Harusi bila mchango

Varbo

JF-Expert Member
Aug 14, 2012
1,117
856
Habari I wana JF mdogo wangu anataka kufanya harusi budget yake ni 14,000000 hataki mchango wa harusi kwa mtu yoyote watu wa kuhudhulia 200. Je pesa hio itatosha. Waliohudhuria Kamati za harusi naomba michango yenu ya mawazo.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Taarifa zako hazijakamilika kuweza kupewa muongozo mzuri.Anyway 14M inaweza kuwa ndogo sanaaa au kubwa sanaaa mpk pale utakapotoa na dadavua taarifa zako sahihi.

Fox


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Akizingatia budget management ambayo ni 14M itamtosha....akitaka kuridhisha wageni wake wote 200 hakuna kiasi kitakachotosha hata aongeze vipi since pesa haijawahi kutosha
 
Mimi nataka kwenye harusi yangu nisipokee mchango wa mtu halafu nitatoa mualiko one week before


sf
 
Akizingatia budget management ambayo ni 14M itamtosha....akitaka kuridhisha wageni wake wote 200 hakuna kiasi kitakachotosha hata aongeze vipi since pesa haijawahi kutosha
Mbona sio mbaya sana maana kwa chakula itategemeana anataka sahani ya kiasi gani. Cake ni cheap, ukumbi haugharimu unless atake zile sehemu flashy, usafiri, mapambo, magari na gharama za wageni kama atakuwa nao.
14 m naona kama inatosha kiasi
 
Taarifa zako hazijakamilika kuweza kupewa muongozo mzuri.Anyway 14M inaweza kuwa ndogo sanaaa au kubwa sanaaa mpk pale utakapotoa na dadavua taarifa zako sahihi.

Fox


Sent using Jamii Forums mobile app

Budget ni m14 wageni 200. Je hio budget inatosha. Harusi ni ya kikristo it’s means hio pesa itoshe ukumbi, Mc, picha usafiri na chakula kwa hio pesa.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nataka kwenye harusi yangu nisipokee mchango wa mtu halafu nitatoa mualiko one week before


sf
Inabidi uwe na moyo na kusimamia maamuzi yako mkuu bila hivyo kuna people wanajua kuyumbisha mawazo ya watu,mi shahidi.
 
Habari I wana JF mdogo wangu anataka kufanya harusi budget yake ni 14,000000 hataki mchango wa harusi kwa mtu yoyote watu wa kuhudhulia 200. Je pesa hio itatosha. Waliohudhuria Kamati za harusi naomba michango yenu ya mawazo.


Sent using Jamii Forums mobile app
Shalom,....

Mosi,kwa uzoefu wangu ni kwamba usipowashirikisha waalikwa kwa ama njia ya kuimba michango au mipango ya maandalizi ya harusi,wengi huwa hawahudhiriihata kama utatoa mwaliko.

Pili,gharama kubwa za harusi huwa ni Chakula,vinywaji na mapambo.Gharama nyingine huwa ni fixed kama bei ya ukumbi,mc,music,dj....kwa.sasa bei ya dj mkali.kwa hapa dsm si chini ya Tshs 2.5mil.

Muhimu,ni kuandaa orodha ya wageni wote wanaotegemewa kualikwa.Waombwe kuthibitisha uwepo wao kwenye harusi hiyo kwa tarehe unayokusudia ili uweze kufanya mipango mapema pamoja na kufanya makadirio hasa ya chakula na vinywaji,uzuri hata vinywaji vikibaki bado kuna nafasi ya kuvirejesha kwa supplier ila atanunua kwa bei ya jumla.

Tofauti na Chakula ambapo kikiandaliwa hakirejeshwi endapo kama hakitatumika na hivyo huishia kuwa hasara.

Mwisho,kiasi hicho cha tshs 14mil,kinatosha sana kufanya harusi ya wageni 200.

Mpe hongera sana mdogo wako na Mwenyezi Mungu awajalie maharusi maisha ya mema yenye kheri na furaha ktk ndoa yao.

Kuoa na kuolewa ni jambo la kheri.

Wasalaam,

Mwenzetu



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inatosha kabisa itategemea mkoa uliopo
1. Ukumbi 1.500.000
2. Chakula aweke mpishi 3.500.000=
3. Mapambo kawaida 1.800.000
4. Vinywaji beer soda whisky 2.500.000 kila mmoja beer 4 na kali kidogo itajiset yenyewe
5. Cake nzuri tu 600.000
6. MC na Music 800.000
7. Picha 200 na Video 800.000
8. Usafiri gari la maharusi 400.000 marafiki wanajitolea magari unaweka mafuta.
9. Usafiri wa wakwe 300.000 na wachache wa wakwe.
Total 12.200.000
10. Inayobaki matumizi mengine 1.800.00









Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bado mpango wangu upo palepale, harusi yangu haitozidi watu 50, eneo ni open areas probably beach, hakutokuwa na michango just ndugu na marafiki wa karibu tu, PERIOD!
 
Yaani mil.14 unatoa kuwafurahisha watu? Duh kweli tunatofautiana. Alafu huyo mke ndo anakuja kuliwa kimasihala na uliowaalika bure waje waone kifaa chako hahaaaaaaa. Tunachezea pesa sana. Sio mbaya sijui unapookota hizo pesa. Mwambie hazitoshi afanye mil. 28 ili wageni wapate pa kulala pia.
 
Inabidi uwe na moyo na kusimamia maamuzi yako mkuu bila hivyo kuna people wanajua kuyumbisha mawazo ya watu,mi shahidi.

Maisha ya siku hizi ni stress tu. Tena kama mtu unataka kuoa huk bado unasaka mkwanja katika hali ya juu ni kosa kubwa sana. Nadhani ni bora usioe kabisa kama huna maisha MAZURI kweli kwelikweli. Na kama unategemea mapenzi ya dhati baada ya kuoa yawe constant unahitaji msaada wa Mungu na sio juhudi zako. Kwangu mimi faida ya kuoa ninayo iona ni kuzaa watoto ndani ya circle ya ndoa kwani hii ni nzuri kuliko kuwa na watoto walio tapakaa.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom