Harufu mbaya kikwapa: Wanaume wako pia.....

Harufu mbaya kikwapa: Wanaume wako pia.....

Wiyelelee

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2012
Posts
1,071
Reaction score
348
Umewahi kukutana na mtu mwenye harufu mbaya ya kikwapa? Mwaka jana, nilikuwa ofsini nafanya kazi kama kawa mida ya ashubuhi. Pembeni kulikuwa na chai yangu. Aliingia dada mmoja hivi, du! Hata hamu ya kunywa chai iliishia hapo. Japo alihitaji ushauri wa kitalaam, nilimvumilia sana na nilipomalizana nae, ilinibidi nifungue madirisha yote ili harufu mbaya itoke. Alikuwa na harufu ya kikwapa ile mbaya, japo alivaa vizuri sana na ni mrembo.

Jana tu nilikuwa na mkutano kwenye ofisi moja kubwa. Jamaa niliekaa nae karibu balaa! Sijui aliweka mzoga wa panya kwenye kikwapa ata sielewi. Nilipomtazama vizuri, nikakuta ana pete ya ndoa! Nikajiuliza hivi mke wake hasikii harufu hiyo? Jamani, huenda huyu mtu anasoma JF hapa, hebu msaidie aondokane na harufu ya kikwapa. Mezani tuliwekewa juice ya azam na korosho wala sikugusa kitu, hata maji sikunywa kabisa.

Wewe mke wa huyu jamaa, huoni aibu? Au na wewe una tatizo la kikwapa? Watu wengine bwana...
 
Kwasabau unahela ndo mana unasema ivo. Ungekua huna afu akaku-propose usinge kataa.
 
Unajua kuna vitu viwili watu hawaelewi, kuna kikwapa cha uchafu na cha asili.

Hawa wenye vikwapa vya asili ni balaa, anaweza kuoga asuhuni safi akaenda azini ile purushani ya daladala na kutembea kidogo tu, atatoa harufu kama kuna mzoga wa mbwa pembeni!!

Watu hawa huwa nawaonea huruma sana. Sasa sijui huyo mtu anaangukia group gani hapo?
 
Halafu hawa jamaa wapendaga sana stori za kunyanyua nyanyua mikono na mambo ya ku hug wenzao
 
Ila kwa kweli
Kuna wanawake sijui nisemeje hata
Wanawaachia waume zao kama mashamba ya katani, bila uangalizi wowote

Mwanamme anarudia shati na vesti ya ndani siku 2
Boksa na soksi nazo anarudia

Anamwacha tu msitu wa kongo unamea kama amazon foresti, kweli?? Afu unalalaje naye?

Binadamu hata kama una kwapa la asili, kuna jinsi ya kulipunguza
Kwanza hakikisha misitu yote imefyekwa kabisa
Afu jaribu body spray au body mist au zote kwa pamoja
Oga asubuhi na jioni

Mbona harufu inapungua kabisa?
 
Ila kwa kweli
Kuna wanawake sijui nisemeje hata
Wanawaachia waume zao kama mashamba ya katani, bila uangalizi wowote

Mwanamme anarudia shati na vesti ya ndani siku 2
Boksa na soksi nazo anarudia

Anamwacha tu msitu wa kongo unamea kama amazon foresti, kweli?? Afu unalalaje naye?

Binadamu hata kama una kwapa la asili, kuna jinsi ya kulipunguza
Kwanza hakikisha misitu yote imefyekwa kabisa
Afu jaribu body spray au body mist au zote kwa pamoja
Oga asubuhi na jioni

Mbona harufu inapungua kabisa?


I like this indeed. Wakati natafuta mchumba, wenye harufu ya kikwapa nilikuwa nawapita mbali... Jamani watu tuna u busy gani hadi tulimikize msitu wa pande kwenye kikwapa?
 
Kwasabau unahela ndo mana unasema ivo. Ungekua huna afu akaku-propose usinge kataa.

Kwa vyovyote vile, ila mimi sio mwanamke.... Na hata kama nisingekuwa na kazi yangu ni marufuku kumfuata mtu ambae anaweza kutafuta ufumbuzi wa tatizo alilo nalo akaupata ila hafanyi hivyo. Lengo ni kumsaidia aondokane na tatizo hili pengine yeye hajui.
 
Jamani tuache uvivu, hapa kwenye jukwaa kila siku hivi vitu vinajadiliwa na mbinu mbadala zinatolewa hapa kwa kuangalia hali halisi ya mifuko ya watanzania wa hali zote. Sasa nastaajabu kabisa kuona bado tunachangia kwa lugha kali na sisi tunaojua hatuko tayari kuwafunza wengine tujirekebishe.
 
Ila kwa kweli
Kuna wanawake sijui nisemeje hata
Wanawaachia waume zao kama mashamba ya katani, bila uangalizi wowote

Mwanamme anarudia shati na vesti ya ndani siku 2
Boksa na soksi nazo anarudia

Anamwacha tu msitu wa kongo unamea kama amazon foresti, kweli?? Afu unalalaje naye?

