Hatua saba muhimu za uponyaji wa CHADEMA!

LENGEJU BOB kama wapenda mabadiliko wote tungekuwa kama wewe basi mgogoro huu ungeonekana mdogo sana. Binafsi nimefurahishwa sana na makala hii. ni matumaini yangu kuwa wahusika watahusoma na kuhufanyia kazi.
 
Last edited by a moderator:
Asante ndugu mpenda mabadiliko.... Naamini hakuna lisilowezekana chini ya jua... ni suala la kuvua ubinafsi na kuvaa uzalendo tu! na Pengine hiki ni kipimo kwa wapenda nchi wote... Tukiamua kufuata msemo wa mwaga mbona namwaga ugali ni sawa! na matokeo yake tutayaona....na tukiamua kuweka mbele maslahi mapana, tunaweza kuokoa jaazi na kuipaisha demokrasia ya Tanzania!
 
Slaa katoa amri swala hili lisijadiliwe, lakini Godbless Lema na viongozi wengine wamepuuzia amri hiyo ya Slaa...
 
Umenigusa, umenitia Moyo...Asante

Lengeju, kakudanganya demokrasia yaendana na uchumi hivyo uchumi kwanza then demokrasia. Mi ni CCM nina biashara zangu ambzazo zinasahmiri na kumea kwa uwepo wa CCm nina influence kubwa kwa sababu baba yangu ni mjumbe mkuu CCM, halafu wewe unaleta usatwi wa demokrasi wapi bwana.
 
Watu wengine akili zao ziko kwenye kucha, Sasa wakishakata kucha ndo huibuka na nyuzi Kama hizi.
Yaani kurudisha wasaliti kwenye injini ya chama ndo kunusuru chama?
Tunasubiri kwanza, kucha zako ziote ili utupe ushauri wako.
 
Mtoa mada, wewe ni mwanasheria/unasomea sheria, bila shaka ungeweka input ya kisheria katika mada yako ungemake sense zaidi. TUELEZE BWANA LENGAJU, NI KWA VIPI NA NI KWA NAMNA GANI UNAWEZA KUMUWEKA HATIANI ZITTO KABWE KUHUSIKA NA ULE WARAKA?. KWA USHAHIDI UPI?.

Usiogope kusimamia haki ili kuappease kundi fulani, Unaweza vipi kuisifu kamati kuu kufanya maamuzi ya Kijinga, bila hata wewe kujiridhisha ni Ushahidi gani unamuweka katika makosa Zitto?.
 
Nawashukuru wote mlichangia...nawakaribisha wengine wenye mawazo. Suala la Demokrasia ni suala la ustawi wa nchi. Tushirikiane kujenga Nchi yetu! Nawapenda sana....Tuipende Nchi yetu!
 
Hillarious indeed....!

Yaani Mbowe anyimwe haki yake ya kikanuni,kikatiba na kidemokrasia kwa sababu ameongoza kikao kilichowaadhibu wasaliti?

Yes,CHADEMA ina watu wengi.Wapo akina Lissu na wengine wenye misimamo isiyotiliwa shaka lakini haiwezi kuwa hoja ya kumnyima Mbowe nafasi ya kugombea

1461376_638256166215624_726567862_n.jpg
 
Vita yoyote duniani huwa inakuwa na mshindi hata kama ni baada ya miongo kadhaa. Ila kwa dunia ya sasa wenye busara hujitahidi kuzuia vita isitokee au kukolea pale inapokuwa imeanza kutokea. Kuna msamiati unaitwa MEZA YA MAZUNGUMZO siku hizi ndio ambao ulimfanya Kikwete akatukanwa sana na Kagame.

Katika siasa pia vita za kisiasa ndani ya vyama na zenyewe washindi hupatika. NCCR walipatikana, UDP walipatikana, CUF walipatikana na hata CHADEMA watapatikana. Swali ni je vita hii itakiacha Chama na nguvu ile ile?

Katika nchi vita husababisha wakimbizi, uchumi kuporomoka, majengo kuharibiwa, vifo n.k. Historia inaonyesha palipotokea vita katika vyama Chama kilikufa na kupoteza nguvu na mvuto wake.

Naona Chama kikiwa hatarini hasa kipindi hiki tunapoendelea na uchaguzi wa ndani. Maana kunaweza kutokea kundi la wanaoshindwa kwenye uchaguzi na wanaoshinda.

NAAMINI KATIKA MAZUNGUMZO NA SIO MSHINDI WA VITA ATAKUWA NANI.
 
Mwenye kehima kuokoa maisha, lakini mbabe hujichimbia kaburi lake mwenyewe! Negotiation and compromise is a sign of strength, wisdom and vision.
 
Vita yoyote duniani huwa inakuwa na mshindi hata kama ni baada ya miongo kadhaa. Ila kwa dunia ya sasa wenye busara hujitahidi kuzuia vita isitokee au kukolea pale inapokuwa imeanza kutokea. Kuna msamiati unaitwa MEZA YA MAZUNGUMZO siku hizi ndio ambao ulimfanya Kikwete akatukanwa sana na Kagame.

Katika siasa pia vita za kisiasa ndani ya vyama na zenyewe washindi hupatika. NCCR walipatikana, UDP walipatikana, CUF walipatikana na hata CHADEMA watapatikana. Swali ni je vita hii itakiacha Chama na nguvu ile ile?

Katika nchi vita husababisha wakimbizi, uchumi kuporomoka, majengo kuharibiwa, vifo n.k. Historia inaonyesha palipotokea vita katika vyama Chama kilikufa na kupoteza nguvu na mvuto wake.

Naona Chama kikiwa hatarini hasa kipindi hiki tunapoendelea na uchaguzi wa ndani. Maana kunaweza kutokea kundi la wanaoshindwa kwenye uchaguzi na wanaoshinda.

NAAMINI KATIKA MAZUNGUMZO NA SIO MSHINDI WA VITA ATAKUWA NANI.

Ndani ya CHADEMA hakuna vita isipokua maamuzi ya kinidhamu.Kama ni vita basi ni kati ya Kanuni,sheria na katiba Vs Watovu wa nidhamu na wahaini waliokiri kosa

Kwa hiyo CHADEMA kuna mchakato wa maamuzi ya kinidhamu na utekelezaji wa maazimio ya kamati kuu juu ya hatua za kinidhamu kuhakikisha chama kinakua kisafi na misingi yake inaheshimiwa tofauti na hivyo vyama vingine

Hakuna Mjadala na watovu wa nidhamu.Hata mimi binafsi nilishawahi kuadhibiwa na hakujawahi kuwa na majadiliano katika kulinda misingi ya uanzishwaji wa chama


Nampongeza Mwanasheria Mkuu wa Chama Tundu Lissu kwa kusimama kidete katika hili.Namuunga Mkono kwa 100%.Hakuna mjadala na wahaini wanaoharibu umoja na mshikamano zaidi ya kuchora mstari mwekundu wa moto
 
unamaanisha kwamba mtu mmoja au hata 50 kama inavyosemekana wako vitani na chama chao , au tuseme wanaipiga cdm ?
 
Mimi pia nimeguswa sana na kinachoendelea CDM, kusema ukweli kufa kwa chadema hata mwana CCM makini hawezi kufurahia.
CDM ni chama cha watanzania ,niliwahi kufanya kazi na watu kutoka USA, hata kama mtu ni Republican/Democrats hawezi kuota wala kuwaza eti chama kimojawapo kife kwa maanufaa ya chama chake,mmoja alinitolea mfano wa kutupa T shirt kwa sababu umepata shart,kwa maana yeye anaamini kila nguo itafaa kwa wakati na majira furani.
Nimefarijika sana na makala yako bwana Lengeju,ni makala iliyojaa kila chembe ya Utanzania na upeo wa kuionea huruma hii nchi,maana anaye ionea huruma nchi hii ni sharti awe na maono ya kukomaza Demokrasia.

Ni kweli usio pingia kuwa binadamu tumeumbwa kwa kutofautia mmoja na mwingine,ili maisha yaende ni sharti tukabali usemi usemaosema (give and take).

Haiwezekani tukubaliane kwa kila jambo,na ukikuta watu wanakubaliana kila jambo,fuatilia huenda watakuwa na matatizo ya kufikiri,nadiriki kusema huenda ni majuha.Maana haiwezekani watu wote watano mfano mukubaliane kwa kila kitu,haiwezekani,ila watu wenye busara hukubali pia mawazo pinzani/kinzani na wao.

Mfano mimi ni Dr wa magojwa ya binadamu,nawaza namna gani mgonjwa anaye umwa ugonjwa fulani nitamtibuje,mwingine ni engineer anawaza hivi atapitisha umeme kwenye maji ufike Zanzibar. Laiti hawa wote wangewaza kitu kimoja hakika maisha yangekuwa majanga,dunia ingekuwa sehemu mbaya kabisa kuishi,lakini kwa kuwa binadamu tunatofautiana kuna vitu anuwai vinaendelea kwa wakati mmoja.

Hivyo mimi ni muumini mkuu wa kuamini kila fikira/wazo au mtizamo furahi unahiji kuangaliwa kwa umakini mkubwa pengine unaweza kuwa ndo mwanzo wa kitu kimoja bora kabisa,ili mradi umepewa nafasi ,umepata tafakuri ya kina na kuja na ufafanuzi wenye kuonesha mlengo hasi na chana na watu ambao hawana mlengo fulani ili kutendea haki wazo/mtizamo fulani.Ikidhihirika kuwa si bora kwa wakati wowote au kwa wakati huu au wakati fulani,pia mwenye wazo akubali au aende ajipange upya kwa maana ya kuboresha zaidi,au atafute namna nyingine ya kuwasirsha mawazo yake apate kueleweka maana pingine hakueleweka vizuri,ila asitumie nguvu au jadhiba kuladhimisha anachoamini.

Mh ZZK na wenzie pamoja na Viongozi wa chadema walioko madarakani hasa Mwenyekiti wetu mpendwa Freemani Mbowe kama kweli wanapenda maendeleao na uhai wa demokrasia changa ya nchi yetu ,niwaombe tu wasome makala ya huyu bwana hasa hatua ya kwanza,ya sita na ya saba.

Kijana amejitahidi sana kuchambua bila kuegemea upande wowote,binafsi nakubaliana naye mia kwa mia.Tofauti zetu sizizime doto ya vijana wa kitanzania.

Pia naomba niwaonye wana chama wa chama pinzani na CDM kama kweli wako nyuma ya mipango hii ovu,hawako salama maana dhambi hii ni kubwa kuliko ufisadi,hela zinatafutwa ila demokrasia hainunuliwi kwa pesa wala thamani yake haipo.

Litakuwa jambo la ajabu sana eti mtu kuwa CCM anafanya mipango ya kuua chama kingine tena kwa kodi zetu,ni dhambi ambayo huwezi kutubu ukapata msamaha.

Kwa hili naomba Rais Kikwete aingilie kati,pamoja na mambo mengi anayozushiwa Mkuu wa nchi yetu sijaona akiwa msitari wa mbele kuhanisi demokrasia ya nchi yetu.
Naamini anayo nia thabiti ya kuona emokrasia ya nchi yetu inakua kuliko wakati wowote wa uhai wa Taifa hili changa,hivyo sidhani wala siamini kama anaweza kuruhusu hela za kodi zitumike kunajisi demokrasi kiasi hiki.

Mungu ibariki Afrika,Mungu ibariki Tanzania

Bro u truely great great thnker
 
Back
Top Bottom