Hataki nimchukue mwanangu, sijui anataka nini kwangu?

juvenile davis

JF-Expert Member
Apr 13, 2015
4,752
4,467
Kama mjuavyo kwamba ninao watoto watatu wa mama tofauti,SEAN,TRAVIS na MOUREEN,.sasa hao wa kiume wote wawili nilishawachukua na wapo pale kwa mama yangu mzazi na nimewatafutia house girl.wote wapo nursery shule moja maarufu hapa dsm na wana miaka minne wote ila wamepishana miezi tu.sasa nataka na Moureen nimchukue nimpeleke kwa mama pia ila mama Mama moureen hataki kunipa mwanangu kabisa.na huyu ndie mkubwa maana ana miaka 6.yupo darasa la kwanza.nataka nimchukue akae kwa mama yangu na wale wenzake maana naona naingia hasara sana kuhudumia huku na kule.ni bora niwe natuma pesa sehemu moja ieleweke moja.sasa mwenzangu kila nikiongelea kumchukua mtoto anakuja juu sana.nashindwa kuelewa lengo lake.tafadhari mama moureen najua upo humu na unasoma sana nyuzi zangu nakuomba unipe mwanangu ..
 
Hakunaga kitu kama 'mtoto wa kwangu'..

chukulia mfano wa nyumba au gari ambayo umechangia nusu na mtu mwingine..utaweza sema ni nyumba au gari yako?

sasa mtoto si kitu cha thamani kuliko gari au nyumba?

why useme wako? why mama mtoto asishiriki kupanga maendeleo ya mwanae?

Kwani malezi ni shule tu na kuweka housegirl?
 
Hakunaga kitu kama 'mtoto wa kwangu'..

chukulia mfano wa nyumba au gari ambayo umechangia nusu na mtu mwingine..utaweza sema ni nyumba au gari yako?

sasa mtoto si kitu cha thamani kuliko gari au nyumba?

why useme wako? why mama mtoto asishiriki kupanga maendeleo ya mwanae?

Kwani malezi ni shule tu na kuweka housegirl?
Acha mambo ya lodilofa
 
Na ujanja wako wote unapeleka watoto kwa mama?

Mama amekulea wewe na pia unataka alee wajukuu tena?

Muda wa mama kula pensheni yako sio kumjazia mizigo ya kulea.

Chukua hao watoto ukae nao wewe.

Na pia kuwa 'sperm donor' sio ujanja.
Kama sijaoa hao watoto nakaaje nao??hakuna bibi anayekataa wajukuu,kwani wanamgasi nini wakat kuna mfanyakaz
 
wasiwasi wangu kumlundikia mama yako watoto 3! hata kama kuna housegirl ina maana ni wa 4 loooh! kumzeesha mma yako umuongezee kero ya watu wa nne huoni aibu?

hata kama unatoa hela ! kutoa hela inayowatosheleza watu wanne asubuhi hadi jioni na mahitaji mengine ni myingi sana maana ni sawa na gharama za mtu mwenye mke watoto 2& house girl ni hela nyingi mama unampa shingapi?
 
Bibi halei mtoto ila anafuga mtoto. Uangalizi wa bibi na uangalizi wa mzazi ni vitu viwili tofauti, bib atahakikisha mtoto anakula na kuwa na afya njema ila kitabia hatamfatilia. Ila mzazi atakuwa karibu zaidi na mtoto hata pale mtoto abadilikapo tabia mzazi ni rahisi kugundua na kumnyoosha mapema. Ndo maana watoto wengi waishio na bibi wana tabia za ajabu kuliko wale walioishi na wazazi. Hitimisho muache huyo #Maureen akae na mama yake , kwa bibi aende kutembea tu.
 
Ninadhani ungependa watoto wote wakue pamoja, mama Moureen ana msimamo tofauti, je anakuruhusu kumchukua Moureen aspend weekend na bibi yake?
 
Back
Top Bottom