Nimeamini kweli sisi Wa afrika hatupendani tena hasa sisi Tanz Maania, ivi ukimwelewesha mtu kitu kama haki unadhani kwa yeye atafaidika sana au?
Basi jamani tulieni niwaambie kuhusu Google Adsense.
Mimi ni web developer kutokea Tanzania na nipo katika hii sector takribani miaka mitano sasa na ninafanya katika katika Envato Market soko lililopo Australia kama mtengeneza wa php script na kama muuzaji katika soko hilo, link ya profile yangu hii hapa
ST2014 | CodeCanyon
Miaka ya nyuma nilikuwa nikitumia Google Adsense ni ilinipatia faida sana, mala ya kwanza nilipata USD 145 = Tsh 250,000.
Kwanza Google Adsense nini?
Google Adsense ni tawi la kampuni ya google ambalo linajihusisha na masuala ya matangazo online ambapo matangazo hayo huweza kuonekana katika mtindo wa banner (460px x 80px n.k), na maandishi (Text).
Katika Google adsense kuna vitu viwili kuna Google Adsense Publisher na Google Adsense Adword (Google Adword).
Unacho takiwa wewe ni kujisajili kama Publisher yaani mtangazaji wa matangazo.
Kujisajili nenda
http://adsense.google.com kisha fuata hatua za usajili.
Ukifika hatua ya pili watangambia uweke jina la Domain name weka jina domain name yoyote ambayo unajua ina lugha ya English kisha SUBMIT form yako, utaambiwa usubiri ndani ya masaa machache subiria, kisha utaona ujumbe katika email yako kwamba "Your account for adsense was approve" na kutankuwa na kiunganishi ambacho kitakupeleka katika kukubali mashaliti yao na kisha kupewa akaunti yako ya adsense publisher.
Ukisha patiwa akaunti utaona kuna mstari mwekundu utatokea katika Dashbord yako ya adsense na watahitaji upaste code katika website yako ulioombea sasa wewe unatakiwa kuondoa kwanza ile domain ulio ombea na kuweka domain yako ambayo inalugha ya kiswahili kama website yako ina lugha ya kiingeleza basi katika form yako utatakiwa ujaze domain name yako.
Hii njia ni njia ambayo itakuwezesha kuwa na akaunti ya adsense kwa wale wenye blog zinazotumia lugha ya kiswahili.
Je! adsense wanalipaje?
Adsense wanalipa kila mwisho wa mwezi yaani tarehe 16 au 22.. inategemea na akaunti yako uli weka pini yao siku gani na kama akaunti imefikisha dola 100.
Pini ni nini?
Pini ni namba ambazo unatumiwa katika P.O. BOX yako uliyo jaza katika form yako wakati wa kujisajili, ambapo akaunti ikifika dola 10 ndiyo wanakutumia PIN hiyo katika P.O. BOX yako.
Na njia nzuri ya kupokea pesa kwa adsense ni BANK, na bank nzuri isiyo na makato ni NBC, mimi nilitumiwa USD145 na nikapokea kama ilivyo katika akaunti yangu ya NBC.
Haya maelezo ni kwa ufupi tu lakini kwa ulefu zaidi uanweza wasiliana nami kwa namba hii 0657 315 394.
Kwa anae hitaji Domain name ninaweza nikamsaidia kwa TSH 50,000 pamoja na kumuunganishia katika blogger yake pamoja na adsense.