nachukia sana sms za aina hii manake zinawaadhibu watoto ambao ni safi kabisa.
je, unaunga mkono migomo kama moja ya njia ya kuishinikiza serikali kutimiza madai yenu?
Mi nadhani hapa wa kulaumiwa ni serikali ambayo kwa makusudi kabisa wameamua kuwadharau na kuwatelekeza walimu. Serikali yetu imeamua kwa makusudi kudhoofisha mfumo wa elimu yetu.
Wewe kama ni mwalimu kweli,basi utakuwa uko mjini ambapo kuna huduma zote na unaweza kuzipata kwa urahisi.wenzako wa huko swekeni wanataabika vibaya mno,hawana makazi ya kuishi (nyumba za kupanga ni za tope), maji shida,huduma nyingine za kijamii kama vituo vya tiba viko mbali na dawa hazipatikani (hata store za dawa ni issue), huduma za mawasiliano shida, umeme hakuna.
Wenzako huko wanalazimika kusafiri umbali mrefu kufuata mshahara,na inambidi wakati mwingine kulala hukohuko mpaka siku ya pili (shida ya usafiri,foleni huko benki,network kwenye atm)
waulize walimu wa huko malinyi (ulanga),mngeta,mlimba,mang'ula(kilombero);likolombe(tandahimba),chawi,mahurunga(mtwara rural) wanavyotaabika.
Huko shuleni hata vifaa vya kufundishia shida, hawana chaki, hawana madaftari ya maazimio,kwingine hata vitabu vya mhutasari ya masomo shida.
Mwalimu wa namna hiyo atakuwa na moyo na morali ya kufundisha kweli ilhali hata hajui atakula nini?
Hebu tuwe wakweli ndugu zangu, walimu wana hali ngumu sana!
Mbona serekali inawaadhibu waalimu ambao ni safi kabisa?
Ishu ya waalimu sio ndogo kama unavyoifikiria bi mkubwa, Binadamu yoyote, narudia tena yoyote, huwa anafanyakazi kutokana na matarajio ya ujira. Kweli unategemea waalimu waendelee kuwa na moyo wa kazi katika mazingira haya ya sasa? Na kama hawana moyo ulitegemea nini mrembo?
Serekali ilipotumia ubabe kurudisha waalimu kazini toka kwenye mgomo kweli hawakutegemea hili?
Bimkubwa kama wewe ni mwalimu ni dhahiri hufundishi primari za kijijini au st kayumba sekondari, basi kaa kimya tu usiwashangae wanaotaabika.
Ubarikiwe sana
skiliza nikwambie BHULULU waalim wangeunga mkono hoja ya kujitoa CWT ingekuwa safi sana but under an umbrella of CWT never will it be ukombozi wa mwl ukatokea.Hata walimu hawapendi kugoma kimoyomoyo ila serikali ndiyo inayolazimisha haya yote."Dharau kwa walimu"Kumbuka mwalimu peke yake hawezi kuboresha elimu nchini ni pamoja na serikali.Unajitolea kufundisha halafu unakatishwa tamaa maana yake nini?Acha tu atakaebahatika atatokamo.
Je, unaunga mkono migomo kama moja ya njia ya kuishinikiza serikali kutimiza madai yenu?
Mi nadhani hapa wa kulaumiwa ni serikali ambayo kwa makusudi kabisa wameamua kuwadharau na kuwatelekeza walimu. Serikali yetu imeamua kwa makusudi kudhoofisha mfumo wa elimu yetu.
Wewe kama ni mwalimu kweli,basi utakuwa uko mjini ambapo kuna huduma zote na unaweza kuzipata kwa urahisi.Wenzako wa huko swekeni wanataabika vibaya mno,hawana makazi ya kuishi (nyumba za kupanga ni za tope), maji shida,huduma nyingine za kijamii kama vituo vya tiba viko mbali na dawa hazipatikani (hata store za dawa ni issue), huduma za mawasiliano shida, umeme hakuna.
Wenzako huko wanalazimika kusafiri umbali mrefu kufuata mshahara,na inambidi wakati mwingine kulala hukohuko mpaka siku ya pili (shida ya usafiri,foleni huko benki,network kwenye ATM)
Waulize walimu wa huko Malinyi (ulanga),Mngeta,Mlimba,mang'ula(Kilombero);Likolombe(Tandahimba),Chawi,Mahurunga(Mtwara rural) wanavyotaabika.
Huko shuleni hata vifaa vya kufundishia shida, hawana chaki, hawana madaftari ya maazimio,kwingine hata vitabu vya mhutasari ya masomo shida.
Mwalimu wa namna hiyo atakuwa na moyo na morali ya kufundisha kweli ilhali hata hajui atakula nini?
HEBU TUWE WAKWELI NDUGU ZANGU, WALIMU WANA HALI NGUMU SANA!
kwani mbinu pekee ya kutatua hili tatizo ni kubomoa majengo na kuchoma vitabu??
wanaweza wakademonstrate kwa amani, wakatumia chama chao kupeleka hoja mahususi, wakatumia asasi za kiraia kupeleka ujumbe na wakaskilizwa.
unless wewe sio mwl lkn ungekuwa ni mwl basi ungeelewa ninachomaanisha manake hata tatizo la mwl sio salary peke yake. kama ishu ni mshahaa mbona hilo in rahisi kulisemea??
imagine mwaka 2012/2013 waalimwaliostahili kupanda vyeo hawajapandishwa simply kwasasabu serikali haina hela na ulitumwa waraka kwamba serikali haina pesa ya kupandisha vyeo kwani watakosa hela za mishahara mipya.
wafikiri kwa situation kama hii na wakati kupanda cheo ni haki ya mtumish wa umma, ukigoma kufundisha itakuwa ni sahihi?? kwann CWT isifungue kesi dhidi ya jamhuri kwamba watumisha wake wamenyimwa haki yao ya msingi?? tena kwa kufanya hivi wangeifanya serikali iwajibike pasavyo.
tuache kutuana midaid ya ugomvi tufikiri in a more positive way dhidi ya watoto wetu tunaowafundisha.
Sina uhakika kama wewe ni Mwl, serious kabisa!
They will not help me at all, what I meant is that you comment as if you are not in the field!kama utapenda jaribu hata kusoma Wiliam Maslo's Hierarchy of Needs then angalia maisha ya mwl. na uangalie kama walimu wanahaki ya kufanya hivyo au la!hahahahah! nikupa tsd namba?? na cheque namba pamoja na ed/pf namba??
They will not help me at all, what I meant is that you comment as if you are not in the field!kama utapenda jaribu hata kusoma Wiliam Maslo's Hierarchy of Needs then angalia maisha ya mwl. na uangalie kama walimu wanahaki ya kufanya hivyo au la!
Tatizo lingine ni pale watu tunaposhindwa kuadress matatizo yetu kwa mtu husika, swala la CWT ni lingine na swala la madai ya walimu kwa serikali ambaye ndiyo mwajili ni jingine, inawezekana kabisa CWT wanamapungufu lakini je si kwa umoja wa walimu CWT inaweza kubadilika?Je CWT ndo wanachangia mwl. asipandishwe cheo? Mwl. asongezewe mshahara? Asiwe na mazingira mazuri ya kufanyia kazi? Kusiwe na Vitabu mashuleni, chaki, viti na meza za walimu , nyumba za walimu nk? Je unataka kuniambia CWT hawajafanya hata moja la maana? Si semi hawana mapungufu!tatio mnaenda kwa hisia na sio kutumia akili. hivi mnafikiri hasimu wa mwl ni serikali?? basi kaa uchunguze vzr utakuja kuniambia hasimu wa mwl ni nani. manaishkilia na kuikumbatia CWT ambayo kila mwez inawakata % ya mshahara halafu haiwasaidii kwa chochote kile zaid ya kununua magari mazuri ya kupanda viongozi na samani za ofc basi. lkn haijawah kusmama kwa dhati kumtetea mwl ikashinda halafu mnaona sawa??nakuambia mm ukombozi wa mwl haupo kama bado kitu kinaitwa CWT kitakuwepo, na ukweli acha niitwe mhaini nakwenda kufile kujitoa kwenye cwt mahakaman tena nikiwa na sababu nzito.
swala hapa hatupaswi kuwahukumu innocent kids. bali tujenge hoja kwa serikalini,na sio kuadhibu watt
migomo imefanyika, majadiliano yamefanyika, au wewe una njia ipi ya kujenga hoja?
skatai mkuu waalim wana hali ngumu sana ila kwa mwl yyte yule atajua kwamba hasimu wa mwl wala sio serikali bali ni CWT yaani chini ya hawa watu ambao wako corrupted watu ambao wamesaini kushikilia misimamo ya vyama vya siasa na si kusimamia haki za wanachama wao ni shida. mimi ingawa napigwa vita sana lkn daima nasema ukweli juu ya CWT huyu ndiye anayeua waalimu ingawa kila mwezi huwa anakata 16% ya mshahara ya huu mwl kama monthly contribution fee.
