Watumishi waliorejeshwa kazini ni wale walioondolewa kazini mwaka 2017 kwa maagizo ya kuwataka wakatafute sifa ya kuwa na cheti cha kidato cha nne

BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Jan 12, 2019
328
414
Wiki hii palizuka taarifa ya upotoshaji iliyodai Serikali imewarudisha kazini watumishi wa umma zaidi ya 4,000 walioondolewa kazini mwaka 2017 kwa sababu ya kughushi vyeti na watumishi hewa.

Msemaji Mkuu wa Serikali Ndugu Gerson Msigwa leo Jumamosi Agosti 28, 2021 wakati anazungumza na Wanahabari ametolea ufafanuzi taarifa hiyo kwa kusema:-

Watumishi waliorejeshwa kazini na kurudishwa kwenye orodha ya malipo ya mshahara ni wale ambao walioondolewa kazini mwaka 2017 kwa maagizo ya kuwataka wakatafute sifa ya kuwa na cheti cha kidato cha nne. Watumishi hawa ni wale wote ambao waliajiriwa kabla ya mwaka 2004 kwa sifa ya elimu ya darasa la 7.

Kwahiyo Serikali imewarudisha kazini na kuwarejeshea malipo yao ya mshahara watumishi hao 4,380 ambao baada ya kuondolewa kazini kwa sababu hawakuwa na sifa ya kidato cha 4, walikwenda kutafuta sifa ya elimu ya kidato cha 4 na sasa wameipata na ndiyo pekee ambao Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa kwa niaba ya Serikali ameagiza warudishwe kazini lakini sio wale walioondolewa kazini kwasababu ya kughushi vyeti na wale watumishi hewa, hao hawatarejeshwa tena kazini.

Kwahiyo taarifa ya kwamba Serikali imewarejesha kazini watumishi walioondolewa kwasababu ya vyeti feki na watumishi hewa ni ya uongo na ya upotoshaji mtupu.

#KaziInaendelea
 
Mmmmh cheti cha form tu walikuwa nacho? kama hapana wamewezaje wote kuwa na cheti cha form 4? na mbona wale wa Darasa la saba hawakuondolewa ushahidi ninao na wote walibaki na ajira zao.
Mimi pia wapo nawajua wana elimu ya la saba ingawa wana vikozi vya vidogovidogo vya kazini na wanaendelea kupiga kazi
 
Mmmmh cheti cha form tu walikuwa nacho? kama hapana wamewezaje wote kuwa na cheti cha form 4? na mbona wale wa Darasa la saba hawakuondolewa ushahidi ninao na wote walibaki na ajira zao.
Hakuna darasa la Saba alieajiriwa kabla ya 2004 aliondolewa. Wanachokwepa kusema ni kuwa kuna watu waliondolewa kimakosa hivyo walifanya uhakiki baada ya MTU mmojammoja kulalamika. Vyeti vilivyoleta shida ni vya form 4. Kuna dada ni Nesi ni ndugu yangu alikumbwa na hili zoezi. Msigwa Apache uongo kama WA Sirro.
 
Mmmmh cheti cha form tu walikuwa nacho? kama hapana wamewezaje wote kuwa na cheti cha form 4? na mbona wale wa Darasa la saba hawakuondolewa ushahidi ninao na wote walibaki na ajira zao.
Yeye ndiye ana jichanganya!!ni hivi kabla ya 2004, hata mtu aliyekuwa na elimu ya std 7, alikuwa na sifa ya kuajiriwa serikalini, na hao hawakutakiwa kuondolewa kazini, ila wale waliokuwa na elimu ya std 7, walioajiriwa kuanzia 2004 kwenda mbele, na hawakujiendeleza na kupata elimu ya kidato cha nne, ndio walioondolewa kazini.Hivyo wanaorudishwa ni hao wa std 7 walioajiriwa kabla ya 2004, na wale tu waliojiriwa kuanzia 2004, lakini walijiendeleza na kupata cheti cha kidato cha nne, halisi.
 
Yeye ndiye ana jichanganya!!ni hivi kabla ya 2004, hata mtu aliyekuwa na elimu ya std 7, alikuwa na sifa ya kuajiriwa serikalini, na hao hawakutakiwa kuondolewa kazini, ila wale waliokuwa na elimu ya std 7, walioajiriwa kuanzia 2004 kwenda mbele, na hawakujiendeleza na kupata elimu ya kidato cha nne, ndio walioondolewa kazini.Hivyo wanaorudishwa ni hao wa std 7 walioajiriwa kabla ya 2004, na wale tu waliojiriwa kuanzia 2004, lakini walijiendeleza na kupata cheti cha kidato cha nne, halisi.
Sijui walijiendelezaje wakati hawakupewa masharti kuwa wakajiendeleze. Wao walikatiwa mishahara tu bila hata kupewa barua na sababu wakaambiwa kwa mdomo kuwa hawana cheti cha form 4, ilikuwaje mpaka wakaanza kujiendeleza? Toka 2017 mpaka leo ni miaka 3, wamefanya mtihani wa QT na wa Form 4 na kupata vyeti haraka hivyo?? Hizi ni stori tu
 
