Bora yako kuliko
MK254 anafuata upepo unakokwenda leo mara magufuli kesho lowasa ujuaji tu
MOTOCHINI Nimekuambia mara nyingi kwamba una ulimbukeni sana kwenye masuala ya siasa. Fahamu mimi na Mkenya mwezangu
Iconoclastes tupo tu kama wadadisi na wachambuzi, na wala hatuegemei upande wowote.
Magufuli anafahamika kama mtendaji, pamoja na kwamba alikua kwenye mazingira magumu ndani ya CCM, alifaulu kupenya na kutenda. Na kufikia hadi sasa, hana doa mbali na tetesi kwamba aliuza nyumba fulani. Hivyo ina maana uongozi wake utakua wenye ujasiri na busara. Kuna kipindi alibomoa nyumba zilizojengwa kwenye hifadhi ya barabara, hadi akabomoa na za wakwe zake bila kusita. Ni mtu mwenye uwezo wa kufanya maamuzi magumu bila uwoga.
Lowassa naye, pia anafahamika kama mtendaji, ila yeye alishindwa kubanana na unyang'au ndani ya CCM na akaamua kushuka. Pamoja na kwamba ametajwa kwenye ufisadi wa Richmond, hamna yeyote aliyejitokeza na kumhusisha moja kwa moja. Mwakyembe alitishia kufanya hivyo, lakini akasita baadaye.
Kwa sasa Lowassa ana mashibiki wengi na kuna uwezekano mkubwa kwa yeye kuibuka mshindi kama UKAWA watamkabidhi wadhifa wa kuwania.
Lakini pia patakua na ushindani wa hali ya juu maana Magufuli naye anakubalika sana. Halafu naona Wasukuma wamechangamka na wengi wapo tayari kujitokeza kwa mamilioni kumpigia kura. Japo Tanzania huwa mnadai kutokua na ukabila, lakini mwenyewe najionea na bila kuambiwa. Hata Wamaasai nao wameibuka kwa ajili ya Lowassa wao na hapakaliki.
Mimi binafsi ingelikua napiga kura Tanzania, basi chaguo langu angekua yule mtu wenu wa Kigoma, Zitto Kabwe. Huyo jamaa huwa nampenda sana na kawaida anadhihirisha kuwa na uchungu na nchi. Amepigana na ufisadi sana, halafu anaonekana kuelewa suluhu za matatizo ya Tanzania. Anaogopwa sana na wafisadi. Siku moja nilikua na kikao na wakuu wa idara muhimu sana Bongo, tukiwa kwenye maongezi, kinara wetu akaanza kuhoji mikakati na utendaji wetu na kutuomba tuwe makini sana ili mapungufu yoyote yasimfikie Zitto Kabwe, maana hatakawia kulipua bungeni. Tangu hiyo siku nilianza kumfuatilia kwa karibu bwa Zitto na nimegundua ni mtu muhimu sana kwenye hiyo nchi yenu, ila kwa nyie wafuata mkumbo, hamtaliona hilo.