekuwepo na watumishi wachache wa idara hii kwa kuongozwa na hulka za kupenda ku-show their real Identity na kuzi-misuse in public kwa ajili ya tabia na matokeo ya ki-binafsi.

Kama taifa, tuna matatizo mengi yanayohitaji ufumbuzi, na mengi yameingia au kuingizwa nchini ikiwa ni matokeo ya idara ya usalama wa taifa kukosa umakini, najua na wengi wetu tunatambua kuwa ni kweli kuna ugumu ambao idara hii huwa inakumbana nao katika utendaji wake, ugumu ambao husababishwa na watunga sera, hata Martin Petersen ambaye ni retired senior CIA Directorate of Intelligence (DI) officer aliwahi ungelea katika moja ya maandiko yake (articles). Kwa maandiko yake Peterson alipata kulalamika kuwa "It is not surprising then that Policymakers do not always see how we can help them" akaendelea kulalamika kuwa unaweza kumfuata policy makers kwa lengo la wewe kuufanya wajibu wako wa kumshauri na kumsaidia namna ya kuliangalia jambo, lakini ataishia kukudharau na kukujibu kuwa:

After all, I, the policymaker, am smart and have excellent sources of information (including all the ones you have), and I am very busy, so why should I spend some of my most precious commodity on you?

Hapa najaribu kuonyesha kuwa kuna baadhi ya vikwazo ambavyo idara yetu ya usalama wa taifa imekuwa ikikumbana navyo katika kufanya majukumu yao yapo very global, Uingereza yapo, Marekani yapo, Italy yapo, Russia yapo, na sehemu nyingine nyingi yapo, hivyo wasisuse kwa kuwa mazingira yanawabana kutimiza wajibu wao, bali wana wajibu wa kujifunza na kutengeneza mbinu ya namna ya kukabiliana na changamoto hizo.

Nimemkariri Peterson ili kukiri na kukubali kutambua vikwazo vilivyopo.

Naendelea na upande lengwa uonyeshao namna ambavyo kushindwa huko wakati mwingine na mwingi hausababishwi na Policy makers bali wao wenyewe, na zaidi kwa ulevi wa sifa zitokanazo na kubahatika kuingia katika idara hiyo nyeti na kichwa cha jamii. Mtanisamehe wasomaji sitapiga moja kwa moja bali huu nitaufanya kama mwanzo katika kuelekea kufumua uozo unaofanywa na watumishi wachache wa idara hii wasio waaminifu, nikiwa na mifano halisi na mmoja ukiwa umenitokea binafsi na jamaa mmoja kutoka idara hii nyeti ambaye anafanyia katika NGO moja, naangalia namna ya kushughulika naye ila nimeamua kuufanya huu kama mwanzo.

Pia Nimeandika hapa ili wajiangalie na kujaribu kurekebisha mwenendo wao, na washiriki ktika kulinasua taifa kutoka katika mwelekeo wa kusambaratika. Ujinga wa kudhani wanafahamu kila kitu ndiyo udhaifu unaowafanya wabaki watazamaji katika mambo yanayo wapasa kuyatimiza au kuyagundua yakiwa tayari kwenye vyombo vya habari sawia na sisi raia wengine.

Hivyo wasidhani kuwa wana kazi ngumu ili hali wanaishi maishi mazuri maishi yatokanayo na uwepo wetu sisi kama taifa, kwani waelewe kuwa si na sisi tayari tuna jukumu kubwa na gumu la kuishi katika umaskini na unyonge huu tulio nao. Pia hawakuingia katika idara hiyo ili kutaafuta unafuu wa maisha bali kuitumikia jamii iliyopana na yenye migongano ya kimawazo na wakati mwingine vigeugeu, na zaidi waongeze katika uelewa wao kuwa wao kama ilivyo kwa wanajeshi na polisi si wafanyakazi. Na zaidi wanajukumu la kuto exist.

Watu wa namna hi kama tutaamua kuwaita wajinga na malimbukeni basi tutakuwa tunawakosea nidhamu wajinga na malimbukeni halisi.

Ni afadhali kama una personal issue zishughulikie kwa uwezo wake kama raia mwingine ili kulinda your true Identity na si kutengeneza mazingira ya kutaka watu wakufahamu wewe ni nani, mulewe kuwa jamii ni pana kuliko uwezo wenu wa kufikri unapoishia and you may think that you are snoping us, but be reminded that we are watching you as run in the circles like headless chicken. We are capable in so many and in so less things, but we wont let you know, we will keep on living our life and do the living as we supposed to do.

Tangu kuanzishwa kwake idara hii ya usalama wa taifa ilitegemewa iwe ndiyo an eye and if possible think-tank ya taifa lakini wameacha au hawajui majukumu yao, na sisi tukiwa kama raia tunaoheshimu uhuru wetu, wajibu na mipaka msidhani tunatishika tena na upupu na upumbavu wa baadhi ya watumishi hao wasiojua miiko ya kazi yao, tuna uwezo wa kujilinda na hata kulinda wenzetu iwe kwa mapambano au diplomasi au kisheria, tumeamua kujitwisha jukumu la kufikiri na kujilinda badala ya wao kufanya kazi hiyo kutokana na mapungufu wanayoyaonyesha katika utendaji.

Inawezekana vipi mtu ambaye alichunguzwa na kufuatilia hatua kwa hatua kwa muda wa miaka miwili kabla hajawa enrolled kwenye intake, anarudi uraina akiwa ame qualify mafunzo na kuishia kufanya madudu ya kiwango tukionacho? Unadhani tutabaki tena kuwa na imani ile ile na watu wa idara ya aina hii? Mnaweza mkatupa sababu nzuri ya kwanini tusiingilie kazi zenu na kuzifanya sisi kwa maslahi ya taifa letu na la ya vizazi vijavyo?

Mbegu ili iote na kustawi ni lazima ife sawa nadhani matumizi mabovu ya falsafa hii ndiyo yameharakisha baadhi yenu mlifikishe taifa letu hapa lilipo japo kulikuwa hakuna ulazima wa kuliua.

Ninamaliza kwa kusema sasa itakuwa ni hatua kwa hatua and many more to come...... Si lazima tuwafahamu ninyi bali kuna umuhimu wa ninyi kuufahamu wajibu wenu.
 
Hivi hii idara ipo Tanganyika?! Taifa hili limeharibiwa kiasi hiki, bado hii idara inajiita ipo! Huu si ni uleule usanii wa kuwa bado tuna jeshi la anga?! Najua wapo watakaotetea kuwa kuna taarifa nyeti tunazipata kwa kuvujishwa na wazalendo wachache walio huko, lkn hizo hazitoshi kuhalalisha kuwa idara hii ipo.... Nakataa. Kama ipo tusingekuwa na rais wa ajabu kama huyu, rostam na genge lake wasingeila nchi hii kiasi hiki. Kama wangekuwemo wazalendo wa kutosha kama hawasikilizwi na hao watunga sera, wangekuwa wanaondoa baadhi ya ' vikwazo' wenyewe! Ujuzi na uwezo huo wanao.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom