Hatimaye Wema akubali posa ya rubani

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,268
1577053270860.jpeg

1577635441552.jpeg

KIMEELEWEKA! Baada ya kuruka viunzi vya hapa na pale, hatimaye, mrembo kutoka Bongo Movies, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ ameridhia kupokea posa ya rubani wa ndege, Hamdan Zakwani ‘Danzak’, Gazeti la IJUMAA linakupa habari kamili.

Mapema mwaka huu, rubani huyo ambaye pia anafanya muziki wa Bongo Fleva, alijitokeza hadharani na kutangaza azma yake hiyo, lakini akakutana na kizingiti kutoka kwa Wema.

TUJIUNGE NA CHANZO

Chanzo kilicho karibu na Wema kimelitonya IJUMAA kuwa, mrembo huyo aliweka ngumu awali, lakini baada ya kutafakari kwa makini, ameona rubani huyo anafaa.

“Awali, Wema kweli alikataa, lakini kadiri muda ulivyozidi kwenda alimtafakari na kuona ni mtu mzuri,” kilisema chanzo hicho.

CHANZO CHAZIDI KUTIRIRIKA

Chanzo hicho kilichoomba hifadhi ya jina kilizidi kueleza kuwa, sababu hasa za kumkubalia ni baada ya kumruhusu kuwa karibu na kuona ni mtu mzuri anayemfaa.

“Unajua alichokifanya Wema ili kumjua tabia ni kumuweka karibu. Kama umefuatilia, siku za hivi karibuni Wema amekuwa karibu sana na Danzak. Kama unakumbuka juzikati walikuwa wote Arusha na Wema. Hapo ndipo alipomjua kiundani na kuona ni mwanaume mwenye sifa anazozitaka na akamruhusu alete mahari,” kilisema chanzo hicho na kuongeza;

“Alichokuwa amekifanya awali Wema ni kumkataa mwanaume huyo bila hata kumjua vizuri. Aliangalia tu kwa juujuu na kuona hamfai, sasa alipokaa naye akaona wanaendana.”

DANZAK ATHIBITISHA

Kufuatia taarifa hizo, Gazeti la IJUMAA lilimtafuta Danzak ambapo alipopatikana alithibitisha kuwa amekubaliwa kupeleka posa na amejipanga kwa ajili ya jambo hilo.

ALISARANDIA VYA KUTOSHA

Alisema anaona sasa ni muda muafaka kwa kuwa ni muda mrefu alikuwa akipigwa chenga na Wema kila alipotaka kwenda kutoa mahari.

“Nilikuwa nikirushwa sana kwenye kutoa barua na hata mahari maana alikuwa kama hajanielewa kabisa, lakini sasa ninamshukuru Mungu nimekubaliwa na ninaamini mambo yataenda vizuri na mwisho wa siku watu waliokuwa hawapendi kuona jambo hili watabaki midomo wazi maana kwa kweli nimehangaika nalo kwa muda mrefu sasa,” alisema Danzak.

WEMA ANASEMAJE?

Baada ya kuzungumza na Danzak, Gazeti la IJUMAA lilimsaka Wema na kumuuliza kuhusu suala ambapo alisema yeye hana kipingamizi kwani jambo la heri linaenda na heri na kama imepangwa hawezi kupangua, anasubiria kwa hamu.

“Unajua siku zote jambo la heri linaenda na heri hivyo basi kama ikifika hiyo siku mimi nitashukuru na itakuwa wakati wangu umefika sina zaidi la kusema kikubwa ni kuomba hiyo siku ifike na hilo jambo litimie,” alisema Wema.

TUJIKUMBUSHE

Januari mwaka huu, Danzak ambaye alifika nchini akitokea Uarabuni anakofanyia kazi na kutangaza kuwa anataka kumuoa Wema.

Pamoja na hilo, alisema dhumuni la ujio wake Bongo ni pamoja na kuachia nyimbo zake mbili; Fall In na Kichaa.

WAONEKANA HOTELINI

Wakati watu wakiwa wanasubiri majibu ya Wema kuhusu rubani huyo, gazeti ndugu la hili la Amani, lilimnasa akiwa anaingia kwenye hoteli moja maarufu jijini Dar.

Hata hivyo, baadaye Wema aliibuka kwenye Gazeti la Ijumaa Wikienda na kuikataa posa ya rubani huyo kwa kile alichodai kuwa hataki kuolewa na msanii wa Bongo Fleva.

Kwa kauli yake ya sasa na urafiki walionao wawili hao ni dhahiri kwamba kweli ametengua kauli yake na sasa kinachosubiriwa ni posa, mahari na hatimaye ndoa!

KUHUSU DANZAK!

Danzak ni Mtanzania ambaye kabla ya kwenda masomoni nje ya nchi na kuhitimu urubani kisha kuanza kazi, amewahi kufanya kazi za muziki katika Kundi la TNG Squard la jijini Tanga lililokuwa likiundwa na wasanii Agustino John ‘Latino Man’ na Malick Bandawe. Kwa sasa anafanya muziki na pia anaendelea na kazi yake ya urubani.
 
View attachment 1300750

KIMEELEWEKA! Baada ya kuruka viunzi vya hapa na pale, hatimaye, mrembo kutoka Bongo Movies, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ ameridhia kupokea posa ya rubani wa ndege, Hamdan Zakwani ‘Danzak’, Gazeti la IJUMAA linakupa habari kamili.

Mapema mwaka huu, rubani huyo ambaye pia anafanya muziki wa Bongo Fleva, alijitokeza hadharani na kutangaza azma yake hiyo, lakini akakutana na kizingiti kutoka kwa Wema.

TUJIUNGE NA CHANZO

Chanzo kilicho karibu na Wema kimelitonya IJUMAA kuwa, mrembo huyo aliweka ngumu awali, lakini baada ya kutafakari kwa makini, ameona rubani huyo anafaa.

“Awali, Wema kweli alikataa, lakini kadiri muda ulivyozidi kwenda alimtafakari na kuona ni mtu mzuri,” kilisema chanzo hicho.

CHANZO CHAZIDI KUTIRIRIKA

Chanzo hicho kilichoomba hifadhi ya jina kilizidi kueleza kuwa, sababu hasa za kumkubalia ni baada ya kumruhusu kuwa karibu na kuona ni mtu mzuri anayemfaa.

“Unajua alichokifanya Wema ili kumjua tabia ni kumuweka karibu. Kama umefuatilia, siku za hivi karibuni Wema amekuwa karibu sana na Danzak. Kama unakumbuka juzikati walikuwa wote Arusha na Wema. Hapo ndipo alipomjua kiundani na kuona ni mwanaume mwenye sifa anazozitaka na akamruhusu alete mahari,” kilisema chanzo hicho na kuongeza;

“Alichokuwa amekifanya awali Wema ni kumkataa mwanaume huyo bila hata kumjua vizuri. Aliangalia tu kwa juujuu na kuona hamfai, sasa alipokaa naye akaona wanaendana.”

DANZAK ATHIBITISHA

Kufuatia taarifa hizo, Gazeti la IJUMAA lilimtafuta Danzak ambapo alipopatikana alithibitisha kuwa amekubaliwa kupeleka posa na amejipanga kwa ajili ya jambo hilo.

ALISARANDIA VYA KUTOSHA

Alisema anaona sasa ni muda muafaka kwa kuwa ni muda mrefu alikuwa akipigwa chenga na Wema kila alipotaka kwenda kutoa mahari.

“Nilikuwa nikirushwa sana kwenye kutoa barua na hata mahari maana alikuwa kama hajanielewa kabisa, lakini sasa ninamshukuru Mungu nimekubaliwa na ninaamini mambo yataenda vizuri na mwisho wa siku watu waliokuwa hawapendi kuona jambo hili watabaki midomo wazi maana kwa kweli nimehangaika nalo kwa muda mrefu sasa,” alisema Danzak.

WEMA ANASEMAJE?

Baada ya kuzungumza na Danzak, Gazeti la IJUMAA lilimsaka Wema na kumuuliza kuhusu suala ambapo alisema yeye hana kipingamizi kwani jambo la heri linaenda na heri na kama imepangwa hawezi kupangua, anasubiria kwa hamu.

“Unajua siku zote jambo la heri linaenda na heri hivyo basi kama ikifika hiyo siku mimi nitashukuru na itakuwa wakati wangu umefika sina zaidi la kusema kikubwa ni kuomba hiyo siku ifike na hilo jambo litimie,” alisema Wema.

TUJIKUMBUSHE

Januari mwaka huu, Danzak ambaye alifika nchini akitokea Uarabuni anakofanyia kazi na kutangaza kuwa anataka kumuoa Wema.

Pamoja na hilo, alisema dhumuni la ujio wake Bongo ni pamoja na kuachia nyimbo zake mbili; Fall In na Kichaa.

WAONEKANA HOTELINI

Wakati watu wakiwa wanasubiri majibu ya Wema kuhusu rubani huyo, gazeti ndugu la hili la Amani, lilimnasa akiwa anaingia kwenye hoteli moja maarufu jijini Dar.

Hata hivyo, baadaye Wema aliibuka kwenye Gazeti la Ijumaa Wikienda na kuikataa posa ya rubani huyo kwa kile alichodai kuwa hataki kuolewa na msanii wa Bongo Fleva.

Kwa kauli yake ya sasa na urafiki walionao wawili hao ni dhahiri kwamba kweli ametengua kauli yake na sasa kinachosubiriwa ni posa, mahari na hatimaye ndoa!

KUHUSU DANZAK!

Danzak ni Mtanzania ambaye kabla ya kwenda masomoni nje ya nchi na kuhitimu urubani kisha kuanza kazi, amewahi kufanya kazi za muziki katika Kundi la TNG Squard la jijini Tanga lililokuwa likiundwa na wasanii Agustino John ‘Latino Man’ na Malick Bandawe. Kwa sasa anafanya muziki na pia anaendelea na kazi yake ya urubani.

What the fvck is all this nonsense?

Geeez
 
Back
Top Bottom