Strawberry
JF-Expert Member
- Nov 29, 2012
- 274
- 108
Hivi hizo harufu unazisikiaga wewe tu?Mie mbona nakuvumilia sana harufu yako ya mdomo na miguu honey wangu wala sikutangazi kwa watu loh.
Mmh, haya
Huwezi jua kama forest inaongeza kikwapa sababu kila mtu kazoea kikwapa chake
Ila ukweli ndio huo, msitu ni sumaku ya kikwapa
NB: Mie bado mdogo sijaanza mambo ya kuota v.z.
kama msemaji wa awali alivotangulia kusema kuna vikwapa aina 2, ....1.cha asili na 2.cha uchafu kwakile cha uchafu ni kweli kuna haja ya kuwasema hawa watu ili walau wakiweza wajirekebishe ila kwa wale ambao ambao na wa asili mi kimtazamo wangu naona ni kama kukisema kilema cha mtu ni najisikia huruma na aibu kukisemea vile najua sio kwa mapenzi yake bali ndo jinsi alivozaliwa, na kwa mnavojua vipodozi na marashi ya kutibu tatizo kama hili ni ghali mno kwa vile ukitibu na vipodozi vya kichina ndo tatizo linakuwa kubwa balaa.
Ila kwa kweli
Kuna wanawake sijui nisemeje hata
Wanawaachia waume zao kama mashamba ya katani, bila uangalizi wowote
Mwanamme anarudia shati na vesti ya ndani siku 2
Boksa na soksi nazo anarudia
Anamwacha tu msitu wa kongo unamea kama amazon foresti, kweli?? Afu unalalaje naye?
Binadamu hata kama una kwapa la asili, kuna jinsi ya kulipunguza
Kwanza hakikisha misitu yote imefyekwa kabisa
Afu jaribu body spray au body mist au zote kwa pamoja
Oga asubuhi na jioni
Mbona harufu inapungua kabisa?
Hivi hizo harufu unazisikiaga wewe tu?Mie mbona nakuvumilia sana harufu yako ya mdomo na miguu honey wangu wala sikutangazi kwa watu loh.
Sasa ndipo nimepata sababu ya kwanini wanaume wanaSISITIZA 'usafi' wa mke mtarajiwa pindi wawekapo mabango ya kutafuta wachumba; kumbe wao ni WACHAFU na USAFI wao hutegemea MWANAMKE.
Halafu sijawahi kuona mwanamke akisisitiza USAFI kwa mwanaume.
hapo unamaanisha .......mwanaume anarudia suruali na shati siku mbili tatu ,yaani unajiuliza alilala kwa mkewe au vipi?
kuna wanawake magatuso jamani acha!
Halafu hawa jamaa wapendaga sana stori za kunyanyua nyanyua mikono na mambo ya ku hug wenzao