Jaslaws
JF-Expert Member
- May 31, 2011
- 6,016
- 5,300
Hawa jamaa sijui wana matatizo gani..juzi kati walikua na kipindi/shindano la kumtafuta mtu mwenye wazo la kibiashara na mshindi angepewa milioni kumi,wafadhili walikua ni Nssf,shindano lilijulikana "kama ndoto za kitaa''jamaa mmoja anakaa maeneo ya pugu ndo aliyeshinda,wazo lake ilikua ni kurenew mifuko iliyotumika,sasa hawa clouds kwa uroho wa hela wanataka kumdhurumu pesa yake,wanamlazimisha afungue akaunti kwenye benki wanayoitaka wao,kisa ndo benki inayowapa mikopo,pia wanamlazimisha awape milioni tatu kwa maelezo kua wao ndo walio mfanya ashinde hiyo pesa kitu ambacho sio makubaliano yao,....clouds mpeni kijana pesa zake zot,acheni kuwanyonya vijana kwa sababu ya umasikini wao,mnawanyonya kwenye mziki naona hamjaridhika mmehamia na uku sasa..