sasa leo brother
MK254 naomba utengue kauli zako na ukubaliane na mimi kuwa magufuli hakuwa chaguo sahihi la watanzania,bali alipatikana kutokana na vita vya panzi.wakati huu tanzania inapopita leo ni dhahili mataifa ya wenzetu yalioyoendelea yalipita kitambo
Kaka
falcon mombasa weka ushabiki pembeni na uchambue siasa jinsi zilivyo. Magufuli alichaguliwa na wachache ndani ya CCM, vipi naye Lowassa alichaguliwa na nani??? ili awe kiongozi wa Chadema. Pia yeye katokea huko ghafla na kuteka chama, mbona Dr. Sla yupo kimya, hajahudhuria vikao kadhaa vya wanahabari, ni wazi humo ndani kuna mvutano wa kiaina na Mbowe hajali maana yeye labda kahakikishiwa wadhifa wa Waziri mkuu.
Kitu ambacho nawapongeza Watanzania, ni kwamba mmefikia mahali tulikua mnamo mwaka wa 2002, hali ambayo imewafanya CCM wa-panic na wamebaki kimya kutathmini jinsi hii ngoma itachezwa. Ni wazi na dhahiri kweli CCM inaweza pigwa chini, hili limewaingia kichwani na labda watumie umafia na unyang'au, sioni wakipona hapa, maana Lowassa mwenyewe anaifahamu fika CCM, na hamna janja yao asiyoijua. Aidha wacheze kwa
- Kuvuruga ndani ya Chadema, watumie fursa hii Dr. Sla amenuna.
- Waibe kura kwa fujo bila kujali.
- Wamwage hela vijijini, yaani Lowassa na mabilioni zake abaki ameshangaa, maana huko vijijini ndipo kwenye kura.
Wasipofanya yao mapema, Lowassa anauchukua uongozi mchana peupe, na hapo Chadema itaweka bendera ikulu, jambo ambalo lilikua ndoto ya mbali kwa muda. Nimewahi hudhuria vikao na wakuu kadhaa wa Chadema na kila mara niliwaona kama wanaota ndoto tu, lakini hii ndio fursa yao kuongoza nchi.