Hatimaye wameamua kumkamata

CCM washatepeta...wameona hii ni hatari.. lissu yupo ndani Heche anasonga mbele...

Hapa Duniani hakuna mjinga wa milele...watanganyika na wazanzibari wameshastuka - huwezi kuzuia hii kitu

Huyu ni Tundu Antipas Lissu na si Mbowe ambaye mlizoea kuchezea sharubu zake.

Watch out - Dunia nzima muda huu inajua..Mungu wetu anajua na nguvu zake zitawafumua wote.
 
Anafungua nchi!
Anaupiga mwingi
 
Lissu ni mpango wa Mungu hawatamuweza.
 
mimi si mtu wa siasa ila huyu TL ananikumbusha stori fulani ya mchungaji mmoja anaitwa Father of pentecost kule naijeria Bishop idahosa,
kulikuwa na kongamano kubwa litakalo kutanisha wachawi wote duniani wakutane Nigeria, yule bwana hili lilimuudhi sana yeye kama mtumishi wa Mungu kwa nini wachawi wapate gutts za kujitangaza kabisa kwenye vyombo vya habari kwamba wanafanya mkutano wao,

Yeye alichofanya akapinga huo mkutano kupitia hivyo hivyo vyombo vya habari akapita kila sehem kutangaza mkutano hautafanyika!. kila mtu alimshangaa ikiwemo wachungaji wenzake wengine walimshauri asichezee hao wachawi afanye tu huduma yake na kukaa kimya.
idahisa alikataa kukaa kimya waandishi wa habari walimuita mkuu wa wachawi studio na wakamwita na idahosa aeleze mbele yake kuwa hatafanya mkutano... aloo nchi yote ya Nigeria ilisimama kumsikiliza mtu mmoja jasiri alinayekataa na kupinga uchawi na shughuli zao zote..

walivyofika studio mkuu wa wachawi akaanza na tambwe zake, ikiwemo ku quote mistr ya biblia huku akimuambia idahosa hata Mungu hawezi zuia huu mkutano.

kwa unyenyekevu mkubwa idohosa akasema ; Ni kweli kabisa Mungu hawezi kuzuia huu mkutano maana ana ishu nyingi za kufanya hii ishu ndogo hivi si ya Mungu bali ni yangu mimi, akaendelea; mimi ndio niliyezuia na tiyari nimeshazuia na la ziada nataka kusema, Biblia inaniambia nisimuache mchawi akaishi huyu mtu akubali mwenyewe kuwa ni mchawi ili afe sasa hivi hapa😄
yule mchawi akikataa kukiri uchawi wake na kiufupi ule mkutano ulizuiliwa na shughuli zote za kichawi hazikufanyika kumbe raisi wa nchi wa kipindi hicho alikuwa akiangalia ule mdahalo na akavutiwa na confidence ya Mtumishi wa Mungu na hivyo akaamuru kuzuiliwa kwa wageni wengi waliokuwa wanatoka sehemu mbalimbali kuingia naijeria kwa akili ya huo mkutano
 
Badala ya kutumia hili tukio kuunganisha chama nyie mnaendeleza chuki na mgawanyiko. Badala ya kuhakikisha Chadema inaongea kwa sauti moja kuhakikisha Mwenyekiti wake anaachiwa, wewe unachochea moto wa kukigawa chama.

Amandla...
 
Kama magufuli alimshindwa, lissu sio mtu wa kawaida! Na kwa sasa ndo kabisa wanawasha moto kwenye petroli! Wananchi walishaichoka ccm na lissu ni mpango wa Mungu kuwatetea watanzania atakayecheza naye atakakwenda na maji!
Siyo yesu wala mhamad tena bali ni lissu?
 
vibaka na matapeli wa kisiasa siku zote hukamatwa kama kuku kwasabb tu ya midomo chafu ya matusi 🐒
 
LEO TUMEPIGWA MABOMU MJINI MBINGA KATIKA MKOA WA RUVUMA.

Hii ni shajara (diary) iliyotumiwa na Mhe Tundu Lissu muda mfupi kabla hajahutubia wananchi wa Mbinga Mjini. Nilikabidhiwa diary hii muda mabomu yanarindima. Nilihutubia mkutano na kuomba kabla Lissu na Lema hawajahutubia. Ganda linaloonekana ni mabaki ya mabomu yaliyolikuwa yanapigwa. Yalipigwa mabomu mengi ambayo idadi yake inakadiriwa kuzidi zaidi ya 100.

Tulimaliza Mkutano kwa amani na kwa wakati ndipo akaja Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD) na kumtaka aende Kituo cha Polisi. Kulitokea majibizano wakati Lissu anahoji sababu za kutaka aende kituoni. Ilichukua kama dakika 15 kabla Polisi hawajaanza kupiga mabomu.

Nilifanikiwa kuomba kwa muda mfupi kabla ya giza nene la hofu kutanda. Nilikuwa kando ya Mhe. Lissu ndipo wakaanza kutupiga mabomu.
Mabomu yalivyopigwa, watu wakatawanyika na tukabaki na Lissu pamoja na wasaidizi wake.

Wakati mabomu yanaendelea kupigwa, askari wawili wakaja wakanivuta na kunitenga kwa nguvu na Mhe. Lissu. Watu kadhaa walianza kuvuja damu mbele yangu akiwemo mzee mmoja aliyekimbizwa hospitalini.

Nilibaki uwanjani hadharani huku watu wengi wakiwa wameanguka chini. Ndiyo watu wengi wakakimbilia kujificha katika nyumba za karibu.
Nilijisikia siko salama kukimbia au kukaa katika mahali pa kificho. Nilikuwa na maji niliyotumia kunawa ili nibaki salama.

Mzee mmoja aliyeumizwa nimehisi amepigwa na risasi ya moto. Pengine itajulikana baadaye kama ni risasi ya moto au la. Kuna risasi ilifika karibu nami ambayo nilihisi ni ya moto lakini sikuwa na muda wa kutafakari.

Niliendelea kukaa hadharani nikiepuka kuwa katika kificho huku nikiwa kinga ya mama na mtoto wa miezi mitatu hivi ambaye alikuwa katika hali mbaya sana.

Mhe. Lissu na watu wengine watano akiwemo Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa, Mhe. Mayala wamekamatwa. Taarifa kutoka barabarani zinaeleza kuwa walionekana Jeshi la Polisi wakiwa nao kuelekea njia ya Songea.

Kwa taarifa hii umma unajulishwa kuwa Askofu Mwamakula yupo salama.
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Mbinga, Ruvuma 9 Aprili 2025; saa 1:35 jioni
 
Wameshindwa kujibu hoja zake sasa wanakimbilia mabomu na risasi za polisi.
 
Haleluya.
 

Attachments

Hizo ndio 4R za mama Abdul.

Waione kwenye jalada kunguni waandamizi wa mama.

ChoiceVariable The Sunk Cost Fallacy 2 Lucas Mwashambwa .
Hivi hawa CCM wanajua kuwa wanajitengenezea visasi vya baadae bila sababu? Au wanaamini kuwa wao ni watawala wa maisha yote?
Hii yaweza kuwa kiama kwao kama ataingia mtawala mwenye wafuasi wenye kutunza vinyongo na kuanza kulipiza.
CCM mtawaachia wenenu vilio vibaya sana kwa kukosa kwetu kutumia maarifa
 
Nauliza

Hivi mfano Chadema wamechukua madaraka hawa askari polisi waliofanya hivi vitendo watajificha wapi nyuso zao?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…