Yeye ndiye ana jichanganya!!ni hivi kabla ya 2004, hata mtu aliyekuwa na elimu ya std 7, alikuwa na sifa ya kuajiriwa serikalini, na hao hawakutakiwa kuondolewa kazini, ila wale waliokuwa na elimu ya std 7, walioajiriwa kuanzia 2004 kwenda mbele, na hawakujiendeleza na kupata elimu ya kidato cha nne, ndio walioondolewa kazini.Hivyo wanaorudishwa ni hao wa std 7 walioajiriwa kabla ya 2004, na wale tu waliojiriwa kuanzia 2004, lakini walijiendeleza na kupata cheti cha kidato cha nne, halisi.
Sasa kama aliondolewa kihalali kwanini amerudi baada ya kujiendeleza wakati wapo wengi wenye kuhitaji hizo nafasi na wana vyeti vyao
 
Mmmmh cheti cha form tu walikuwa nacho? Kama hapana wamewezaje wote kuwa na cheti cha form 4? Na mbona wale wa Darasa la saba hawakuondolewa ushahidi ninao na wote walibaki na ajira zao.
Sawa kabisa. Alichoongea Msigwa ni uongo sheria na utaratibu wa ajira hauko hivyo

Kama hao waliajiriwa kwa sifa ya darasa la saba na hakukuwa na condition yoyote kwamba tunakuajiri kwa cheti cha darasa la 7 na unapewa muda fulani kujiendeleza basi hao watu kuondolewa kwenye nafasi zao walionewa, hovyo kabisa maana sheria hiyo imekuja bada ya wao kuajiriwa

Msigwa katulisha tango pori, sheria haifanyi kwa kurudi nyuma bali kwa kwenda mbele!
 
Hakuna darasa la Saba alieajiriwa kabla ya 2004 aliondolewa. Wanachokwepa kusema ni kuwa kuna watu waliondolewa kimakosa hivyo walifanya uhakiki baada ya MTU mmojammoja kulalamika. Vyeti vilivyoleta shida ni vya form 4. Kuna dada ni Nesi ni ndugu yangu alikumbwa na hili zoezi. Msigwa Apache uongo kama WA Sirro.
Binafsi sijakuelewa
 
Yeye ndiye ana jichanganya!!ni hivi kabla ya 2004, hata mtu aliyekuwa na elimu ya std 7, alikuwa na sifa ya kuajiriwa serikalini, na hao hawakutakiwa kuondolewa kazini, ila wale waliokuwa na elimu ya std 7, walioajiriwa kuanzia 2004 kwenda mbele, na hawakujiendeleza na kupata elimu ya kidato cha nne, ndio walioondolewa kazini.Hivyo wanaorudishwa ni hao wa std 7 walioajiriwa kabla ya 2004, na wale tu waliojiriwa kuanzia 2004, lakini walijiendeleza na kupata cheti cha kidato cha nne, halisi.
Sielewi hasa kama anataakiwa atoe ufafanuzi au atoe taarifa. Waziri wa kazi na ajira/utumishi je,? Huenda nakosea.

Sent from my Nokia 6.1 using JamiiForums mobile app
 
Watarudi na pocha za graduation ya f4 wamevaa majoho ya chuo kikuu. Na wakirudi watakuwa na nyodo yaani 'njoo kesho' zinarudi tutakoma
 
Wiki hii palizuka taarifa ya upotoshaji iliyodai Serikali imewarudisha kazini watumishi wa umma zaidi ya 4,000 walioondolewa kazini mwaka 2017 kwa sababu ya kughushi vyeti na watumishi hewa.

Msemaji Mkuu wa Serikali Ndugu Gerson Msigwa leo Jumamosi Agosti 28, 2021 wakati anazungumza na Wanahabari ametolea ufafanuzi taarifa hiyo kwa kusema:-

Watumishi waliorejeshwa kazini na kurudishwa kwenye orodha ya malipo ya mshahara ni wale ambao walioondolewa kazini mwaka 2017 kwa maagizo ya kuwataka wakatafute sifa ya kuwa na cheti cha kidato cha nne. Watumishi hawa ni wale wote ambao waliajiriwa kabla ya mwaka 2004 kwa sifa ya elimu ya darasa la 7.

Kwahiyo Serikali imewarudisha kazini na kuwarejeshea malipo yao ya mshahara watumishi hao 4,380 ambao baada ya kuondolewa kazini kwa sababu hawakuwa na sifa ya kidato cha 4, walikwenda kutafuta sifa ya elimu ya kidato cha 4 na sasa wameipata na ndiyo pekee ambao Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa kwa niaba ya Serikali ameagiza warudishwe kazini lakini sio wale walioondolewa kazini kwasababu ya kughushi vyeti na wale watumishi hewa, hao hawatarejeshwa tena kazini.

Kwahiyo taarifa ya kwamba Serikali imewarejesha kazini watumishi walioondolewa kwasababu ya vyeti feki na watumishi hewa ni ya uongo na ya upotoshaji mtupu.

#KaziInaendelea
Hizo sifa walizitafutia wapi , na wakati mnawatuma kutafuta hizo sifa mlikuwa mnawalipa ? wadanganyeni wajinga
 
Back
Top Bottom