Hatimaye Zitto Kabwe akaa meza moja na UKAWA

Hatimaye Zitto Kabwe akaa meza moja na UKAWA

Zitto kweli anahitaji pongezi japo watu kama kina Mnyika na Lissu wanateseka sana kwa ujio wake ukawa
Mwenzio keshaona ACT imeelekea kibla iliyobaki anatafuta hoja za kumrudisha kwenye meli ya Ukawa.
 
Walichokifanya UKAWA dhidi ya hoja ya Zitto ni "Gentlemen Reaction" nawapongeza sana Ukawa.
Gentleman anafanya maauzi kwa kuunga mkono hoja yenye ukweli hatakama inaletwa na mtu asiyetoka kwenye kundi lake,
Gentleman ataunga mkono hoja ya ukweli hata kama mleta hoja aliwahi kwenda kinyume na hoja yako ya ukweli kabisa hapo awali.


Zitto aliwahi kwenda kinyume na msimamo wa UKAWA bungeni na kubaki bungeni tena msimamo wenye hoja ya kweli na nzito, ila hiyo sio sababu ya UKAWA kwenda kinyume na hoja ya kweli iliyoletwa na Zitto simply kwakuwa eti aliwahi kwenda kinyume na hoja za UKAWA mara kadhaa, huu ndiyo unaitwa uungwana.
 
ImageUploadedByJamiiForums1453994712.412455.jpg

Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe (kulia) akipeana mkono na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe.
Siku zote kiburi cha Serekali ya Ccm huwa kinakuwa faida kwa upinzani tanzania.
Mtakubumbuka kiburi cha Ccm kwenye bunge la katiba,kilizaa Ukawa kwa mara ya kwanza Cuf na CDM wakajoin pamoja.
Hilo limejitokeza tena jana.Mwondelezo wa kibri umefuta tofauti kati ya ACT na CDM
Leo nani alitaraji zitto atakula sahani moja na Lema?
Leo zitto yupo pamoja tena na mlezi wake wa kisiasa Freeman
Kiburi kimezaa jeuri
 
ImageUploadedByJamiiForums1453995214.718029.jpg


Zitto Zuberi Kabwe amenguruma katikati ya msitu Uliojaa UKAWA

Japokuwa yupo peke yake ambayeahana kundibingeni ila machachari yake yameonekana siku ya kwanza tu toka bunge la 11 kuanza .

Kuna wengine wanajiita simba hadi wanang'ang'ania jina mitandaoni ila ukiuliza walichofanya hamna zaidi ya kubadilisha wanawake hapa mjini na kukata viuno majukwaani.

Zitto hakika wewe ni Simba
 
Kama ccm walliweza kumuamini slaa mpaka kumpa ulinzi wa USALAMA WA TAIFA na kumlipia hotel ya nyota tano na c malipo kwenye luninga, unashangaa zito kupatana na UKAWA? Slaa aliitwa msaliti pia na ccm lakini leo ni shujaa ndani ya ccm.
 
Napenda sana kuona kuna watu wapo upande wetu kututetea dhidi ya serikali kandamizi. Hakuna kitu kinaniuma kama bei za umeme
 
Wamalize tofauti ili kuliokoa taifa mana ndo njia pekee ya kumuondoa mkoloniccm ili kupata siasa safi
 
Ni aibu kwa kina fulani waliotaka kuona hawa watu wakichapana makonde, huu ndio upinzani hata mwenzako akilikoroga mpe alinywe ili ajirekebishe, maisha yanaendelea.
 
Walichokifanya UKAWA dhidi ya hoja ya Zitto ni "Gentlemen Reaction" nawapongeza sana Ukawa.
Gentleman anafanya maauzi kwa kuunga mkono hoja yenye ukweli hatakama inaletwa na mtu asiyetoka kwenye kundi lake,
Gentleman ataunga mkono hoja ya ukweli hata kama mleta hoja aliwahi kwenda kinyume na hoja yako ya ukweli kabisa hapo awali.


Zitto aliwahi kwenda kinyume na msimamo wa UKAWA bungeni na kubaki bungeni tena msimamo wenye hoja ya kweli na nzito, ila hiyo sio sababu ya UKAWA kwenda kinyume na hoja ya kweli iliyoletwa na Zitto simply kwakuwa eti aliwahi kwenda kinyume na hoja za UKAWA mara kadhaa, huu ndiyo unaitwa uungwana.
Umeongea point wakumbushe zito alisema kutoka bungeni sio ukomavu wa kisiasa naona nae ametoka ili kuunga nguvu ya haki sasa nani anae muitaji mwenzie zaid kwa hilo mi nimeona zito sasa ameamua kufanya busara za kizalendo kabs kubaki alikosea mwanzo
 
Lackeys mnatabu sana,mkiona bwana yenu kamchukia mtu na nyinyi mnalazimika kumchukia hata kama hamjui hata chanzo cha ugomvi wao ili mumridhishe tu bwana yenu na ikitokea wamepatana mnaanza tena kujishebedua.

Hawa jamaa uwezekano wa ku-settle tofauti zao ni mkubwa sababu issue ilikuwa uenyekiti tu na lengo la kumpoteza kisiasa limeshindikana so running dogs jiandaeni tena kuanza kumuimbia mapambio.
 
Back
Top Bottom