FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,028
- 1,924
TUNGO: Hatima ya ujinga wake
MTUNZI: Bux the passionate lover
MWANDISHI: Bux the story teller
MWANZO
Furaha ilikuwa sehemu ya historia ya wapenzi wawili kwenye maisha yao, walikuwa wanaingia kwenye hatua kubwa zaidi kwenye maisha ya mwanadamu yeyote yule aliye hai hata maandiko ya dini yanalielezea hilo kwa usahihi sana.
Ndoa ni ndoto ya kila mwanadamu, inaleta heshima, furaha na pumziko la nafsi wengine wakinogesha na kuita nyonga huwa zinatulia ukifika kwenye hiyo hatua baada ya kumpata huyo mkalia ini.
Jumatano tulivu ndiyo ilikuwa siku ya wapendanao wawili Simon Benedict pamoja na mwanamke wa ndoto zake Cecilia Ambrose, siku hii ilikuwa ni siku ya harusi yao.
Sio ndugu tu bali hata majirani pamoja na wapita njia ambao walihudhuria kwenye sherehe hiyo hawakuacha kutoa maneno mazuri ya kuweza kuisifia wengine wakiona wivu kwa hao wapendanao wawili wakitamani wangekuwa wao kwa jinsi walivyokuwa na furaha ambayo wanadamu wengi huwa hawaipati kabisa kwenye maisha yao yote kwenye tasnia ya mapenzi huenda mpaka wanakufa.
Jua la utosi mida ya saa nane kuelekea saa tisa za mchana eneo husika lilikuwa limepambwa vilivyo, pambio za haja za kuvutia ziliwatoka wanakwaya ambao ni wazi walikuwa wana furaha kupitiliza kwenye pembe moja ya jiji la Dar es salaam ndipo tukio hilo kubwa lilipokuwa linaenda kufanyika mchana wa siku hiyo.
Maeneo ya Posta jijini Dar es salaam katika kanisa kubwa la mtakatifu Joseph (St Joseph Cathedral) ni kanisa kubwa na maarufu sana, ni kanisa ambalo limedumu kwa muda mrefu sana likiwa limejengwa mnamo katikati mwa miaka ya 1897 mpaka 1902 na wamisionari wa kijerumani na kuja kupewa wakfu kuwa kanisa la kiroma mnamo mwaka 1905 hapo ndipo harusi hiyo ilipokuwa imeandaliwa kufanyika.
Bwana harusi alikuwa kwenye suti yake safi ambayo bila shaka fundi aliyekuwa ameitengeneza alitumia zaidi ya robo tatu ya akili yake yote kuweza kuitengeneza ilikuwa imemkaa vyema sana akiwa amesindikizwa na rafiki yake wa siku nyingi Andrew ambaye alihakikisha rafiki yake anapata kile alichokuwa anastahili siku hiyo, ukumbi ulikuwa umejaa na kulipuka kwa furaha aliyekuwa anasubiriwa hapo ni bibi harusi pekee ili jambo hilo litendeke.
Binti Ambrose ambaye kwa majina alifahamika kama Cecilia ndiye kisura aliyekuwa anasubiriwa mchana huo, ni mwanamke aliyekuwa amepata bahati ya kwenda kuitwa mke wa mtu kwenye dunia ambayo kuolewa kwa wanawake imekuwa ni bahati kubwa wakati kiuhalisia ni wajibu na jukumu la kila mtu.
Sifa ya uzuri wake na kiuno laini cha kingoni pamoja na maadili bora aliyo lelewa zilikuwa sababu kubwa za kumfanya bwana Simon asiwe na kauli kabisa anapokuwa mbele ya huyo mwanamke hasa kila aisikiapo sauti nzuri ya kimwali wake huyo ambaye wazazi wake pamoja na ndugu zake wengi wa karibu walikuwa wamesafiri kutoka Songea mkoani Ruvuma mpaka kufika ndani ya jiji la Mzizima lenye kila aina ya vioja kuweza kushuhudia mpendwa wao akiolewa na kuipa heshima kubwa familia yake.
Kwenye viti maalumu alikuwa anaonekana mzee Ambrose akiwa kwenye furaha iliyo pitiliza akimsifia mkewe bibi Ambrose kwa malezi mazuri aliyoweza kumlea binti yao Cecilia.
Kwenye saloon( saluni) moja kubwa sana ya kifahari sana iliyo maalumu kwa ajili ya kupamba maharusi ndiyo sehemu aliyokuwa yupo Cecilia akisindikizwa na jopo la wanawake kadhaa lililochaguliwa kuhakikisha bibi harusi anafana sana kuelekea kwenye siku yake kubwa hiyo, huko nje gari zaidi ya tatu zilikuwa zipo tayari kuhakikisha bibi harusi anafika salama ndani ya ukumbi ambako kulikuwa na mumewe kipenzi.
Bibi harusi alikuwa amepambwa akapambika kwa macho ya kibinadamu tu MUNGU alitulia sana kumuumba mtoto wa watu, alijitazama kwenye kioo yeye mwenyewe moyoni alikiri kwamba alikuwa ni mwanamke mrembo sana nadhani alimuonea sana wivu bwana Simon kwa kubahatika kupata bahati ya kumuoa mwanamke kama yeye.
Huku kanisani bwana Simon aliona kama huyo mwanamke wake anachelewa hivyo alisogea pembeni na kuitoa simu yake ya kisasa mfukoni. Nakumbuka nilimuona vizuri sana kwa sababu mimi nilikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wamehudhuria kwenye lile tukio, muda wote macho yangu yalikuwa yapo kwa mpiga kinanda mle ndani aliyekuwa akikipiga kwa weledi mkubwa utadhani ile sherehe ilikuwa ni yake mwenyewe, kwa vile nilikuwa mbele kabisa ule mjongeo wa bwana Simon kwenda kupiga simu niliuona vizuri sana ikabidi nigeuze macho yako kumtazama bwana harusi huyo alikuwa anataka kufanya nini mpaka asogee pembeni namna hiyo.
Kwenye simu yake hakuwa na shida nyingine zaidi ya kulitafua jina ambalo kwenye kioo kikubwa cha simu yake ya kisasa lili andikwa my Bonnie hakuchelewa akabonyeza kitufe kilicho mruhusu kuipiga simu hiyo, huku upande wa pili simu ilikuwa ikiita na wakati huo alikuwa ameishika msindikizaji mkuu wa bibi harusi, kwenye kioo jina lililo onekana kupiga lilikuwa kimehifadhiwa kama My Clyde likifuatiwa na alama ya upendo pamoja na kakufuli kadogo kuonyesha huyo mtu amefungiwa kwenye moyo wa huyo mwanamke hakuna mtu mwingine anayeweza kuingia tena funguo zilikuwa zimetupwa kwenye bahari ya Hindi ambako hakuna mtu anaweza kuzipata tena.
Binti Ambrose aliipokea kwa bashasha akiwa ametabasamu na uzuri wake wa wazi ukiwa umetaradadi, waliokuwa karibu walibahatika kuona tabasamu adhimu la mrembo huyo pamoja na vishimo viwili kwenye mashavu yake hata wanawake wenzao walimuonea wivu sana kwa namna MUNGU alivyokuwa amempendelea, simu aliiweka sikioni kabla hajaongea chochote aliweza kuisikia sauti ambayo ndiyo pekee alipenda kuisikiliza sana kwenye maisha yake kuliko sauti yoyote ile maskioni mwake.
Wakati nipo pale mbele nilivutiwa sana kusikiliza kile ambacho bwana Simon alikuwa akihitaji kukielezea wakati ule, nilianza kusikia mwanaume akizipangilia na kuzitamka vizuri sarufi nzuri kwa mkewe mtarajiwa ambaye kwa dakika kadhaa alikuwa anaenda kuwa mkewe wa halali kabisa wa ndoa na ndiyo sababu nilivutiwa sana nikaamua kukiandika kisa hiki.
"Nachagua mwenyewe nitakula ndo nile ama nile ndo nitakulaaaaa, najisevia manyama nyama utamu utamu, Naona raha mie unavyonipeleka puta, makodinda mako stamina yanu show show,
Naona raha mie unavyo ishushia kwenye tuta mama, mako dinda mako stamina yani slow slow,
Umeniweza.....mh
Ukinigusa mwili wangu nashtuka moyo paa.......
Baby wangu nishike nisije nikapaa.....
Tena usinipege kiduchu, sugar sugar sugar ....
My life is nothing without you, sugar sugar sugar......
Tena usinipege kiduchu, sugar sugar sugar.........
My life is nothing without you, sugar sugar sugar......
Wahi mapema mama, leo ni siku yetu mke wangu, nakupenda sana malkia. Baada ya kumaliza kuiimba tenzi nzuri sana ambayo imekuwa kivutio kwa watoto wa kike wengi sana mjini wimbo maarufu wa msanii Jay Melody akiwa na Marioo nadhani kwa sababu ya mpangilio mzuri sana wa maneno ya kuvutia bwana Simon aliikata simu yake, niliyasikia vizuri maneno adhimu hayo ambayo nilitamani sana ningekuwa na mtu wa kumpatia hayo maneno ila bahati mbaya sana MUNGU alikuwa hajanipa bado, nilijikuta ninapiga makofi kwa bashasha kwani nilikuaa nimepata somo kubwa sana kutoka kwa bwana Simon.
Sauti kubwa za makelele pale kanisani ilikuwa ishara tosha kugundua kwamba gari zilizokuwa zimemleta bibi harusi pale zilikuwa zimefika kanisani, watu walinyanyuka, vifijo na nderomo ndio yalikuwa mapambio kwa hiyo siku bora, nilikiri kwamba yule bwana alikuwa na macho yenye upeo mkubwa sana sijui ni wapi aliweza kumuona huyo mwanamke ila alikuwa amechagua mwanamke mrembo sana kwenye kila macho ya mwanadamu aliye kamili, nilijikuta natamani sana kuingia kwenye ndoa siku ile ile ila nilikuwa na sababu kuu mbili ambazo kilikuwa kikwazo kikubwa kwangu, yakwanza sikuwa nimemuona mwanamke ambaye alikuwa anaendana na falsafa za maisha yangu kiasi kwamba alikuwa anaweza kuwa mke wa ndoa wengi niliwajaribu kwa vitu vidogo sana hawakuwa wanawake sahihi wa kuwafanya kuwa mama wa familia kabisa, kikwazo cha pili kilikuwa kipato, dunia ya sasa wanawake wengi wanaangalia sana mtu mwenye mfuko mrefu ili kidogo wasiwe na mambo mengi sana wanapo ingia kwenye ndoa, sikuwa moja ya vijana waliokuwa na maisha mazuri hivyo niliishia kuto heshimiwa sana mbele za wanawake.
Ukumbi ulifura kwa shangwe wakati bibi harusi anasogea mbele ya ukumbi, mwendo wa madaha ilikuwa sehemu ya maisha yake mngoni huyu, kiuno kilikuwa ndani ya shela zuri lakini kilionekana namna kilivyo jigawa kwa usahihi, nyuma siongei sana maana kila nikikumbuka nilitamani ningemuoa mimi, sikumuona macho yake haraka kwani alifunikwa, urefu wake kiasi mithilo ya twiga ulitosha kuyatoa meno yote thelathini na mawili ya bwana Simon pale mbele.
Mapenzi, tafsiri sahihi ya kuyaelezea ni namna moyo wako unavyo amua kuyapokea.
It's my passion to talk about love
Bux the passionate lover
Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
MTUNZI: Bux the passionate lover
MWANDISHI: Bux the story teller
MWANZO
Furaha ilikuwa sehemu ya historia ya wapenzi wawili kwenye maisha yao, walikuwa wanaingia kwenye hatua kubwa zaidi kwenye maisha ya mwanadamu yeyote yule aliye hai hata maandiko ya dini yanalielezea hilo kwa usahihi sana.
Ndoa ni ndoto ya kila mwanadamu, inaleta heshima, furaha na pumziko la nafsi wengine wakinogesha na kuita nyonga huwa zinatulia ukifika kwenye hiyo hatua baada ya kumpata huyo mkalia ini.
Jumatano tulivu ndiyo ilikuwa siku ya wapendanao wawili Simon Benedict pamoja na mwanamke wa ndoto zake Cecilia Ambrose, siku hii ilikuwa ni siku ya harusi yao.
Sio ndugu tu bali hata majirani pamoja na wapita njia ambao walihudhuria kwenye sherehe hiyo hawakuacha kutoa maneno mazuri ya kuweza kuisifia wengine wakiona wivu kwa hao wapendanao wawili wakitamani wangekuwa wao kwa jinsi walivyokuwa na furaha ambayo wanadamu wengi huwa hawaipati kabisa kwenye maisha yao yote kwenye tasnia ya mapenzi huenda mpaka wanakufa.
Jua la utosi mida ya saa nane kuelekea saa tisa za mchana eneo husika lilikuwa limepambwa vilivyo, pambio za haja za kuvutia ziliwatoka wanakwaya ambao ni wazi walikuwa wana furaha kupitiliza kwenye pembe moja ya jiji la Dar es salaam ndipo tukio hilo kubwa lilipokuwa linaenda kufanyika mchana wa siku hiyo.
Maeneo ya Posta jijini Dar es salaam katika kanisa kubwa la mtakatifu Joseph (St Joseph Cathedral) ni kanisa kubwa na maarufu sana, ni kanisa ambalo limedumu kwa muda mrefu sana likiwa limejengwa mnamo katikati mwa miaka ya 1897 mpaka 1902 na wamisionari wa kijerumani na kuja kupewa wakfu kuwa kanisa la kiroma mnamo mwaka 1905 hapo ndipo harusi hiyo ilipokuwa imeandaliwa kufanyika.
Bwana harusi alikuwa kwenye suti yake safi ambayo bila shaka fundi aliyekuwa ameitengeneza alitumia zaidi ya robo tatu ya akili yake yote kuweza kuitengeneza ilikuwa imemkaa vyema sana akiwa amesindikizwa na rafiki yake wa siku nyingi Andrew ambaye alihakikisha rafiki yake anapata kile alichokuwa anastahili siku hiyo, ukumbi ulikuwa umejaa na kulipuka kwa furaha aliyekuwa anasubiriwa hapo ni bibi harusi pekee ili jambo hilo litendeke.
Binti Ambrose ambaye kwa majina alifahamika kama Cecilia ndiye kisura aliyekuwa anasubiriwa mchana huo, ni mwanamke aliyekuwa amepata bahati ya kwenda kuitwa mke wa mtu kwenye dunia ambayo kuolewa kwa wanawake imekuwa ni bahati kubwa wakati kiuhalisia ni wajibu na jukumu la kila mtu.
Sifa ya uzuri wake na kiuno laini cha kingoni pamoja na maadili bora aliyo lelewa zilikuwa sababu kubwa za kumfanya bwana Simon asiwe na kauli kabisa anapokuwa mbele ya huyo mwanamke hasa kila aisikiapo sauti nzuri ya kimwali wake huyo ambaye wazazi wake pamoja na ndugu zake wengi wa karibu walikuwa wamesafiri kutoka Songea mkoani Ruvuma mpaka kufika ndani ya jiji la Mzizima lenye kila aina ya vioja kuweza kushuhudia mpendwa wao akiolewa na kuipa heshima kubwa familia yake.
Kwenye viti maalumu alikuwa anaonekana mzee Ambrose akiwa kwenye furaha iliyo pitiliza akimsifia mkewe bibi Ambrose kwa malezi mazuri aliyoweza kumlea binti yao Cecilia.
Kwenye saloon( saluni) moja kubwa sana ya kifahari sana iliyo maalumu kwa ajili ya kupamba maharusi ndiyo sehemu aliyokuwa yupo Cecilia akisindikizwa na jopo la wanawake kadhaa lililochaguliwa kuhakikisha bibi harusi anafana sana kuelekea kwenye siku yake kubwa hiyo, huko nje gari zaidi ya tatu zilikuwa zipo tayari kuhakikisha bibi harusi anafika salama ndani ya ukumbi ambako kulikuwa na mumewe kipenzi.
Bibi harusi alikuwa amepambwa akapambika kwa macho ya kibinadamu tu MUNGU alitulia sana kumuumba mtoto wa watu, alijitazama kwenye kioo yeye mwenyewe moyoni alikiri kwamba alikuwa ni mwanamke mrembo sana nadhani alimuonea sana wivu bwana Simon kwa kubahatika kupata bahati ya kumuoa mwanamke kama yeye.
Huku kanisani bwana Simon aliona kama huyo mwanamke wake anachelewa hivyo alisogea pembeni na kuitoa simu yake ya kisasa mfukoni. Nakumbuka nilimuona vizuri sana kwa sababu mimi nilikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wamehudhuria kwenye lile tukio, muda wote macho yangu yalikuwa yapo kwa mpiga kinanda mle ndani aliyekuwa akikipiga kwa weledi mkubwa utadhani ile sherehe ilikuwa ni yake mwenyewe, kwa vile nilikuwa mbele kabisa ule mjongeo wa bwana Simon kwenda kupiga simu niliuona vizuri sana ikabidi nigeuze macho yako kumtazama bwana harusi huyo alikuwa anataka kufanya nini mpaka asogee pembeni namna hiyo.
Kwenye simu yake hakuwa na shida nyingine zaidi ya kulitafua jina ambalo kwenye kioo kikubwa cha simu yake ya kisasa lili andikwa my Bonnie hakuchelewa akabonyeza kitufe kilicho mruhusu kuipiga simu hiyo, huku upande wa pili simu ilikuwa ikiita na wakati huo alikuwa ameishika msindikizaji mkuu wa bibi harusi, kwenye kioo jina lililo onekana kupiga lilikuwa kimehifadhiwa kama My Clyde likifuatiwa na alama ya upendo pamoja na kakufuli kadogo kuonyesha huyo mtu amefungiwa kwenye moyo wa huyo mwanamke hakuna mtu mwingine anayeweza kuingia tena funguo zilikuwa zimetupwa kwenye bahari ya Hindi ambako hakuna mtu anaweza kuzipata tena.
Binti Ambrose aliipokea kwa bashasha akiwa ametabasamu na uzuri wake wa wazi ukiwa umetaradadi, waliokuwa karibu walibahatika kuona tabasamu adhimu la mrembo huyo pamoja na vishimo viwili kwenye mashavu yake hata wanawake wenzao walimuonea wivu sana kwa namna MUNGU alivyokuwa amempendelea, simu aliiweka sikioni kabla hajaongea chochote aliweza kuisikia sauti ambayo ndiyo pekee alipenda kuisikiliza sana kwenye maisha yake kuliko sauti yoyote ile maskioni mwake.
Wakati nipo pale mbele nilivutiwa sana kusikiliza kile ambacho bwana Simon alikuwa akihitaji kukielezea wakati ule, nilianza kusikia mwanaume akizipangilia na kuzitamka vizuri sarufi nzuri kwa mkewe mtarajiwa ambaye kwa dakika kadhaa alikuwa anaenda kuwa mkewe wa halali kabisa wa ndoa na ndiyo sababu nilivutiwa sana nikaamua kukiandika kisa hiki.
