Harambee ya Prof. Muhongo yapatikana Tsh 40,000 tu

Harambee ya Prof. Muhongo yapatikana Tsh 40,000 tu

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2015
Posts
14,242
Reaction score
34,917
Harambee aliyoiendesha Prof. Muhongo kwa maafisa alioandamana nao Bukoba, yakusanya TZS 40,000/-

Ziara aliyoifanya waziri wa nishati na madini Sospeter Muhongo katika mtaa wa Hamugembe iligeuka kuwa harambee baada ya waathirika wa tetemeko la ardhi kudai msaada wa chakula na mahema

Hali hiyo ilimlazimu Prof. Muhongo kuitisha mchango wa fedha kutoka kwa maofisa aliokuwa nao na kufanikiwa kupata 40,000 na kuwakabidhi wakazi hao.

Mkazi wa mtaa huo Sadick Shaban alilalamika kuwa waathirika wa tetemeko hilo hawajapata misaada inayotolewa, mkazi mwingine Adventina Shumuni amedai tangu maafa hayo yatokee wametembelewa na afisa wa Tanesco aliyewaachia 20,000 tu baada ya kuwahurumia kwa kukosa makazi

Chanzo: Mwananchi
 
🙂🙂🙂🙂 huyu Prf kusema kweli haaminiki, hata hii serikali haiaminiki sema ndio vile tu watu wameguswa na janga miksa kuoneana aibu na imani.
 
Huyu prof. Ni mchangiaji mzuri tu, kule kwao amenunua ambulance ambayo haipatikani mikoa mingi hapa tz.
 
Daaaaah hii nchi ngumu sana!!
Yaani hata Mimi kwenye group la wattaup tumekusanya milion 4,650,00 halafu professor anashindwa kufikisha hata laki 1 ?
 
Back
Top Bottom