kayumba yumba
Member
- Mar 9, 2015
- 93
- 182
Naomba ujumbe huu umfikie mh Jakaya Mrisho Kikwete, Amiri jeshi mkuu wa jamhuri ya muungano Tanzania, Rais aliyebakiwa na siku chache, masaa machache kuiacha Ikulu. Swala la kuiacha ikulu ni swala la kikatiba, tena lipo wazi hakuna wa kulipinga.
Nimefuatilia hotuba ya Rais J. K, kwa makini sana, hasa kwenye kipengele kile cha uchaguzi. Ametumia hasira, ameongea kwa ghadhabu na vitisho vingi kwa watu wa upinzani.
Nikajiuliza sana juu ya kauli zake.
Kwanza nilijihoji mwenyewe kwamba haya maazimisho ni ya chama cha mapinduzi CCM au ni maazimisho ya kilele cha Mwenge au ni maazimisho ya kifo cha mwasisi wa Taifa Letu Mwl. J. K. Nyerere? Maswali haya yalinijia baada ya kuona Mh J. KIKWETE ameuvaa U CCM na sio Urais.
Najua sina uwezo wa kumfikia moja kwa moja Mkuu wa nchi, ila ujumbe wangu utamfikia moja kwa moja au kupitia kwa wapambe wake.
Mh Rais naomba utambue mambo mawili matatu toka kwetu sisi tulio malofa na wapumbavu.Na kwa nia njema kabisa naomba ujue kuwa
1.Hatutaogopa kupigwa mabomu, kufungwa, kuuwawa au lolote kwa kutafuta haki yetu ya msingi. Tunaamin kuwa kifo ni siku moja tu wala sio mara mbili.
2.Tutapiga kura zetu na kuzilinda kwa mjibu wa sheria, taratibu na kanuni za uchaguzi wala si vinginevyo.
Hakuna wakututisha hata kidogo ndani ya nchi yetu ambayo tunaamini ni ya kidemokrasia.
3.Tutahakikisha mgombea tunayemhitaji anashinda kwa kumpigia kura nyingi za kutosha na kuhakikisha hakuna atakayeiba kura zetu, najua mwalijua hilo.
5.Kwa umoja wetu tutashirikiana na vyombo vyote kulinda amani ya nchi yetu Tanzania.
5.Tutatoa ushirikiano kwa yeyote anayependa haki itendeke, na tutamdhibiti atakayejaribu kupoka haki yetu.
Ikumbukwe mita 100 sio mbali sana ni sawa na usawa wa gori moja hadi gori jingine katika uwanja wa mpira.
Rais Kikwete kitendo cha kututishia kuwa tutakaolinda kura tutadhibitiwa na umeyaongea maneno haya kwa hasira kuu, unatudhihirishia wazi kuwa Chama chako cha CCM kimejipanga kuiba kura au kufanya kinyume na taratibu za uchaguzi .
Kama mlipanga mbinu chafu mkadhani tutaogopa basi imekula kwenu, tunatambua wazi kuwa, kuna magari mengi ya washawasha, askari wengi, vitendea kazi vya kisasa lakini sisi tunasema hatutaogopa vifaa hivyo kwakuwa sisi sio watu wa fujo ni watu wa haki.
Mwisho napenda Mh J. KIKWETE atambue kuwa yeye kaongoza kwa miaka yake 10 na anakwenda kupumzika, hivyo aende akapumzike kwa amani kabisa, ajiepushe na matamko yatakayokuja kumpeleka ICC wakati hakustahili kwenda huko hata kidogo, na Tr 25/10/2015 akapige kura alipojiandikishia amchague anayempenda yeye, awe diwani, Mbunge au Rais
Japo kwa Heshima na Taadhima namuomba kura yake upande wa Rais ampigie Mh Edward Lowassa, na naamini atampigia kura.
Naomba nimalize kwa kusema WATANZANIA wote tujitokeze Tr 25/10/2015 tukawapigie kura viongozi tunaoona wanafaaa,binafsi nawaomba kura za Mh. EDWARD LOWASSA na naamini tutampigia kura za kutosha na tutazilinda kwa amani bila vurugu yoyote ile. Tudumishe amani na upendo.
Ahsante
Nimefuatilia hotuba ya Rais J. K, kwa makini sana, hasa kwenye kipengele kile cha uchaguzi. Ametumia hasira, ameongea kwa ghadhabu na vitisho vingi kwa watu wa upinzani.
Nikajiuliza sana juu ya kauli zake.
Kwanza nilijihoji mwenyewe kwamba haya maazimisho ni ya chama cha mapinduzi CCM au ni maazimisho ya kilele cha Mwenge au ni maazimisho ya kifo cha mwasisi wa Taifa Letu Mwl. J. K. Nyerere? Maswali haya yalinijia baada ya kuona Mh J. KIKWETE ameuvaa U CCM na sio Urais.
Najua sina uwezo wa kumfikia moja kwa moja Mkuu wa nchi, ila ujumbe wangu utamfikia moja kwa moja au kupitia kwa wapambe wake.
Mh Rais naomba utambue mambo mawili matatu toka kwetu sisi tulio malofa na wapumbavu.Na kwa nia njema kabisa naomba ujue kuwa
1.Hatutaogopa kupigwa mabomu, kufungwa, kuuwawa au lolote kwa kutafuta haki yetu ya msingi. Tunaamin kuwa kifo ni siku moja tu wala sio mara mbili.
2.Tutapiga kura zetu na kuzilinda kwa mjibu wa sheria, taratibu na kanuni za uchaguzi wala si vinginevyo.
Hakuna wakututisha hata kidogo ndani ya nchi yetu ambayo tunaamini ni ya kidemokrasia.
3.Tutahakikisha mgombea tunayemhitaji anashinda kwa kumpigia kura nyingi za kutosha na kuhakikisha hakuna atakayeiba kura zetu, najua mwalijua hilo.
5.Kwa umoja wetu tutashirikiana na vyombo vyote kulinda amani ya nchi yetu Tanzania.
5.Tutatoa ushirikiano kwa yeyote anayependa haki itendeke, na tutamdhibiti atakayejaribu kupoka haki yetu.
Ikumbukwe mita 100 sio mbali sana ni sawa na usawa wa gori moja hadi gori jingine katika uwanja wa mpira.
Rais Kikwete kitendo cha kututishia kuwa tutakaolinda kura tutadhibitiwa na umeyaongea maneno haya kwa hasira kuu, unatudhihirishia wazi kuwa Chama chako cha CCM kimejipanga kuiba kura au kufanya kinyume na taratibu za uchaguzi .
Kama mlipanga mbinu chafu mkadhani tutaogopa basi imekula kwenu, tunatambua wazi kuwa, kuna magari mengi ya washawasha, askari wengi, vitendea kazi vya kisasa lakini sisi tunasema hatutaogopa vifaa hivyo kwakuwa sisi sio watu wa fujo ni watu wa haki.
Mwisho napenda Mh J. KIKWETE atambue kuwa yeye kaongoza kwa miaka yake 10 na anakwenda kupumzika, hivyo aende akapumzike kwa amani kabisa, ajiepushe na matamko yatakayokuja kumpeleka ICC wakati hakustahili kwenda huko hata kidogo, na Tr 25/10/2015 akapige kura alipojiandikishia amchague anayempenda yeye, awe diwani, Mbunge au Rais
Japo kwa Heshima na Taadhima namuomba kura yake upande wa Rais ampigie Mh Edward Lowassa, na naamini atampigia kura.
Naomba nimalize kwa kusema WATANZANIA wote tujitokeze Tr 25/10/2015 tukawapigie kura viongozi tunaoona wanafaaa,binafsi nawaomba kura za Mh. EDWARD LOWASSA na naamini tutampigia kura za kutosha na tutazilinda kwa amani bila vurugu yoyote ile. Tudumishe amani na upendo.
Ahsante