Hapa Ndipo waziri wa Mambo ya Ndani Lugola anaweza kuangukia pua!

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Waziri wa mambo ya ndani ametoa agizo kwamba kiongozi wa Act, Zitto, akamatwe kwa "kufanya" mkutano wa hadhara nje ya jimbo lake.

Ukifikiria, inawezekana kabisa kwamba Zitto alifanya hivyo makusudi ili hili suala la wabunge kutohutubia nje ya majimbo yao liweze kupatiwa ufumbuzi wa kisheria katika mahakama. Japo Lugola ana background ya sheria, anaweza akawa ameingia kichwa kichwa katika hili na kujikuta anaangukia pua, na kuumbuka yeye, rais na serikali ya CCM kwa ujumla. Mambo makubwa matatu yanayoweza kufanya Lugola aangukie pua ni yafuatayo;
  1. Kwanza Zitto hakufanya mkutano wa hadhara, bali alialikwa katika mkutano halali wa hadhara
  2. Zitto ni kiongozi wa kitaifa, na uongozi wake wa kitaifa unampa wigo wa kufanya kazi yake ya kisiasa sehemu yoyote hapa Tanzania
  3. Hakuna sheria ambayo inamkataza mwanasiasa nchini kufanya mkutano wa hadhara popote nchini, na katiba inaruhusu hilo, hasa ikizingatiwa kwamba tamko la rais halina nguvu ya kisheria, na pale tamko la rais linapopingana na sheria basi mahakama zitatoa uamuzi kulingana na sheria, sio tamko la rais.
Hivyo basi, nina uhakika popote pale alipo Zitto atakuwa anamwambia Lugola bring it on - twende mahakamani!
 
Last edited by a moderator:
Hili tamko lina ukakasi kidogo hata kwa sisi ambao tuna muamini na kumshabikia utendaji wake Mh. JPM.
 
Hata kwenye familia mkuu wa family ukifanya mambo ya kipuuzi kunakuwa na uwezekano mkubwa tabia hizo kufanywa na watoto wako. Kama nchi sasa hivi mambo ya hovyo yameanza kutokea juu na yanakuja chini kwa kasi
 
Kwani nani kakuambia Nchi yetu inaendeshwa kwa mujibu wa sheri?
Nchi yetu inaendeshwa na sheria Mkuu, ila wengi wetu tumeamua kukubali matamko yatuongoze

Kama Mwanahalisi nao wangekubali matamko yawaongoze, wasingekuwa wakitutamkia kwamba Mwanahalisi linarudi mitaani wiki ijayo.

We need to emancipate ourselves from "matamko" slavery
 
Huku ni Kulewa madaraka Zitto hajafanya kosa kwa mujibu wa sheria za nchi hii
 
Waziri wa mambo ya ndani ametoa agizo kwamba kiongozi wa Act, Zitto, akamatwe kwa "kufanya" mkutano wa hadhara nje ya jimbo lake.

Ukifikiria, inawezekana kabisa kwamba Zitto alifanya hivyo makusudi ili hili suala la wabunge kutohutubia nje ya majimbo yao liweze kupatiwa ufumbuzi wa kisheria katika mahakama. Japo Lugola ana background ya sheria, anaweza akawa ameingia kichwa kichwa katika hili na kujikuta anaangukia pua, na kuumbuka yeye, raisi na serikali ya CCM kwa ujumla. Mambo makubwa matatu yanayoweza kufanya Lugola aangukie pua ni yafuatayo;
  1. Kwanza Zitto hakufanya mkutano wa hadhara, bali alialikwa katika mkutano halali wa hadhara
  2. Zitto ni kiongozi wa kitaifa, na uongozi wake wa kitaifa unampa wigo wa kufanya kazi yake ya kisiasa sehemu yeyote hapa Tanzania
  3. Hakuna sheria ambayo inamkataza mwanasiasa nchini kufanya mkutano wa hadhara popote nchini, na katiba inaruhusu hilo, hasa ikizingatiwa kwamba tamko la raisi halina nguvu ya kisheria, na pale tamko la raisi linapopingana na sheria basi mahakama zitatoa uamuzi kulingana na sheria, sio tamko la raisi.
Hivyo basi, nina uhakika popote pale alipo Zitto atakuwa anamwambia Lugola bring it on - twende mahakamani!
Lugola ataumia kwani kwenye hizi kampeni za uchaguzi wa marudio wabunge na viongozi mbali mbali wa ccm wataenda kupiga kampeni kwny mikutano ya hadhara.
 
Mh. Bangi Lugola, Mwili tembo, akili sisimizi. Ameingia kichwa kichwa kwa Zitto, hakika ataumbuka.
 
Back
Top Bottom