"Nachagua mwenyewe nitakula ndo nile ama nile ndo nitakulaaaaa, najisevia manyama nyama utamu utamu, Naona raha mie unavyonipeleka puta, makodinda mako stamina yanu show show,
Naona raha mie unavyo ishushia kwenye tuta mama, mako dinda mako stamina yani slow slow,
Umeniweza.....mh
Ukinigusa mwili wangu nashtuka moyo paa.......
Baby wangu nishike nisije nikapaa.....
Tena usinipege kiduchu, sugar sugar sugar ....
My life is nothing without you, sugar sugar sugar......
Tena usinipege kiduchu, sugar sugar sugar.........
My life is nothing without you, sugar sugar sugar......
Wahi mapema mama, leo ni siku yetu mke wangu, nakupenda sana malkia. Baada ya kumaliza kuiimba tenzi nzuri sana ambayo imekuwa kivutio kwa watoto wa kike wengi sana mjini wimbo maarufu wa msanii Jay Melody akiwa na Marioo nadhani kwa sababu ya mpangilio mzuri sana wa maneno ya kuvutia bwana Simon aliikata simu yake, niliyasikia vizuri maneno adhimu hayo ambayo nilitamani sana ningekuwa na mtu wa kumpatia hayo maneno ila bahati mbaya sana MUNGU alikuwa hajanipa bado, nilijikuta ninapiga makofi kwa bashasha kwani nilikuaa nimepata somo kubwa sana kutoka kwa bwana Simon.
Sauti kubwa za makelele pale kanisani ilikuwa ishara tosha kugundua kwamba gari zilizokuwa zimemleta bibi harusi pale zilikuwa zimefika kanisani, watu walinyanyuka, vifijo na nderomo ndio yalikuwa mapambio kwa hiyo siku bora, nilikiri kwamba yule bwana alikuwa na macho yenye upeo mkubwa sana sijui ni wapi aliweza kumuona huyo mwanamke ila alikuwa amechagua mwanamke mrembo sana kwenye kila macho ya mwanadamu aliye kamili, nilijikuta natamani sana kuingia kwenye ndoa siku ile ile ila nilikuwa na sababu kuu mbili ambazo kilikuwa kikwazo kikubwa kwangu, yakwanza sikuwa nimemuona mwanamke ambaye alikuwa anaendana na falsafa za maisha yangu kiasi kwamba alikuwa anaweza kuwa mke wa ndoa wengi niliwajaribu kwa vitu vidogo sana hawakuwa wanawake sahihi wa kuwafanya kuwa mama wa familia kabisa, kikwazo cha pili kilikuwa kipato, dunia ya sasa wanawake wengi wanaangalia sana mtu mwenye mfuko mrefu ili kidogo wasiwe na mambo mengi sana wanapo ingia kwenye ndoa, sikuwa moja ya vijana waliokuwa na maisha mazuri hivyo niliishia kuto heshimiwa sana mbele za wanawake.
Ukumbi ulifura kwa shangwe wakati bibi harusi anasogea mbele ya ukumbi, mwendo wa madaha ilikuwa sehemu ya maisha yake mngoni huyu, kiuno kilikuwa ndani ya shela zuri lakini kilionekana namna kilivyo jigawa kwa usahihi, nyuma siongei sana maana kila nikikumbuka nilitamani ningemuoa mimi, sikumuona macho yake haraka kwani alifunikwa, urefu wake kiasi mithilo ya twiga ulitosha kuyatoa meno yote thelathini na mawili ya bwana Simon pale mbele.
Mapenzi, tafsiri sahihi ya kuyaelezea ni namna moyo wako unavyo amua kuyapokea.
It's my passion to talk about love
Bux the passionate lover
Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app