Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 359,888
- 828,474
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imeanza kuchukua hatua za kuwaondoa wafanyabiashara wanaofanya shughuli zao katika maeneo yasiyo rasmi, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa, Albert Chalamila, wakati wa ufunguzi wa Soko Kuu la Kariakoo.
Akizungumza katika hafla hiyo, RC alisema kuwa ingawa hatua hiyo inaweza kuonekana kuwa ngumu au chungu kwa baadhi ya wafanyabiashara, ni muhimu kulinda mpangilio wa jiji na kuhakikisha barabara zinabaki wazi. Alisisitiza kuwa utekelezaji wake utaendelea kufanywa kwa kutumia diplomasia na maelewano, badala ya nguvu.
Akizungumza katika hafla hiyo, RC alisema kuwa ingawa hatua hiyo inaweza kuonekana kuwa ngumu au chungu kwa baadhi ya wafanyabiashara, ni muhimu kulinda mpangilio wa jiji na kuhakikisha barabara zinabaki wazi. Alisisitiza kuwa utekelezaji wake utaendelea kufanywa kwa kutumia diplomasia na maelewano, badala ya nguvu.