Binadamu hata kama una kwapa la asili, kuna jinsi ya kulipunguza
Kwanza hakikisha misitu yote imefyekwa kabisa
Afu jaribu body spray au body mist au zote kwa pamoja
Oga asubuhi na jioni

Mbona harufu inapungua kabisa?
sio shamba la katani,ni steel wire!
 
Hakuna kitu kinaongeza harufu ya kwapa kama msitu wa pande

Ni kiboko aisee, afu hata ndimu hukata kabisa hii makitu

I like this indeed. Wakati natafuta mchumba, wenye harufu ya kikwapa nilikuwa nawapita mbali... Jamani watu tuna u busy gani hadi tulimikize msitu wa pande kwenye kikwapa?
 
Makalio ya sufuria hayaogopi moto, unataka ubembelezwe wakati una tatizo?

Fumba macho usisome

Jamani tuache uvivu, hapa kwenye jukwaa kila siku hivi vitu vinajadiliwa na mbinu mbadala zinatolewa hapa kwa kuangalia hali halisi ya mifuko ya watanzania wa hali zote. Sasa nastaajabu kabisa kuona bado tunachangia kwa lugha kali na sisi tunaojua hatuko tayari kuwafunza wengine tujirekebishe.
 
HIlo tatizo ambalo linakwisha, ahakikishe kwenye sehemu zake za siri hakuna nyasi, pawe peupe, halafu aoge kwa kutumia koshekoshe(dodoki) sabuni ya kunukia na maji safi, ajisugue kote, akimaliza hapo apake Doudorant na perfume , awe anakunywa maji mngi ili kusaidia kuondoa hiyo harufu.
Pia asiwe anarudia nguo zake za ndani( underware, vesti, sox) pamoja na shati. awe anavaa kila siku nyingine.
Nafikiri kama atafanya haya hawezi kuwa ananuka kikwapa.
 
sio shamba la katani,ni steel wire!

Hahahahha! nimecheka kwa kweli... Nimeambiwa hapa kwamba hata maji ya ukoko yanaondoa harufu hiyo kali. Sufuria likipikiwa ugali, liwekee maji hadi kesho asubuhi... then tumia ukoko huo kwa dakika tano kabla ya kuogo kwa wiki moja tu.
 
Yaani unaona mtu ana pete ya ndoa afu unawaza, hivi kaoa kweli ama anatania
mwanaume anarudia suruali na shati siku mbili tatu ,yaani unajiuliza alilala kwa mkewe au vipi?
kuna wanawake magatuso jamani acha!
 
Ni kweli wenye kikwapa cha asili na cha uchafu unajua tofauti yake. Nafikiri Wiyelele anaongelea wale wenye kikwapa cha asili. Yaani hao hata wakioga harufu ni ile ile. Nina rafiki yangu yuko hivyo, mzuri kweli, very smart MBA graduate lakini kikwapa utakimbia! Personality yake ni bomba kweli lakini. Ana marafiki kibao.

Nafikir watu wa namna hii inabidi waangalie sana wanachokula. Nilichogundua ni hali chakula kizuri , yaani anashindia junk food, kahawa nyingi, vyakula vilivotengenezwa na unga wa ngano, mchele n.k. Hanjwi maji mengi na mboga hagusi.

Nina uhakika boyfriend wake hakuisikia hiyo harufu. Kuna wengine hawaisikii hiyo harufu au wanasikia harufu nyingine inayowapendeza, na si ile kali wengine tunayoisikia.


Unajua kuna vitu viwili watu hawaelewi, kuna kikwapa cha uchafu na cha asili.

Hawa wenye vikwapa vya asili ni balaa, anaweza kuoga asuhuni safi akaenda azini ile purushani ya daladala na kutembea kidogo tu, atatoa harufu kama kuna mzoga wa mbwa pembeni!!

Watu hawa huwa nawaonea huruma sana. Sasa sijui huyo mtu anaangukia group gani hapo?
 
Last edited by a moderator:
Yaani unaona mtu ana pete ya ndoa afu unawaza, hivi kaoa kweli ama anatania

Alinipa wakati mgumu sana nikaanza kumuwaza mke wake bure kwamba yukoje? Alimtoa wapi? Uhusiano wao ukoje? Wana watoto? Harufu ya mke wake akiwa ananyonyesha inakuaje? Je wanabusiana? Wanashikana wapi au sehemu zipi? HAdi mkutano ukawa mbaya kabisa...
 
I like this indeed. Wakati natafuta mchumba, wenye harufu ya kikwapa nilikuwa nawapita mbali... Jamani watu tuna u busy gani hadi tulimikize msitu wa pande kwenye kikwapa?
Afadhali ungemchukua huyo mwenye kikwapa, ungemtafutia tiba mbadala, na ungekuwa na amani kwenye ndoa yako, kuliko anayenukia halafu huna amani ,matokeo yake, unalala kinondoni, moyo, akili na mapenzi yako kimara!! Lipi Jema hapo Wiyelele?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom