kmbwembwe
JF-Expert Member
- Aug 16, 2012
- 10,940
- 7,847
Binafsi nimeshituka kusikia waziri anasema kati ya cheti feki kiasi cha alfu kumi na tano hivi 4000 wamerudishwa. Kiasi hiki ni kikubwa sana. Hii inatia shaka kama zoezi la kuwatambua lilifanyika vizuri. Vinginevyo tuamini cheti feki wanatumia ujanja na rushwa kurudishwa kazini. La msingi kutambua cheti feki ni fisadi wenye hila kubwa na ni hatari sana kwa mstakabali wa weledi nchini. Ni watu waovu kupindukia. Wapo wasomi na wataalam wahitimu wa kweli wengi wamedhulumiwa na hawa vibaka ambao wameweza kuwadhibiti wasomi wakweli sehemu zao za kazi hivyo kudhuru ufanisi wa kazi sehemu nyingi. Yafaa umma kufuatilia na kupewa taarifa kuona kama kweli vyeti feki wanaorudi wanavyo vyeti halali.