mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,076
- 4,113
Mdada mmoja ameitikia wito wa Mkuu wa Mkoa Dar, Paul Makonda kuhusu wanawake waliotelekezewa watoto kufika ofisini kwake ili kupata msaada wa kisheria. Dada huyo amejitokeza na kudai yeye ni mtoto wa Mzee Edward Lowassa.
Amesema..
Habari zaidi, soma=>Aliyedai kuwa mtoto wa Lowassa akamatwa na Polisi, ni baada ya kuomba radhi
Amesema..
''Nimetokea Kigamboni, nimekuja hapa, nimekuja kusikiliza wito wa mkuu wa mkoa, Makonda kwamba watu ambao wametelekezwa. Sasa mimi ni mmoja wa mtoto ambaye niliyetelekezwa, ambaye baba yangu ni Edward Lowassa. Nimeanza kumtafuta toka nikiwa darasa la sita na mama ananambia ni kweli baba yako ndio huyo huyo. Sasa nimefuatilia kila sehemu lakini sioni mafanikio kwa hiyo nimekuja hapa kwa mkuu wa mkoa Makonda anisaidie kwa hali na mali kwa vyovyote vile itakavyokuwa kama nipo tayari nipimwe DNA na huyo mzee Lowassa ili nisaidiwe nijue nakaa wapi. Kwasababu mama yangu mzazi yupo hata akija atatoa ushahidi na atasema kwamba itakuwaje kama DNA nipimwe basi.''
Habari zaidi, soma=>Aliyedai kuwa mtoto wa Lowassa akamatwa na Polisi, ni baada ya kuomba radhi