Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,788
- 218,420
Leo hii ni siku ambayo tunakumbuka Kuzaliwa kwa Mpigania Haki muhimu wa Tanzania Askofu Emmaus Mwamakula , ambaye wapenda haki wengi wanamuita Desmond Tutu , huku wengine wakimuita Malcom X .
Mwamakula ni Miongoni mwa Viongozi wachache sana wa dini wa kiafrica walioamua kusimama na wananchi katika kupigania haki , hakuwahi kuogopa mikwara ya Watawala wala hakuwahi kuogopa kukamatwa , hakujali hata alipodhalilishwa na Lazaro Mambosasa , bali yeye alisimama na wananchi na kiukweli bado yuko na wananchi wakati huu tukielekea kwenye kupata Katiba mpya.
Si rahisi kuelezea umuhimu wa Askofu huyu kwa nchi hii , Lakini kwa ufupi naomba kumtakia Baba Askofu huyu Maisha marefu , Amina .