Tatizo lingine ni pale watu tunaposhindwa kuadress matatizo yetu kwa mtu husika, swala la CWT ni lingine na swala la madai ya walimu kwa serikali ambaye ndiyo mwajili ni jingine, inawezekana kabisa CWT wanamapungufu lakini je si kwa umoja wa walimu CWT inaweza kubadilika?Je CWT ndo wanachangia mwl. asipandishwe cheo? Mwl. asongezewe mshahara? Asiwe na mazingira mazuri ya kufanyia kazi? Kusiwe na Vitabu mashuleni, chaki, viti na meza za walimu , nyumba za walimu nk? Je unataka kuniambia CWT hawajafanya hata moja la maana? Si semi hawana mapungufu!
sasa mkuu ngoja nikwambie kitu, cwt kama chama cha watumish kilipaswa kuwasaidia waalim kupeleka madai yao na kuyasmamia, tena kilaipaswa kiwe mstari wa mbele kuona kama mwl anatendewa haki yake badala ya kila mwl kusimama alone.Sikatai mkuu kwamba CWT ni moja ya maadui wa walimu wa nchi hii, lakini hatupaswi kuiweka kando serikali ambayo ndiyo mwajiri wa hao walimu na pia ndio mwenye dhamana ya kuisimamia sekta ya elimu nchini.
Madai ya walimu yameelekezwa kwa mwajiri wao sio CWT.
Serikali ndio yenye wajibu wa kuhakikisha kuwa sekta ya elimu iko poa,kuna walimu wakutosha,vitendea kazi,maslahi bora kwa walimu;ina wajibu wa kuboresha mazingira afanyiayo kazi mwalimu,makazi yake na mazingira bora ya kule unakompeleka kufundisha...Sasa kama haitimizi wajibu wake lazima ishinikizwe kufanya hivyo...Na hii ni kwa njia mbalimbali ikiwemo style wanayoitumia sasa(kama kweli), baada ya ile ya mazungumzo na mgomo kufail.
Kwa sasa acha kwanza waidai serikali kuboresha hali zao na za kazi zao, then wautazame umoja wao (CWT) na kuon kama unawasaidia,ikiwezekana waufumue uongozi mzima wa CWT.....LAKINI HII IWE BAADA YA KUFANIKIWA KUPATA HAKI ZAO.
TUWASAIDIE WALIMU KUISHINIKIZA SERIKALI KUTIMIZA MADAI YAO,ILI WAWEZE KUFUNDISHA WATOTO WETU VIZURI NA KWA AMANI.
swala la serikalia kushindwa kuskiliza matatizo ya waalim linachangiwa na CWT kama hujui. umewah kuwa kiongozi hata wa cwt wa kata ukaskia mambo yalivyo??? basi usingesema haya. serikali ni mtekelezaji na kama nyie kwenye umoja wenu hakuna mnachodai kwa umoja hawawez kuwafikiria.
nenda nchi za watu utaona vyama vya wafanyaazi ndivyo vinavyotetea maslah ya wanachama wake lkn hapa kwa cwt hali sio hiyo. wao kila kitu ni ndio mzee ndio mzeee ptuuuuuuuuuuuuuuuuu
siungi na wala sitaunga mkono uhamasishaji wa kulipiza kisasi kwa mwanafunzi hata siku moja ila nitaunga mkono hoja ya kuiwajibisha serikali hata leo asbh.
swala la serikalia kushindwa kuskiliza matatizo ya waalim linachangiwa na CWT kama hujui. umewah kuwa kiongozi hata wa cwt wa kata ukaskia mambo yalivyo??? basi usingesema haya. serikali ni mtekelezaji na kama nyie kwenye umoja wenu hakuna mnachodai kwa umoja hawawez kuwafikiria.
nenda nchi za watu utaona vyama vya wafanyaazi ndivyo vinavyotetea maslah ya wanachama wake lkn hapa kwa cwt hali sio hiyo. wao kila kitu ni ndio mzee ndio mzeee ptuuuuuuuuuuuuuuuuu
siungi na wala sitaunga mkono uhamasishaji wa kulipiza kisasi kwa mwanafunzi hata siku moja ila nitaunga mkono hoja ya kuiwajibisha serikali hata leo asbh.
What kind of mwal. are you? Unasema swala la serikari kushindwa kusikiliza matatizo ya walimu ni CWT!
Serikali iliyomakini ilitakiwa hasa kutekeleza majukumu yake hata bila pressure ya CWT kwani ni wajibu wake kusimamia hili, na mwanzo umesema CWT wanakata % tu, je serikali hawakati wafanayakazi kodi na vyanzo vingine vy mapato? Jibu ni ndiyo sasa je kwa nini isiwape walimu mahitaji na haki stahiki?
Unaongelea nguvu ya vyama vya wafanyakazi nchi za watu japo hujataja hata moja, lakini kwa Africa tuchukue mfano wa COSATU (THE CONGRESS OF SOUTH AFRICAN TRADE UNIONS) Je unafananisha mazingira ya demokrasia kwa wafanyakazi ya Afrika ya kusini na Tanz. au nchi zilizoendelea?